All about Edward Hosea, Mwanyika

Asante sana kwa uchangiaji wenu,unaoruhusu hoja pinzani nazo kujikita mahala,mie nauita ni "open minded thinking".
Kwenye ile taarifa ya kamati kuna mambo mengi sana na ndio maana waziri mkuu hata kaunda kamati nyingine kupitia yale mapendekezo na kuona ni jinsi gani yanatekelezeka bila kuathiri haki za watu au kuwaonea wengine. Kikubwa kilichobainika na kamati ya mwakyembe ni ukiukwaji wa wazi wa taratibu za tendering uliofanywa na wizara,maafisa wake na kitu kinachoonekana kama shinikizo la waziri mkuu. Ukiukwaji wa taratibu huo kwa wenyewe sio rushwa tena kisheria unafall katika administrative law,bali umebeba pia mambo mengine kibao yanayoibua masuala mengine ya kisheria. Point kubwa hapa ni ukiukwaji wa sheria ya tendering na kutofanya due diligence ambayo inategemewa kwa reasonable man wa calibre ya AG,na maafisa wa wizara.
Ukiukwaji kama huu kwa kawaida adhabu zake zipo administratively sio judiciary.Adhabu zao ni kama kushushwa vyeo,kuhamishwa vitengo kwani vile walivyopo sio competent n.k.Sasa HOSE yeye anakuja wapi? Kila mtu katika ile ripoti anasehemu yake aliyochangia kama ni nengligence tunasema contributory negligence.
Kama walivyo wengine HOSEA sehemu inayomgusa ni hii:
Ukisoma kifungu cha 6 cha sheria hiyo ya zamani kinasema kwamba
mtu yeyote ambaye kwa kujua atampa wakala, au wakala yeyote kwa kujua atatumia kwa lengo la kumdanganya mkuu wake, risiti,akaunti au hati au nyaraka yoyote inayohusiana na mambo au shughuli yoyote ya mkuu wake wa kazi na ambayo ina taarifa feki,za kughushi au zilizopotoshwa na kwa jinsi yoyote ile zina lengo la kumdanganya mkuu,atakuwa ametenda kosa.mwisho wa kunukuu.

Sawa Hosea hakuona rushwa,je hakuona pia kipengele hiki cha sheria? je katika mkatba wa richmond hakukuwa na nyaraka feki zenye lengo la kumpotosha mkuu,je kusema kwamba richmond ina ubia na kampuni ile waliyoitaja na kuthbitisha hilo kwa business kadi hakukuwa na lengo la kumpotosha mkuu?je,ukweli kwamba richmond haikuwa mtu kisheria yaani sio kapuni halali kwa kuwa inakosa usajili tanzania na huko USA haipo na kwamba hata kama ilisajiliwa hapa nchini usajili wake haukuwa halali kwa kuwa hatuna one man company kwa mujibu wa kifungu cha tatu,moja cha sheria ya makampuni.je,waliohusika hawakuwa na lengo la kumpotosha mkuu?


Hapa tu,akiclear hapa anapeta,mi ningekuwa wakili wake ningejikita kutafuta defense mahali hapa zaidi,kwani sehemu nyingine zote za sheria namba 16 yupo clean.Hatuna sheria ya harufu wala moshi wa rushwa.Neno harufu au moshi wa rushwa linatokana na sheria ya ushahidi ya ya mwaka 1967 nadhani THE LAW OF EVIDENCE ACT,kifungu cha 3 hadi 15 kinachozungumzia circumstancial evidence, Circumstancial evidence ndio inayounda mazingira au harufu ya tukio la rushwa. Ndio maana nikasema hata katika kesi ya balozi mahalu inayoendelea hakukuwa na rushwa ya moja kwa moja kesi imeenda mahakamani on circumstantial evidence.Na kesi za namna hii huwa ngumu sana kuliko zile za kumshika mtu papo kwa hapo.
Hayo yote ya kamati kuwataja watuhumiwa au la sioni kama ni msingi sana kwa mhe.Hosea ambaye namheshimu sana kama mwalimu wangu somewhere.Ila ni wazi wenzie hata kama wana hila mbaya naye wanataka kumkamatia hapa.Ningeomba mtu mwenye ripoti ya HOSEA atumwagie hapa ile tuweze kujadili vizuri zaidi kwa kuilinganisha na findings za mwakyembe.

Hiyo sheria tunaijua kaka, tatizo ni kwamba soma HOJA ZA SANDE kwanza utupe majibu.

Ushahidi wa kamati ya MWAKYEMBE na majina ya wanaotuhumiwa kwa rushwa ili waende mahakamani.

Hatuhitaji maoni ya watu bali zingatia hayo kwanza.
 
Kwa mantiki hii mimi na wadau wengine ndio maana tunashawishika kukubali kuwa Mhe.HOSEA anawajibika katika sakata hili la Richmond unless aje na maelezo ya kuridhisha zaidi lakini sio kujibu wadau kwa jazba.

wana JF, nimepitia hoja hii nzito kuhusu HOSEA, lakini TAARIFA ya MWAKYEMBE imetuacha SOLEMBA. Kwa sababu haijawataja watuhumiwa ili tuwajue na ushahidi wa kuwa na hisa katika RICHIMOND.

Inaonekana Mwakyembe anamuogopa LOWASSA ndiyo maana kamsafisha mwishoni, SIASA NI MCHEZO MCHAFU. Kwa nini nasema hivyo?, kwa sababu:-
1. Hosea anaweza kutuzidi maarifa akituomba tumpe kifungu cha Sheria Na. 16 ya kuzuia rushwa kinachohusu HARUFU YA RUSHWA, MAZINGIRA YA RUSHWA na Mkataba mbovu.
2.Mwakyembe amekanusha kumtaja ROSTAM AZIZ, sasa nani atamsaidia Hosea kutaja watuhumiwa,
3.Ukurasa wa 18 wa taarifa ya Mwakyembe umeelezea vipengele vitano katika taarifa ya HOSEA kama ifuatavyo:-
-Mchakato wa kumpta Mzabuni ulikuwa wa wazi na ushindani:

Kamati ya Mwakyembe ingejua kuwa Wizara ya madini ina uwezo
kisheria kusimamia mchakato wa manunuzi kwa niaba ya TANESCO
kwa kuwa ni wizara moja, hata Wizara nyingine ingefanya kazi
hiyo kama haja ipo ya kufanya hivyo.

