mrisho shabani
Member
- Feb 11, 2008
- 14
- 0
Asante sana kwa uchangiaji wenu,unaoruhusu hoja pinzani nazo kujikita mahala,mie nauita ni "open minded thinking".
Kwenye ile taarifa ya kamati kuna mambo mengi sana na ndio maana waziri mkuu hata kaunda kamati nyingine kupitia yale mapendekezo na kuona ni jinsi gani yanatekelezeka bila kuathiri haki za watu au kuwaonea wengine. Kikubwa kilichobainika na kamati ya mwakyembe ni ukiukwaji wa wazi wa taratibu za tendering uliofanywa na wizara,maafisa wake na kitu kinachoonekana kama shinikizo la waziri mkuu. Ukiukwaji wa taratibu huo kwa wenyewe sio rushwa tena kisheria unafall katika administrative law,bali umebeba pia mambo mengine kibao yanayoibua masuala mengine ya kisheria. Point kubwa hapa ni ukiukwaji wa sheria ya tendering na kutofanya due diligence ambayo inategemewa kwa reasonable man wa calibre ya AG,na maafisa wa wizara.
Ukiukwaji kama huu kwa kawaida adhabu zake zipo administratively sio judiciary.Adhabu zao ni kama kushushwa vyeo,kuhamishwa vitengo kwani vile walivyopo sio competent n.k.Sasa HOSE yeye anakuja wapi? Kila mtu katika ile ripoti anasehemu yake aliyochangia kama ni nengligence tunasema contributory negligence.
Kama walivyo wengine HOSEA sehemu inayomgusa ni hii:
Ukisoma kifungu cha 6 cha sheria hiyo ya zamani kinasema kwamba
mtu yeyote ambaye kwa kujua atampa wakala, au wakala yeyote kwa kujua atatumia kwa lengo la kumdanganya mkuu wake, risiti,akaunti au hati au nyaraka yoyote inayohusiana na mambo au shughuli yoyote ya mkuu wake wa kazi na ambayo ina taarifa feki,za kughushi au zilizopotoshwa na kwa jinsi yoyote ile zina lengo la kumdanganya mkuu,atakuwa ametenda kosa.mwisho wa kunukuu.
Sawa Hosea hakuona rushwa,je hakuona pia kipengele hiki cha sheria? je katika mkatba wa richmond hakukuwa na nyaraka feki zenye lengo la kumpotosha mkuu,je kusema kwamba richmond ina ubia na kampuni ile waliyoitaja na kuthbitisha hilo kwa business kadi hakukuwa na lengo la kumpotosha mkuu?je,ukweli kwamba richmond haikuwa mtu kisheria yaani sio kapuni halali kwa kuwa inakosa usajili tanzania na huko USA haipo na kwamba hata kama ilisajiliwa hapa nchini usajili wake haukuwa halali kwa kuwa hatuna one man company kwa mujibu wa kifungu cha tatu,moja cha sheria ya makampuni.je,waliohusika hawakuwa na lengo la kumpotosha mkuu?
Hapa tu,akiclear hapa anapeta,mi ningekuwa wakili wake ningejikita kutafuta defense mahali hapa zaidi,kwani sehemu nyingine zote za sheria namba 16 yupo clean.Hatuna sheria ya harufu wala moshi wa rushwa.Neno harufu au moshi wa rushwa linatokana na sheria ya ushahidi ya ya mwaka 1967 nadhani THE LAW OF EVIDENCE ACT,kifungu cha 3 hadi 15 kinachozungumzia circumstancial evidence, Circumstancial evidence ndio inayounda mazingira au harufu ya tukio la rushwa. Ndio maana nikasema hata katika kesi ya balozi mahalu inayoendelea hakukuwa na rushwa ya moja kwa moja kesi imeenda mahakamani on circumstantial evidence.Na kesi za namna hii huwa ngumu sana kuliko zile za kumshika mtu papo kwa hapo.
Hayo yote ya kamati kuwataja watuhumiwa au la sioni kama ni msingi sana kwa mhe.Hosea ambaye namheshimu sana kama mwalimu wangu somewhere.Ila ni wazi wenzie hata kama wana hila mbaya naye wanataka kumkamatia hapa.Ningeomba mtu mwenye ripoti ya HOSEA atumwagie hapa ile tuweze kujadili vizuri zaidi kwa kuilinganisha na findings za mwakyembe.
Hiyo sheria tunaijua kaka, tatizo ni kwamba soma HOJA ZA SANDE kwanza utupe majibu.
Ushahidi wa kamati ya MWAKYEMBE na majina ya wanaotuhumiwa kwa rushwa ili waende mahakamani.
Hatuhitaji maoni ya watu bali zingatia hayo kwanza.