Aliyekuwa katibu wa CHADEMA Mara ajiunga CCM

nilisema , huwezi kuwa member wa ccm ukawa timamu ! Haiwezekani,kielelezo cha fikra lojo.Kwani kazi za serikali wanauliza kadi za chama ! Ni juha anaeweza kufikiri sawa na wewe.Kazi zenye kuhitaji kadi ni zile za chama chenu .Kazi za umma , hazina vyama. Punguza ujuha kidngo uwe timamu.
Asante m-coconut, msukuma mikokoteni
Mie kilaza -ni kweli
Mie juha-hswaa
Siwezi kufikiri wallahi umepata
Ujuha sipunguzi maana maandamano siyawezi.Na virungu si saizi yangu
Na siku nikikuona kwenye maandamano mie nitashusha kioo cha dirisha ili nikupe pole.
Juha mie nikatengeneze pesa.
Lakini tuache mambo haya ya kijuha tuongee ya kichadema
Nikuulize swali dogo
NANI MWINGINE ATAONDOKA?
ILI MUMWITE MBWABWAJAJI?
 
Mnafika tu huyo aende, wenzie wanatafuta mlango wa kutokea yeye anarudi huko huko.kwaheri msalimie shitambala. teh teh tah
 
MBUNGE mteule wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono ameingia katika kashfa ya rushwa ya uchaguzi na huenda akapoteza ubunge, MwanaHALISI limeezwa.
Mkono ametajwa kutoa mlungula kwa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika jimbo hilo, Michael Makanja ili ampe nafasi ya kupita bila kupingwa.

Taarifa zinasema Makanja amewaeleza viongozi wa Kurugenzi ya Ulinzi na Usalama ya CHADEMA, kwamba alishawishiwa na Mkono kupokea kiasi cha Euro 1,000 ( karibu Sh. 2 milioni) ili kujitoa katika kinyang’anyiro cha ubunge.
Fedha hizo ni sehemu ya mamilioni ya shilingi ambayo Mkono inasemekana aliahidi kumlipa mgombea huyo wa Chadema.
“Baada ya Makanja kufika hapa, wanachama walimvamia wakitaka kujua nini kimemsibu. Hapo ndipo mchezo ulipobumburuka,” alisema afisa mwandamizi wa ulinzi na usalama wa Chadema, Hemed Sabula.
Alisema Makanja aliwasili katika ofisi za makao makuu ya chama hicho kwa lengo la kukutana na viongozi wakuu wa chama, lakini kabla hajaingia ndani alikutana na kundi la wanachama waliombana aeleze ukweli wa kilichotokea hata akajitoa.
Makanja alijitoa kugombea ubunge katika jimbo hilo, siku mbili baada ya kuteuliwa kuwa mgombea kwa kumuandikia barua msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.
Aidha, Makanja aliwataja viongozi wawili – katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Sibitari Nyanza na mwenyekiti wa vijana wa mkoa, David Katikiro – kwamba ni wabia katika mpango huo.
Kwa mfano, ujumbe wa simu ya mkononi uliotumwa kwa kigogo huyo kutoka kwa simu ya Makanja (namba tunaihifadhi) unasema, “Mzee ameshanikatia tiketi ya kwenda Dar. Sasa mhimize amalize kiasi kilichobaki, maana hali yangu kiuchumi si nzuri….”
Mwingine ulisema, “Tumeshamaliza kama tulivyokubaliana.” Ujumbe huo ulitumwa tarehe 21 saa 8:21 mchana.
Ujumbe mwingine uliotumwa juzi Jumatatu, mara baada ya Makanja kuingia “mtegoni” ulisema, “Niko makao makuu ya chama. Nimewekwa chini ya ulinzi....”
Akijibu katika namna ya kushtuka, kigogo huyo alijibu, “Wewe nani kakwambia uende huko… Watakuua. Siwezi kuja huko kukutetea....”
Taarifa zilizofikia MwanaHALISI zinathibitisha kuwa tayari Chadema kinaandaa malalamiko rasmi kwa Msajili wa vyama vya siasa dhidi ya hatua hiyo ya Mkono.
Mkuu huo ndiyo ukweli nami nillitaka kuweka bayana hilo, na kwa taarifa tu hiyo nafasi ya katibu aliyosimamishwa bawaba Nyanza bado haijajazwa baada ya kutemwa kwa usaliti wake. Kisha anasema ana mapya ama kweli CCM hapo wamelamba galasa na ndiyo mwisho wake kisiasa.
 