-Hakuna ushahidi uliopatikana kuthibitisha vitendo vya
Rushwa,.... Pia hakuna ushahidi uliopatikana wa afisa yeyote
serikalini kumiliki hisa au madaraka katika Richmond....

Tume ya Mwakyembe imetuletea majungu ambayo hayawezi
kutusaidia kuwapeleka watuhumiwa mahakamani. Tume ina jukumu
la kumsaidia Hosea kupambana na rushwa kwa kuwa ni janga la
kitaifa, ushahidi wa kisheria unapokosekana, uwajibishaji wa
kisiasa, kiutawala unaweza kutumika kupunguza kasi ya rushwa.

Labda TUME ingependekeza HOSEA awekewe kipengele cha sheria
itamruhusu kushughulikia kuwawajibisha watuhumiwa kwa HARUFU
ZA RUSHWA AU MAZINGIRA YA RUSHWA!

Kwa kasi ya Hosea akipewa nafasi ataua watu kwa pressure!

-Kamati maalumu iliyoundwa haikupata muda wa kutosha kuifanyia
uchambuzi kampuni ya RICHMOND...

Huo ni udhaifu mkubwa ambao TAKUKURU waligundua na kwa
udhaifu huu matokeo mabaya yalianzia hapa.

Kwa hiyo atafutwe aliyepaswa kurekebisha kasoro zinazotokana
na kamati iliyoundwa na LOWASSA, MSABAHA AU KARAMAGI!

-Utafiti wa kina haukufanywa kutambua uwezo wa
kampuni .....Richmond ....!

TAKUKURU walitimiza wajibu wao wa kuishauri serikali katika
hili, wasingeweza kuanzisha kesi mahakamani bila kuwa na
ushahidi na watuhumiwa.

TUME itupe majina halisi ya watuhumiwa wa RUSHWA na siyo
SIASA!

-Mapungufu machache yaliyokuwepo lakini ni ya 'kawaida
kiutendaji' na hayakuhusisha rushwa au .....

Tume ya MWAKYEMBE iliegemea kipengele hiki, ikumbukwe kauli
hii inayotolewa kwenye vyombo vya habari ni UFUPISHO wa
maelezo marefu na mengi mno ukimpa nafasi mhusika kujieleza!

HATA hivyo sisi wataalam wa habari tunajua kuwa HOSEA ana maadui wengi nje(hata baadhi ya wabunge) na ndani ya TAKUKURU tukianzia na msaidizi mkuu wa Hosea (Lilian Mashaka) hutuuzia habari nyeti, lakini wakati wa TUME hii kulikuwa na mawasiliano ya karibu sana Dr. Mwakyembe, wakati sisi wataalam tunaijua picha yote!

Mwakyembe, Lilian Mashaka, awadhi Mohamed na wengine tumewahifadhi tupeni majina ya watu gani wapelekwe mahakamani?

Pia TUME itoe kila kifungu cha sheria iliyokiukwa na kila mtuhumiwa kwa kuwa ina wataalam wa sheria waliobobea, mtaani tumeikosa sheria inayotokana na maoni yao.

NAIPONGEZA TUME KAMA HARUFU ZA RUSHWA UWAJIBISHAJI WAKE UWE NI WA KIUTAWALA NA KISIASA kila tunapokosa ushahidi wa kina. Pia kukosa ushahidi wa moja kwa moja iwe ni mwanzo wa tume kama hii kusaidia kupiga vita rushwa!

SANDE[/QUOTE]

Ndugu yetu mwanaJF naona hoja yako imetuchanganya kidogo tupe data za ziada kama zipo, naona watu wanaizunguka hoja yako, why, kwa nini?
 
Asante sana kwa uchangiaji wenu,unaoruhusu hoja pinzani nazo kujikita mahala,mie nauita ni "open minded thinking".
Kwenye ile taarifa ya kamati kuna mambo mengi sana na ndio maana waziri mkuu hata kaunda kamati nyingine kupitia yale mapendekezo na kuona ni jinsi gani yanatekelezeka bila kuathiri haki za watu au kuwaonea wengine. Kikubwa kilichobainika na kamati ya mwakyembe ni ukiukwaji wa wazi wa taratibu za tendering uliofanywa na wizara,maafisa wake na kitu kinachoonekana kama shinikizo la waziri mkuu. Ukiukwaji wa taratibu huo kwa wenyewe sio rushwa tena kisheria unafall katika administrative law,bali umebeba pia mambo mengine kibao yanayoibua masuala mengine ya kisheria. Point kubwa hapa ni ukiukwaji wa sheria ya tendering na kutofanya due diligence ambayo inategemewa kwa reasonable man wa calibre ya AG,na maafisa wa wizara.
Ukiukwaji kama huu kwa kawaida adhabu zake zipo administratively sio judiciary.Adhabu zao ni kama kushushwa vyeo,kuhamishwa vitengo kwani vile walivyopo sio competent n.k.Sasa HOSE yeye anakuja wapi? Kila mtu katika ile ripoti anasehemu yake aliyochangia kama ni nengligence tunasema contributory negligence.
Kama walivyo wengine HOSEA sehemu inayomgusa ni hii:
Ukisoma kifungu cha 6 cha sheria hiyo ya zamani kinasema kwamba
mtu yeyote ambaye kwa kujua atampa wakala, au wakala yeyote kwa kujua atatumia kwa lengo la kumdanganya mkuu wake, risiti,akaunti au hati au nyaraka yoyote inayohusiana na mambo au shughuli yoyote ya mkuu wake wa kazi na ambayo ina taarifa feki,za kughushi au zilizopotoshwa na kwa jinsi yoyote ile zina lengo la kumdanganya mkuu,atakuwa ametenda kosa.mwisho wa kunukuu.

