Nemo,
Angalau nimepata uhakika toka kwamba wewe ni mwanamke, hizi avator zinaweza kumchanganya mtu ukafikiri ndiye kumbe siye...
Sasa tuje kwenye hoja.
Cha msingi ni nini? Ndoa au kutimiza ndoto yako?
Naamini ndoa ni sehemu ya ndoto yako na wala si ndoa ndiyo ndoto yako.
Jiulize kusudi kubwa la maisha kwako ni nini? Kuolewa, hii ni sehemu tu.
Wazazi wako au jamii siilaumu kwani wengi wanafikiri ndoa ndiyo kila kitu na hata mara nyingine ukimkosa fulani na hasa kama ana kile kinachoitwa PESAAA, basi wanafunga milango yote ya kuona, kusikia , kutafakari hata kufikiri kisa mwanaume ana pesa au nafasi na sana sana wazazi au jamii wanaangalia jinsi gani jamaa anaweza kusaidia maisha yao siku za mbele.
Mwali, ushauri ni kwamba endeleza ndoto yako, kwa staha yote mueleze mwenzio juu ya hilo , kwani hutaki kuchanganya mambo na usije ukashindwa kufikia malengo yako. Naamini kama umeahirisha ndoa kwa ajili ya mambo ya msingi , hata huyo mwenzio ataliona hilo, kama halioni hilo basi tambua anaangalia kwa kutumia miwani ya kwake mwenyewe na kama yu tayari kukuvunja ili mradi akuoe kwa kutimiza lengo lake binafsi, basi hapo waweza kutambua huyu ni wa kukaa mbali naye.
Fikiria utajenga ndoa ya namna gani endapo, huyu mume anakupa ultimatum kabla ya ndoa ! Je Ukiingia kwenye ndoa itakuwaje? Kama mwenzio unampenda, basi umshirikishe katika mambo yako na yeye akushirikishe kwenye ndoto zake, kama ndoto zenu zinashabihiana basi mtajenga himaya....
Angalau nimepata uhakika toka kwamba wewe ni mwanamke, hizi avator zinaweza kumchanganya mtu ukafikiri ndiye kumbe siye...
Sasa tuje kwenye hoja.
Cha msingi ni nini? Ndoa au kutimiza ndoto yako?
Naamini ndoa ni sehemu ya ndoto yako na wala si ndoa ndiyo ndoto yako.
Jiulize kusudi kubwa la maisha kwako ni nini? Kuolewa, hii ni sehemu tu.
Wazazi wako au jamii siilaumu kwani wengi wanafikiri ndoa ndiyo kila kitu na hata mara nyingine ukimkosa fulani na hasa kama ana kile kinachoitwa PESAAA, basi wanafunga milango yote ya kuona, kusikia , kutafakari hata kufikiri kisa mwanaume ana pesa au nafasi na sana sana wazazi au jamii wanaangalia jinsi gani jamaa anaweza kusaidia maisha yao siku za mbele.
Mwali, ushauri ni kwamba endeleza ndoto yako, kwa staha yote mueleze mwenzio juu ya hilo , kwani hutaki kuchanganya mambo na usije ukashindwa kufikia malengo yako. Naamini kama umeahirisha ndoa kwa ajili ya mambo ya msingi , hata huyo mwenzio ataliona hilo, kama halioni hilo basi tambua anaangalia kwa kutumia miwani ya kwake mwenyewe na kama yu tayari kukuvunja ili mradi akuoe kwa kutimiza lengo lake binafsi, basi hapo waweza kutambua huyu ni wa kukaa mbali naye.
Fikiria utajenga ndoa ya namna gani endapo, huyu mume anakupa ultimatum kabla ya ndoa ! Je Ukiingia kwenye ndoa itakuwaje? Kama mwenzio unampenda, basi umshirikishe katika mambo yako na yeye akushirikishe kwenye ndoto zake, kama ndoto zenu zinashabihiana basi mtajenga himaya....