Chadema tunasikia mnazo evidences kwenye video (in his own words) tuleteeni public au download JF tunauhakika ccm na usalama wa taifa wala hawana mipango ya ku-prosecute ccm bali Mbowe na Dr Slaa.

Thats ccm na mafisadi angalieni wanavyopenda pesa huko bungeni, it's not matter of who did or didn't but wangapi ccm walifanya hii mipango ya kuwanunua wapinzania kwa manufaa ya kupata hizi posho. Tunafiiri wanakwenda dodoma kwa ajili ya wananchi kumbe ni familia zao na vimada wao.
 
Breaking News: PIGO CHADEMA MARA

Katibu wa CHADEMA wa Mara Nyanza Sibitari amerejesha kadi rasmi jioni hii katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na aliyekuwa mbunge wa Musoma Mjini Vedasto Manyinyi.

Sibitari aliyeongozana na vijana wengine 126 na bendera na Kadi za CHADEMA anadai kuwa kajiengua CHADEMA kwa sababu zifuatazo:

  • CHADEMA Kuendeshwa kama Taasisi na si chama
  • Kushamiri kwa makundi ndani ya Chama hicho
  • Mgogoro ulioanza toka nyakati za uteuzi wa viti maalumu hadi Ubunge

Anadai alipotea na sasa karudi nyumbani

More UP DATE to follow
Umeyaona majibu yako, acha ushabiki utaheshimika kuliko kuwa kama FaizaFoxy.
 
Old News... Huyo Mbunge wa Chadema aliyejitoa alikanusha kwanza kwahiyo hakuna Ushahidi-- CASE CLOSED TUSUBIRI 2015
 
Breaking News: PIGO CHADEMA MARA

Katibu wa CHADEMA wa Mara Nyanza Sibitari amerejesha kadi rasmi jioni hii katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na aliyekuwa mbunge wa Musoma Mjini Vedasto Manyinyi.

Sibitari aliyeongozana na vijana wengine 126 na bendera na Kadi za CHADEMA anadai kuwa kajiengua CHADEMA kwa sababu zifuatazo:

  • CHADEMA Kuendeshwa kama Taasisi na si chama
  • Kushamiri kwa makundi ndani ya Chama hicho
  • Mgogoro ulioanza toka nyakati za uteuzi wa viti maalumu hadi Ubunge

Anadai alipotea na sasa karudi nyumbani

More UP DATE to follow


Huyu ameamua kurudi rivasi badala ya kwenda mbele lakini kwa sababu rivasi nayo ni mwendo ila wa kurudi nyuma basi tumwache . Asitupotezee muda wa kumjadili huyu zumbukuku kwa sababu walioko upande wetu ni wengi yaani wao ni minority na sisi majority. Tusimwone adui bali opportunist ambaye hata kama angebaki CDM angekuwa tatizo na hivyo tumchukulie kama jipu lililopasuka na cha kufanya hapa ni kuweka dawa na kufunga plasta na safari iendelee.

Hii ya kumwaga sumu akiwa nje ya CDM itakuwa ngumu kwani tutegemee kupigwa mawe kama Mh. Nyambiri halafu isitoshe huyu Bwana ni ndumilakuwili hata huko CCM watamshangaa. Kipindi cha CCM kugawa vyeo kwa waliohama upinzani kimepita kule ataenda kulamba tu viatu vya wakubwa
 
Walikuwa kwetu lakini hawakukaa kwetu kwasababu walikuwa si wetu. Amefanya jambo jema kuondoka maana hatufai wananmapinduzi!
 
Wanafki na wajinga hatuwahitaji cdm,huyu ni sawa na mbwa aliyetapika na kurudia matapishi yake.Aondoke zake.
 
Naomba usipotoshe umma,hii si breaking news kwani mtu huyu alisha fukuzwa kwenye chama siku nyingi.yawezekana kwa kuwa alikuwa katibu atakuwa alikuwa na masalia ya kadi.

Oh damn inaelekea huna taarifa na chama hiki utakuwa umedandia treni kwa mbele, hapa kila mwanachama haelewi ni hasa kimetokea kwa huyu jamaa ghafla bila maelezo na likuwa akifanya kazi za Chama mpaka jana. Usikurupuke soma hoja tuje tunafanyaje hapa.

Kumbuka asilimia 90 ya wapiga kura wetu Musoma ni kutoka Mwalo wa Mwigobero na Soko kuu ambao ni wajasiamali wadogo kimtazamo wanaweza kuyumbishwa sana na uamuzi huu.
 
Back
Top Bottom