Sawa Hosea hakuona rushwa,je hakuona pia kipengele hiki cha sheria? je katika mkatba wa richmond hakukuwa na nyaraka feki zenye lengo la kumpotosha mkuu,je kusema kwamba richmond ina ubia na kampuni ile waliyoitaja na kuthbitisha hilo kwa business kadi hakukuwa na lengo la kumpotosha mkuu?je,ukweli kwamba richmond haikuwa mtu kisheria yaani sio kapuni halali kwa kuwa inakosa usajili tanzania na huko USA haipo na kwamba hata kama ilisajiliwa hapa nchini usajili wake haukuwa halali kwa kuwa hatuna one man company kwa mujibu wa kifungu cha tatu,moja cha sheria ya makampuni.je,waliohusika hawakuwa na lengo la kumpotosha mkuu?


Hapa tu,akiclear hapa anapeta,mi ningekuwa wakili wake ningejikita kutafuta defense mahali hapa zaidi,kwani sehemu nyingine zote za sheria namba 16 yupo clean.Hatuna sheria ya harufu wala moshi wa rushwa.Neno harufu au moshi wa rushwa linatokana na sheria ya ushahidi ya ya mwaka 1967 nadhani THE LAW OF EVIDENCE ACT,kifungu cha 3 hadi 15 kinachozungumzia circumstancial evidence, Circumstancial evidence ndio inayounda mazingira au harufu ya tukio la rushwa. Ndio maana nikasema hata katika kesi ya balozi mahalu inayoendelea hakukuwa na rushwa ya moja kwa moja kesi imeenda mahakamani on circumstantial evidence.Na kesi za namna hii huwa ngumu sana kuliko zile za kumshika mtu papo kwa hapo.
Hayo yote ya kamati kuwataja watuhumiwa au la sioni kama ni msingi sana kwa mhe.Hosea ambaye namheshimu sana kama mwalimu wangu somewhere.Ila ni wazi wenzie hata kama wana hila mbaya naye wanataka kumkamatia hapa.Ningeomba mtu mwenye ripoti ya HOSEA atumwagie hapa ile tuweze kujadili vizuri zaidi kwa kuilinganisha na findings za mwakyembe.


Mkuu Augustoos, samahani sikusoma vizuri hoja yako mwishoni nikaelewa tofauti. Sorry, kwa kutokukuelewa please!
 
Kutumia madaraka yako kupata Tender ya serikali sio kosa wala Rushwa hata kidogo na sheria za Azimio zinawa protect zaidi..
MAZINGIRA YANAASHIRIA RUSHWA NA HUYU HOSEA NDIO ANGA ZAKE HIZO maana amefanya Ph.D Law: Mapambano dhidi ya Rushwa nchini Tanzania: Nguvu ya Ushahidi wa Mazingira
 
Nashindwa kumuelewa HOSEA
Jamani wanajf humu ndani inaonesha kuna wanasheria wengi sana tena waliobobea ikibidi zaidi ya mwakyembe na Hosea,ndio maana hii mijadala labda haiishi,lakini pamoja na hayo siasa na misukumo binafsi nayo imetuelemea mno kiasi saa nyingine tunashindwa kutoa hoja na badala yake tunang'ang'ania misimamo yetu. Aliyemwanazuoni atakubaliana nami kuwa lazima akubali kupingwa na katika kufanya hivyo hoja yoyote anayoitoa anaitoa akiwa na open mind huku akielewa kuwa wapo watakaompinga wapo watakaomkubali na pia wapo watakaotaka kuelimishwa zaidi.Lakini katu hatowachukia wanaompinga kwani nao wanahoja zao shindani.

Baada ya kusema hayo,sasa narudi kwa HOSEA.Mhe. HOSEA wakati anachunguza sakata la Richmond alikuwa akitumia sheria namba 16 ya mwaka 1971 kadiri ilivyofanyiwa marekebisho kwa vipindi toauti.Vilevile wakati HOSEA nachunguza kuhusu sakata la balozi Mahalu vilevile alikuwa akitumia sheria hii hii. Makosa yote haya mawili yalihusisha viongozi wa serikali kwa upande mmoja na watu binafsi au makampuni yaliyoko nje ya nchi. Na katika makosa yote hayo mawili yaliyoiingoza hasara nchi yetu hakuna aliyewahi kushikwa red handed akiomba,au kupokea rushwa. Yote yanahusisha ushahidi wa kimazingira tu. Makosa yote mawili pia hayahusishi rushwa tu bali pia uhujumu uchumi.

Hivi karibuni Hosea amesikika kwenye vyombo vya habari akisema,yeye kazi yake ni rushwa na kwamba alifanya kazi kwa mujibu wa sheria ya rushwa ya mwaka 1971 ilivyokuwa,hivyo kazi yake si miktaba wala uhujumu uchumi. Jibu hili linafanana sana na alilolitoa mwanyika wakati anahojiwa na kamati ya mwakyembe. Swali hapa je,uhujumu uchumi na mikataba ni kazi ya nani? si makusudi yangu kujibu swali hili leo hapa,bali kuangalia uhalali wa kauli za HOSEA kuhusu wajibu wake kwa masuala yote hayo mawili hapo juu.
TAKURU ya zamani iliundwa kwa mujibu wa kifungu cha tatu cha sheria ya rushwa mwaka 1971 ikiwa na majukumbu yafuatayo,hapa nitanukuu
1.TO take necessary measures for the prevention of corruption in the public,parastatals and private sector.
2.To investigate and prosecute offences under the Act and other offences involving corrupt transactions.
3.Advise the governement and other parastatals organization on the ways and means to prevent corruption.
Sheria pia inaendelea kusema kuwa wakati wakitekeleza majukumu yao,watakuwa na mamlaka ya kipolisi sawa na askari mwenye cheo cha ASP.Hivyo kwa ufupi hizo ndizo kazi zao. Ukiangalia kwa haraka haraka tu utakuta kwa kauli za hosea,haguswi na richmondi kwani labda alishafanya kila jinsi kuzuia rushwa,pili alishachunguza akakuta hakuna rushwa ya moja kwa moja na tatu aliishauri serikali kwamba iendelee tu na richmond kwani hakua rushwa na haipati hasara yoyote.
Hivi kusema serikali inapata hasara au haipati ilikuwa ni kazi yake? hiyo kazi inafall wapi kati ya hizo kazi tatu kuu hapo juu? naam labda alisema kwakuwa hizo zilikuwa hadidu za rejea za uchunguzi wake. Lakini mimi naenda mbali zaidi.

