Acheni kuzunguka zunguka. Mnataka kusema huyo dereva alikuwa amepewa task ya kuondoa roho ya zitto?? Mnaanza kuhukumu hata uchunguzi haujafanyika. Mmoja hapo juu anasema eti hilo fusso lilifuata moja kwa moja gari la marehemu. Naomba kumuuliza, ajali huwa zinatokea vipi?? is it not the case kwamba magari inabidi yakutane uso kwa uso ili ajali iweze kutokea??? Sasa ajali ingetokeaje kama kila dereva angeendelea kubaki kwenye lane yake???
Hivi hapa nchini mwetu, ni muda upi hupita mpaka topsecrete na confidential files (simaanishi mikataba) nyingine zina kuwa legally released to public?!
SteveD.
Mungu ni mkuu na mwema sana!!! naamini ataendelea kumlinda mh. Zitto na kila aina ya hila na ubaya unaolengwa kwake!!
It looks as if he was the target!!
Sijui ni kwanini watu wanapenda sana kukuza na kuandika mambo ambayo hayapo.
PHP:Labda wangetaka tuamini kuwa Zito ndio alikuwa target basi wangetuambia how they think the whole plan was executed and what went wrong. From my simple understanding and from what the madia has reported hii inaonekana ni ajali ya kawaida tu ambayo ingeweza kumpata mtu yoyote. Kama Zito alikuwa target basi dereva wa lori lazima alijua Zito anatumia gari gani. Unless gari lake na la Marehemu yalikuwa sawa then jiulize kwanini alikosea na kuligonga gari la Marehemu? Pili mwandishi anataka tuamini kuwa Marehemu, Zito, Sumaye na Mathayo walikuwa wanaongozana barabarani kiasi kwamba kama dereva wa lori angeikosa gari ya Marehemu basi angeligonga gari la Zito. Zito mwenyewe kasema kuwa alifika sehemu ya tukio baada ya dakika tano hivi. Kwa wale wenye uzoefu wa kusafiri safari ndefu, dakika tano kwa gari linaloenda Km 80 kwa saa ni sawasawa na umbali wa Km 6 hivi. Sasa kwa umbali huo utaona kuwa hata kama angeikosa gari ya Marehemu basi angeweza kuanguka mwenyewe tu unless mwandishi anataka tuamini kuwa hiyo error kama isingetokea kwa Marehemu basi ingetokea kwa Zito. Pia mwandishi anakuwa na mashaka juu ya maelezo ya polisi kuwa dereve wa lori alitoroka au "kutoroshwa" baada ya ajali. Kwa kumbukumbu zangu mara nyingi madereva wasababishapo ajali hukimbia kuhofia maisha yao na wengine wakiogopa kushitakiwa. Mimi naona hii ilikuwa ni ajali ya kawaida tu kama ajali nyingine.
Hii ni assassination attempt that went wrong, I said it, yes I said it!
Sitaki kuamini nini kinasemwa hapa!!Lakini nilipata kufanya kazi na mtu makini sana.Nae alinipa maneno ambayo ni key kwenye mambo yangu mengi,Mzee yule aliwahi kuniambia "Be suspicious with Everything" Baada ya Uchunguzi uliochukua karibu miezi 12, Report ilimbana Mkuu wa kitengo kwa uizi,ambaye ndie alikuwa muelekezaji wa kila kitu ili kurahisisha Uchunguzi!,Kwa mazingira ya kawaida mtu huyo usingeweza kumfikiria kuwa ndiye mwizi Mwenyewe!!!
Sasa Waungwana tuwe waangalifu na tupime kila kitu kwa uzito wake."Sio kila aendae kanisani ni mcha Mungu".Tusiyakanushe yasemwayo sasa na wala tusiyakubali moja kwa moja ,lakini lazima tuweke (?) na kusubiri Uchunguzi.
Ha ha eti Assassination Attempt, duh!! jamaa alimiss darasa la planning.Inabidi apelekwe kwenye training ya Blackwater USA awe polished.
Ila this is funny it has made my day.
Lisemwalo lipo na kama halipo linakuja. Maneno mazito hayo mkuu kama unakumbuka vizuri wakati tetesi za jaribio la kumuua Moringe Sokoine alipokuwa anatoka kusali kanisani na baadaye kwenda kutibiwa nje na aliporudi Mwalimu alikuwa safarini Mozambique, nafahamu kuna watu wana picha zile zilizotoka Daily News wakati ule na alihamisha kambi ya kusali ikawa ST. Joseph, pia mauza uza yaliyojitokeza baada ya kifo chake baada ya yule rubani kwenda na hamsini zake. Tusubiri tutaona mengi.
Je, huyo dereva alitokomelea wapi? Hivi sasa yuko wapi?
Insurgent,
U'r signature says it all! even on this case.
Have an open mind kwani kama unaamini:-
The fact that a believer is happier than a skeptic is no more than the fact that a drunken man is happier than a sober one.
Then anything is possible!