Shoo Gap
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 246
- 71
Nimekutana na mabinti watatu sasa waliomaliza kidato cha nne mwaka jana ambao wanafanya kazi za house girl. Mwanzoni sikuyaamini macho na masikio yangu. Siku ziliposogea na kukaa na kuzungunza nao niligundua kuwa ni sahihi wao kufanya kazi hiyo kwani uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana. Nina maana elimu ya msingi na miaka minne ya sekondari haikuwakomboa. Mimi kama mwalimu ninasikitika sana kuona jinsi ambavyo jamii na taifa wakiongozwa na waalimu tumeshindwa kuwaandaa watoto kukabiliana na changamoto za maisha. Yaani hawa niliowaona wamefeli CSEE na pia elimu ya maisha tu.
Hii ni dalili mbaya sana kwa Taifa na wadau wote wa elimu. Tunakipeleka wapi kizazi chetu cha leo? Kuna dalili zinazoonesha wazi kesho si ajabu kukuta F6 leaver au hata Graduate akitafuta kazi ya House girl, kutokana na mfumo mbovu wa elimu.
Ni lazima tuchukue hatua haraka ili wanetu, wanafunzi wetu, watoto wetu wasifikike hapa hawa mabinti walikofikia. Angalau akifeli CSEE basi awe ameelimika kukabiliana na maisha akitumia rasilimali zinazomzunguka.
Hii ni dalili mbaya sana kwa Taifa na wadau wote wa elimu. Tunakipeleka wapi kizazi chetu cha leo? Kuna dalili zinazoonesha wazi kesho si ajabu kukuta F6 leaver au hata Graduate akitafuta kazi ya House girl, kutokana na mfumo mbovu wa elimu.
Ni lazima tuchukue hatua haraka ili wanetu, wanafunzi wetu, watoto wetu wasifikike hapa hawa mabinti walikofikia. Angalau akifeli CSEE basi awe ameelimika kukabiliana na maisha akitumia rasilimali zinazomzunguka.