Ukisoma kifungu cha 6 cha sheria hiyo ya zamani kinasema kwamba
mtu yeyote ambaye kwa kujua atampa wakala, au wakala yeyote kwa kujua atatumia kwa lengo la kumdanganya mkuu wake, risiti,akaunti au hati au nyaraka yoyote inayohusiana na mambo au shughuli yoyote ya mkuu wake wa kazi na ambayo ina taarifa feki,za kughushi au zilizopotoshwa na kwa jinsi yoyote ile zina lengo la kumdanganya mkuu,atakuwa ametenda kosa.mwisho wa kunukuu.

Sawa Hosea hakuona rushwa,je hakuona pia kipengele hiki cha sheria? je katika mkatba wa richmond hakukuwa na nyaraka feki zenye lengo la kumpotosha mkuu,je kusema kwamba richmond ina ubia na kampuni ile waliyoitaja na kuthbitisha hilo kwa business kadi hakukuwa na lengo la kumpotosha mkuu?je,ukweli kwamba richmond haikuwa mtu kisheria yaani sio kapuni halali kwa kuwa inakosa usajili tanzania na huko USA haipo na kwamba hata kama ilisajiliwa hapa nchini usajili wake haukuwa halali kwa kuwa hatuna one man company kwa mujibu wa kifungu cha tatu,moja cha sheria ya makampuni.je,waliohusika hawakuwa na lengo la kumpotosha mkuu?
Watu wote waliokuwa wakideal na richmond walikuwa wanajua nini kinachoendelea toka mwanzo hadi mwisho,na ukweli wote hapo juu walikuwa wanaujua je,hakuwa na nia ya dhati ya kumpotosha mkuu? ili aingie mkataba na mtu asiyekuwepo(yaani fictitious person?) Hosea hili hakuliona kabisa? Kama hakuliona anatofautiana vipi na sisi walei(laymen) wa taaluma ya kuchunguza rushwa? basi ameprove incomptence kwenye taasisi yake iwapo atashindwa kuthibitisha hili.Basi uchunguzi wake ulijikita kwenye nini? yaani ni vitu gani alivyoviangalia hadi akaandika ripoti?
Je,kama vigezo hivyo hapo juu havikwepo kwa maana kwamba kampuni ilitoa nyaraka feki juu ya uwepo wake kisheria na maafisa wetu wakavipokea na kumwaminisha mkuu ili anendelee kuingia mkataba je,hakukuwa na harufu ya rushwa iliyowapofusha maafisa wetu wasiweze kuchunguza zaidi juu ya uwezo wa richmond kisheria na kama je,imetimiza masharti yote ya sheria za tanzania?Mbona ukisoma mkataba wa richmodn maafisa wetu wanasaini kabisa kauli zao kwamba wameridhika richmondi ni kampuni halali kisheria na haijavunja sheria yoyote ya tanzania,wakati kwa hakika imevunja sheria ya makampuni na sheria ya mikataba ya mwaka 1961.

Sawa Hosea atasema yote haya si kazi yake na hayakuwamo Richmondi. Ok,si kazi yake ndiyo lakini jaji mmoja kwenye kesi ya Donoghue v,stevenson[1932]QB aliwahi kusema "....iwapo tutakwenda hatua moja kwanini isiwe hamsini?" HOSEA alifikiaje uamuzi wa kumshitaki balozi mahalu? alijuaje kuwa pale kuna mkono wa rushwa wakti mazingira yake yalikuwa swa na richmond? Ni kwanini HOSEA alitumia kifungu cha sita katika suala la mahalu kumtia mahalu hatiani wakti kwenye richmond hakukitumia?ilikuwaje katika mashtaka ya mahalu Hosea huyohuyo akamchaji pia balozi mahalu na uhujumu uchumi pamoja na wizi kama mtumishi wa umma kwa mujibu wa sheria ya kanuni ya adhabu(pena code cap16) na pia sheria ya rushwa 1971,wakati kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1971 hakuwa na mamlaka ya kuestablish makosa hayo?

Mamlaka ya kuchaji mahalu kwa kutumia penal code na Economic and organised crimes control Act aliyapata wapi.Hivyo basi kama aliweza kwenye hili la mahalu tultegemea aweze pia kwenye richmond kwani kanuni za haki zinasema "justice must not only be done but must be seen to be done" na katiba yetu intambua equality before the law. Ni kutokana na mashaka haya niliyoataja hapo juu ndio maana mhe. Hosea anatuhumiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine kwenye sakata la richmond kwa kuufumbia macho uovu wa wazi.
Na kama mwanazuoni? utafiti wowote unasehemu ya hitimisho na mapendekezo,ambayo tulitegemea hosea aseme,pamoja na kuwa kazi yangu si kuangaliwa mikataba na masuala ya uhujumu uchumi,lakini katika utafiti wangu au uchunguzi nimegundua mapungufu yafutayo kwenye mkataba wenyewe na kwenye uhalali wa kampuni ya richmond kisheria ambao napendekeza ziundwe tume maalumu zenye mamlka ya kuchunguza uhalali wa mkataba huu nk.ili kujiridhisha zaidi. Hapa angekuwa safe,lakini yeye alikana kabisa na kusema mchakato wote ulizingatia sheria na ulienda kwa kufuata vipengele vyote wala hakuna harufu ya rushwa na wala hatupati hasara.mmh HOSEA ulienda mbali mno uliposema vipengele vyote vya sheria vilifuatwa je,na kanuni za manunuzi zinazosema tenda itangazwe siku 45 na wao wakatangaza siku kumi je,huko kulikuwa ni kufuata sheria? au ripoti ya PPRA hakuiona?

Kwa mantiki hii mimi na wadau wengine ndio maana tunashawishika kukubali kuwa Mhe.HOSE anawajibika katika sakata hili la Richmond unless aje na maelezo ya kuridhisha zaidi lakini sio kujibu wadau kwa jazba.

........hayo ndio mambo niliyokuwa nasema

....salute Augustoons and God Bless!!
 
Kuhusu TUKURU kila siku tunasema hii TUKURU ni kama mbwa kibogoyo na kwa kwa vile hana meno hawezi kuuma mtu. Halafu tena TUKURU iko chini ya rais mwenyewe sasa mbwa gani amabye anatabia ya kumuuma bwana wake?

Kama rais atahusishwa na ufisadi wowote basi utakuwa ni ule wa mikataba ya Madini kwa vile hapo awali alikuwa ni Waziri wa Nishati na Madini. Ndio maana mawaziri wengine wa zamani walifanya kisingizio kwamba wamelitumikia taifa kwa muda mrefu na sasa wanataka kupumzika. Baadhi ya hao waliopumzika huwenda wakatajwa kwenye skashfa ya mitataba ya Madini.

Tume ya Bunge kuhusu Richmond imeandika waziwazi kwamba TUKURU haikuchunguza inavopaswa na walisema owongo.Hosea mwenyewe anakiri kwamba kuchunguza vigogo si kazi rahisi, Nadhani hapa alipo ona jina la waziri mkuu wa zamani na uhusiano wake na Richmond ndio hapo TUKURU ikaandika ripoti ya uwongo.Kitendo hiki pia kinafanya kuwe na tuhuma za Rushwa kwani ni nani aliyefanya TUKURU iseme uwongo?

Waziri Mkuu mpya ataunda task force amabayo utafuatilia mapendekezo yote yaliyofanywa na tume ya Dr.Mwakyembe. Task force hii ndio ambayo itaandaa kazi ya kuwapeleka watuhumiwa mahakamani. Majina matatu tunayo lakini watuhumiwa ni wengi sana kwani kazi ya mafisadi ilikuwa ni ya kiina kikubwa mno.

Lowasa alitakiwa alieleze taifa kupitia Bungeni ni kitu gani alichofanya na mambo gani yalitokea katika mkutano wa baraza la mawaziri ambalo liliamua Richmond ipewe contract. Mpaka sasa hivi watanzania hatujaelezwa undani wa jambo hili.

Hapa ni kwamba serikali yote pamoja na rais Kikwete inahusika kwa kuwakosesha watanzania umeme wakati ule wa kiangazi. Sasa hapa Kikwete hawezi kujiepusha na kumtupia mpira wote Lowasa. Yeye pia amefanya makosa kwani hakuchukua hatua zinazostahili haraka na baadaye aliiweka nchi yote gizani kwa muda mrefu.

TUNAZIHISABU SIKU ZAKE CHACHE ZILIZOBAKIA KAMA RAIS WA TANZANIA.
 
Wadau naomba niwakumbushe kitu,katika kufanya huu mjadala pia hebu tusisite kujiuliza kwamba mbali ya hseria ya kutangaza tenda siku 45 kukiukwa na utaratibu mzima wa tendering,je,ni kwa nini labda kampuni ambayo kila iliposhindanishwa na kampuni nyingine ilionekana ya mwisho ndiyo ikapewa tenda ya kuzalisha umeme?mmh yaani mnapiga pepa halafu wa mwisho au wale watu wa tatu mwishoni ndio wanaingizwa kwenye mchakato kwa kuchaguliwa kuingia kidato cha tano wale wenye division one au two wanaachwa kwamba hawafai?Ipi ni tafsiri ya jambo hili? jamani mambo mengine magumu,lakini wadau wa jf nawaaminia mnaweza kudadavua.Kwa uelewa wa kinadharia kamati zote mbili ya HOSEA NA MWAKYEMBE hazikuweza kugundua waziwazi uwepo wa rushwa na kwa sheria ya mwaka 1971 hakuna rushwa.Swali gumu pale ni je,ipi tafsiri ya ukiukwaji ule wa sheria?ni kwa nini mtu anayefeli ndio apewe tenda,ni kwa nini siku 10 badala ya 45,ni kwa nini baadhi ya watu walikuwa concerned sana hata kama hawahusiki,tafsiri yake ni nini?mimi na wewe hatujui hapa hasa ndipo panahitajika utafiti zaidi.
Kwa uanazuoni wangu naona makosa mengi hapa ni ya kutowajibika zaidi kuliko rushwa.Watu hawakuwa responsible kwenye vitengo vyao,walizembea mno,walipuuzia majukumu yao hata kama hawakupokea senti tano ya mtu. Mtu unapokosa kutimiza wajibu wako kisheria mf.polisi aliyepewa kazi ya kulinda benki,yeye akasimama tu pale mbele ya benki,wezi wakapitia upande wa nyuma wakavunja benki na kuiba bila yeye kujua,anawajibika kisheria japo usiku mzima alikuwa macho hakulala wala kusinzia hata tone. .
Kwa kuwa wajibu wake kisheria unamtaka asiishie tu kuwa macho na kushika silaha bali atumie uwezo wake wote na ujuzi aliosomea kuhakikisha anashtuka hata kudondoka kwa jani la mti tu,asipuuze kwani hicho chaweza kuwa kishindo cha mruka ukuta.Hosea hakukuta rushwa hata ningekuwa mimi nisingeona rushwa pale labda,kinachomning'iniza huyu ni conclusion zake.Au kama kweli wabunge wanavyosema ripoti aliyoitoa kwa umma haikuwa hata na tarehe na kwamba haikuwa yenyewe,original aliificha hilo suala ni gumu sana,ndio maana naomba sana wadau hebu tupatieni hiyo ripoti aliyoitoa hosea hapa tuidadavue ili tuone kama twaweza kumsulubu kiasi gani au kumclear.Na tutafanya hivyo tu kwa kuangalia hadidu zake za rejea na wajibu wake kisheria.
 
Wadau naomba niwakumbushe kitu,katika kufanya huu mjadala pia hebu tusisite kujiuliza kwamba mbali ya hseria ya kutangaza tenda siku 45 kukiukwa na utaratibu mzima wa tendering,je,ni kwa nini labda kampuni ambayo kila iliposhindanishwa na kampuni nyingine ilionekana ya mwisho ndiyo ikapewa tenda ya kuzalisha umeme?mmh yaani mnapiga pepa halafu wa mwisho au wale watu wa tatu mwishoni ndio wanaingizwa kwenye mchakato kwa kuchaguliwa kuingia kidato cha tano wale wenye division one au two wanaachwa kwamba hawafai?Ipi ni tafsiri ya jambo hili? jamani mambo mengine magumu,lakini wadau wa jf nawaaminia mnaweza kudadavua.Kwa uelewa wa kinadharia kamati zote mbili ya HOSEA NA MWAKYEMBE hazikuweza kugundua waziwazi uwepo wa rushwa na kwa sheria ya mwaka 1971 hakuna rushwa.Swali gumu pale ni je,ipi tafsiri ya ukiukwaji ule wa sheria?ni kwa nini mtu anayefeli ndio apewe tenda,ni kwa nini siku 10 badala ya 45,ni kwa nini baadhi ya watu walikuwa concerned sana hata kama hawahusiki,tafsiri yake ni nini?mimi na wewe hatujui hapa hasa ndipo panahitajika utafiti zaidi.
Kwa uanazuoni wangu naona makosa mengi hapa ni ya kutowajibika zaidi kuliko rushwa.Watu hawakuwa responsible kwenye vitengo vyao,walizembea mno,walipuuzia majukumu yao hata kama hawakupokea senti tano ya mtu. Mtu unapokosa kutimiza wajibu wako kisheria mf.polisi aliyepewa kazi ya kulinda benki,yeye akasimama tu pale mbele ya benki,wezi wakapitia upande wa nyuma wakavunja benki na kuiba bila yeye kujua,anawajibika kisheria japo usiku mzima alikuwa macho hakulala wala kusinzia hata tone. .
Kwa kuwa wajibu wake kisheria unamtaka asiishie tu kuwa macho na kushika silaha bali atumie uwezo wake wote na ujuzi aliosomea kuhakikisha anashtuka hata kudondoka kwa jani la mti tu,asipuuze kwani hicho chaweza kuwa kishindo cha mruka ukuta.Hosea hakukuta rushwa hata ningekuwa mimi nisingeona rushwa pale labda,kinachomning'iniza huyu ni conclusion zake.Au kama kweli wabunge wanavyosema ripoti aliyoitoa kwa umma haikuwa hata na tarehe na kwamba haikuwa yenyewe,original aliificha hilo suala ni gumu sana,ndio maana naomba sana wadau hebu tupatieni hiyo ripoti aliyoitoa hosea hapa tuidadavue ili tuone kama twaweza kumsulubu kiasi gani au kumclear.Na tutafanya hivyo tu kwa kuangalia hadidu zake za rejea na wajibu wake kisheria.

Wana JF
ushauri wa Augustoons nauunga mkono, taarifa original ya Hosea ipatikane mapema.

Tatizo ninaloona hivi sasa, itakuwa ni vigumu kupata habari kwa sasa kwa kuwa baadhi ya wana JF wametoa siri ya njia walizotumia kupata taarifa na data za TAKUKURU, ulinzi wa nyaraka utakuwa mkubwa.

Tutoe subira, lakini wenye uwezo wa kupata hiyo taarifa 'original' inayosemwa ya Hosea waitoe.

Hata hivyo Mwakyembe anapaswa kulaumiwa kwa kuwa alikuwa na jukumu la uchunguzi na TAKUKURU wakati huo alikuwa na watu wake waliotajwa hapo juu na SANDE, angemtuma LILIAN MASHAKA au AWADH MOHAMED ili waipate hiyo document!

Hata hivyo kama ipo tutaipata tu.


Mome
 
Nina wasiwasi hii thread ni mtu mmoja mwenye majina zaidi ya moja anajitahidi kumsafisha mtu.
 
The Bank of Tanzania Saga - The Asian Link We the Asian Community now living in Canada, have been making a follow up of what is happening in our beloved mother country, Tanzania. Problems facing our country range from being political, social and economical, but the underlaying cause of all these problems are CORRUPTION. We have discovered that it's corruption that is "eating" Tanzania and all efforts being made by the Prevention and Control of Corruption Bureau (PCCB) has failed.In our opinion, the fight against Corruption will only be successful if the right person is appointed to head the Bureau. Here we have a person going by the name of Edward Hosea, the current Director General of PCCB. Mr. Hosea is the right handyman of Martern Lumbanga the former Chief Secretary. All Lumbanga's property is taken care of by Mr. Hosea, whom in the eyes of those who appointed him considers him as being "Clean." This is the opposite, and he might be the dirtiest man than most Tanzanians tend to believe! Since one Jitesh Ladwa a highly indebted businessman circulated an email message all over the world on what has become to be known, the "BOT Scam" Mr. Hosea has turned to be a nuisance to businessmen and investors in Tanzania. Being a close friend to Mr. Ladwa, Hosea has been contracted by Ladwa to make sure that all those mentioned in those email messages are taken to task including prosecution. The trick, of which we know, is to make sure the current BOT Governor Mr. Daudi Ballali and some Asian businessmen are taken to court and a new Governor is appointed. The complete deal would see Hosea getting paid Tsh 1 billion! Hosea has initiated a dirty campaign full of threats whereby he moves from one bank to the other requesting banks' authorities to furnish him with bank statements of some of the businessmen. These businessmen are summoned and given a condition of giving huge money to him or face corruption charges. Surprisingly, these bank statements, believed to be top secret are exposed in different areas in Dar es Salaam including bars and hotels. Some of the bank statements have been spotted at places like pubs and bars! Hosea, who's said to be a devoted Christian who goes to church every Saturday, has sent his wife Sarafina and children Magembe and Shoma to the US on forged documents. His wife is being paid about $9,500 per month. (All documents with regard to this scandal are available).It's no secret that Hosea also owns a house in the US. This is the man who is supposed to be in the forefront fighting corruption. Recently, Hosea received a lot of money from Barrick Gold as an inducement to interfere a Court Case. It's Barrick who have built him a multibillion house at Mbezi Beach. The house is in three plots where you meet eight (eight??) dogs on guard and bills settled by PCCB. It's the same Hosea who is fully involved in Prof Mahalu's case, and that's why there are two conflicting reports on Mahalu's investigation report. One prepared by Hosea himself and the other by PCCB. Hosea, who's at the payroll of Mohamed Enterprises Ltd has caused Tanzanians to suffer a lot following his failure to investigate a multibillion fertilizer scandal involving the company. The outcome was the decision by the Japanese government to cancel a fertilizer grant to Tanzania. The same Hosea is sitting on another big scandal involving the same company.Recently, Mohammed Enterprises imported hundreds of tones of sugar which was declared that it was meant for the Democratic Republic of Congo (DRC). But TRA discovered later that the huge consignment of sugar was for the Tanzanian local market. TRA decided to impound the sugar, and reports have it that the matter "was recently settled" by some government officials, PCCB team and TRA officials after the importer, Mohammed Enterprises Ltd agreed to give away Tsh 500 million. The matter was reported to almost all media houses, but the story is not coming out because editors and reporters were "paid" millions so that they can contain the scandal. Recent news have it that already the matter had been solved "amicably" whereby Hosea and some TRA officials have been paid millions to cover the would be Tanzania's biggest scandal for 2007! Memories are still fresh in most Tanzanians especially the media fraternity when Hosea, engineered the arrest and prosecution of the editor of Family Mirror, one Zephania Musendo on arranged and calculated plan aimed at silencing him from publishing stories on Hosea's unethical behaviour. The Family Mirror was carrying stories of complaints from many people whom after being charged by the then Prevention of Corruption Bureau (PCB) were forced by Hosea to hire his law firm. The then PCB Director General (rtd) Brig General Kamazima had warned Hosea that having a law firm that was giving service to those charged by the PCB was unethical because of conflict of interest, but as of now most of those charged by PCB are forced to use the services of Hosea's Law firm! We were also victims of this arrangement.What's interesting in Hosea's bid to fight corruption is the style he applies. Although he's conducting investigations on the BOT scandal, we have never heard of many Asians being interrogated. Hosea's victims are only black Tanzanians and they are the ones he wants to sacrifice, Tanzanians watch out believe from me Planted Black Tanzania on the BOT scam will be the ones to be implicated. Why? Jitesh Ladwa, a close friend of Hosea and the author of ALL emails in relation to the so-called BOT Scam was in the past a major beneficiary of the EPA Account.On March 7th, 2005, he applied for a Deed of Assignment and Indian Ocean Hotels Expansion Project. He wrote to the Bank of Tanzania saying that he had purchased Commercial Debt of Itochu Corporation of Japanese Yen 1,078,439,516 from Itochu Corporation formerly known as C. Itoch and Company Ltd. According to the "executed" Deed of Assignment of Commercial Debt said to have been signed by Hiroyuki Sogabe on behalf of Itochu Corporation and Jitesh Ladwa on behalf of Indian Ocean Hotels Ltd its (Itochu's) address is Africa Re Centre, 6th Floor, Hospital Road, Upper Hill, P.O. Box 30288, Nairobi, Kenya. The Deed was executed on December 7th, 2004. Mr. Jitesh told the Bank of Tanzania that he intended to utilize the funds for the expansion of the controversial Indian Ocean Hotels with new convention Centre, suites, serviced apartments and rental area in an effort to bring conference tourism in Tanzania. His application was rejected by the BOT via the bank's letter dated Sept 1st, 2005. The bank said it was unable to process his request at the moment. The main reason why Ladwa's application was rejected was the fact that the Deed of Assignment was forged. It was discovered that some of the JPY did not exist and some had been applied by other companies. Also the Deed's signature by one Hiroyuki Sogabe was forged. This is the cause of Jitesh's war with the BOT management and his fellow Asian businessmen. Jitesh who is close to the Finance Minister, Zakia Meghji, has caused a lot of damage to Tanzania. He has tarnished the name of our country through almost all media houses such as Times and Africa Confidential and all local newspapers using some corrupt local and foreign senior reporters and editors who frequent his offices at Golden Tulip Hotels. The same Jitesh Ladwa started attacking our fellow Asians, including Jeethu Patel because Jeethu had turned down his request for money. Instead, he compromised with Tanzania's KING maker, Rostam Aziz who gave some of his cut to Jitesh and that's why although Rostam received the EPA funds he's not mentioned anywhere in Jitesh's emails. In fact, in Tanzania we have two governments, one under Jakaya Kikwete and the other under Rostam Aziz. Rostam Azizi's government seems to be more powerful than Kikwete's because his government (comprising of corrupt businessmen) has the money which is badly needed by CCM. What we see here is that Jitesh is trying to scandalize the government and the BOT because he is highly indebted by many financial institutions i.e.: IFC ($6 million), EuroAfrican Bank (Tsh 1 billion) and Barclays Bank ($2 million). All the hotels, Golden Tulip and Karibu Hotels are mortgaged. Surprisingly enough, Jitesh is using his friend Hosea to threaten the banks. Tanzanians must watch out; the secret agenda why Asians are fighting for political posts is to get information from the government and how they can influence such decisions. Ordinary Tanzanian may ask why in the EPA there was NO black Tanzanian. The next move is to make sure the year 2010, some Asian heavy weights entering the parliament i.e. Yusuph Manji. Their number and of course their financial muscle, would make them powerful in the House, and eventually have the first Asian Speaker of the National Assembly. What's needed is to make sure the government is deliberately empowering black Tanzanians otherwise poverty would continue haunting them and we will continue seeing the Sabodo's enjoying the money they swindled..The so called BOT scam was carefully created in order to fool the public, but in fact this was an Asian business conflict affair. Let the government form a probe committee to investigate the accumulated wealth of Mr. Hosea, it would be discovered that he is "the most corrupt Tanzanian." Some of us are not in Canada because we love this country, but ran away from Hosea's threats. One would ask, why all National Housing Corporation (NHC) joint projects go to Asians OR Why all concessions in the Serengeti go to Indians and Arabs? Did the Corruption boss, Hosea, took trouble to investigate? And now the big scam: The mother of all scams is in the making. This is the decision by the Tanzanian government to privatize half of the Serengeti National Park in what they call Concession for 99 years. The plan under the cover of the Tanzania National Parks Authority (TANAPA) includes all players in the major scandals in Tanzania. At the centre of the project, "The Serengeti National Park Privatization Project," is Mr. Paul Jones who has been commissioned to conduct a 'study'. We are informed that TANAPA is footing all travel, food and accommodation expenses for Mr. Jones. Under the project, we have learnt that the US millionaire Mr. Tudor James would construct a Presidential Lodge in the Serengeti. What a shame? Hosea knows all this; and that corruption is involved in the whole deal, but he has not taken or initiated any investigation against TANAPA's management and its Directors because the engineers of this project had promised him a big cut once the project is endorsed. In simple language, Tudor James owns TANAPAThrough lobbying by TANAPA's Board of Directors, while in New York recently, Kikwete met the Serengeti 'investor," Tudor James. With this friendship, (Tudor and Kikwete) it's now evident that Serengeti will be SOLD to an American tycoon!
 
Hii ilishatoka hapa JF kitambo.

Jamani, tujifunze angalau kufanye editing kidogo ili iwe rahisi kusoma. Sasa post kama hayo haina hata paragraph, utaisomaje?
 
TAKUKURU haiko usingizini- Hosea

2008-04-29 10:10:56
Na Onesmo Kapinga


Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuizua Rushwa Nchini, (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, amesema uchunguzi wa kesi kubwa 10 za rushwa utatangazwa mwaka huu.

Alisema kuwa kati ya kesi tano matokeo yake yanatarajiwa kutangazwa baada ya mwaka wa fedha wa serikali ambao unamalizika Juni 30, na zingine ifikapo Desemba, mwaka huu.

Hayo alisema jana wakati akifunga semina ya siku mbili iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la African International Group of Political Risk Analysis (PORIS) kuhusu maboresho ya Utawala Bora dhidi ya kupambana na rushwa iliyofanyika, Bagamoyo mkoani Pwani.

Dk. Hosea alisema uchunguzi wa kesi zimefikia katika hatua nzuri ya kukamilika na matokeo ya kwanza yanatarajia kutangazwa mwishoni mwa mwaka wa fedha.

Alisema PCCB itachunguza kesi zote ambazo zinawakabili baadhi ya viongozi wa ngazi ya juu serikalini ambao wanahusika na kuingia mikataba mibovu ya serikali ambayo inadaiwa rushwa ilitumika katika kupitisha mikataba hiyo.

Dk. Hosea alisema taasisi hiyo haijalala usingizi kuhusiana na tuhuma za rushwa ambazo zinawakabili viongozi ambazo zingine zimeibuliwa na wabunge.

Aidha alisema kuwa, wananchi wasifikiri hawafanyi lolote dhidi ya tuhuma za rushwa na kuongeza kwamba jamii inatakiwa kushirikiana na chombo hicho ili kuweza kutoa taarifa za rushwa.

Dk. Hosea alisema kuwa baada ya uchunguzi wao watapeleka uchunguzi wao mbele ya vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.

Hata hivyo, aliushukuru Ubalozi wa Ubelgiji kwa ufadhili wa fedha kutoka PORIS katika kuenzi utawala bora nchini Tanzania.

Mkurugenzi wa PORIS, Bw. Prince Bagenda, alisema kuwa semina hiyo inafuatia matokeo ya Brussels yaliyofanyika Machi 14-15 mwaka jana nchini Ubelgiji kuhusiana na maboresho ya Utawala bora na jinsi ya kupiga vita rushwa.

SOURCE: Nipashe
 
The problem with our top leaders is ....wanafanya timing!!! wanaagalia upepo while in need ya kutoa maamuzi au utatuzi mzito wa mambo. Na pengine kama hayo "mambo" yanawahusu watu wazito serekalini au kwenye vyama vyao!

No!

This is not the right time ya kumumuyanya mumunya maneno na kufikicha vidole..!

They sould take heart!

AND

Do what must be done for the good of the nation!
 
Hivi huyu mtu bado anajidanganya kuwa watu waamini uchunguzi wake, hata hao hatakao wachunguza watasema yeye sio clean kwahiyo hawezi kutuchunguza. Yeye binafsi ana kashifa kibao kama kuwa na nyumba ya gharama USA, kulamizimisha washitakiwa wa PCCB kutetewa na kampuni yake, kuusika kwenye Richmond bado anajipa imani kuwa watu watamwamini.

Kama anaweza mimi nafikiri angeanza kujichunguza yeye mwenyewe kabla hajachunguza wengine. Intergrity ya kumchunguza Mkapa au Yona hana, ila anabwabwaja ili watu watulie wakati mafisadi wakiendelea kutafuna nchi yetu.
 
unajuwa kuwa moja ya CV ya Wadanganyika ni ufisadi kama huna basi mambo magumu, bado wadanganyika wamo kwenye usingizi kuliko wa Hosea
 
Mie nauliza... Mbona Balali hajawajibishwa na tuhuma zinazomkabili? Huko kumfukuza kazi kulitosha kweli?

./Mwana wa Haki!
 
TAKUKURU haiko usingizini- Hosea

2008-04-29 10:10:56
Na Onesmo Kapinga


Mkurugenzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuizua Rushwa Nchini, (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, amesema uchunguzi wa kesi kubwa 10 za rushwa utatangazwa mwaka huu.

Alisema kuwa kati ya kesi tano matokeo yake yanatarajiwa kutangazwa baada ya mwaka wa fedha wa serikali ambao unamalizika Juni 30, na zingine ifikapo Desemba, mwaka huu.


SOURCE: Nipashe

Hivi ni vibweka kweli kwanini isiwe muda huu hadi wakimbie ndio utueleze huo utumbo wako wakamate sasa hivi warudishe jasho letu tunakamuliwa wao wanakula kwa raha wewe unasema tusubiri hadi Dec
 
Hii ni dhiaka...... Huyu jamaaa naona kaamua kuwa mwanasiasa, mwishoni mwa mwaka 2007, Huyu jamaa alitamba kwenye vyombo vya habari kwa kauli tata .... nawapa wala rushwa muda, washerehekee waka mpya baada ya hapo wawe tayari kukabilialiana na sheria....

ni huyu huyu leo anakuja na story

ya Mungu mengi labda this time atakuwa serious.......
 
Back
Top Bottom