Nifah
JF-Expert Member
- Feb 12, 2014
- 32,122
- 68,046
Mtasumbili sana sidhani kama mmepata mlichotegea endeleeni tu mvumilivu hula mbivu
Ama kweli leo watu mmechanganyikiwa jamani!Video ina masaa tu mnashindwa hata kuandika vizuri???
Mtasumbili sana sidhani kama mmepata mlichotegea endeleeni tu mvumilivu hula mbivu
Hata ungekuwa wewe lazima ungetetemeka!Hii habari ya Kiba sio mchezo ujue!,Ama kweli leo watu mmechanganyikiwa jamani!Video ina masaa tu mnashindwa hata kuandika vizuri???
siongei ushabiki siongei chuki whatever but video kimuonekano (rangi na mavazi) ni nzuri kiasi chake but location haina uhusiano na alicho imba by the way kwa mtu ambae hajui kiswahili hatoweza kuconnect dots nini kina imbwa.
ushauri kwa management ya kiba muwe active kummanage kijana wenu,msimuache anakaa kimya kwa mda bila kutoa ngoma mkiendelea hivyo kila siku mtakua mnasema "return of the king" mna waumiza mashabiki wa kiba kwa kusubiri kila siku.
ushauri kwa mashabiki wa kiba tumieni mitandao ya kijamii kumshauri kiba na management yake ili "kudumisha maisha ya kiba kimuziki" ili kuleta ushindani maana diamond anavyo jiona yuko peke yake anaweza kubweteka ila kukiwa na watu wanao muwashia taa nyuma yke atashtuka pia.
hongera kiba kwa uthubutu wa kutoa video nje ya mipaka ya east africa.
Hata ungekuwa wewe lazima ungetetemeka!Hii habari ya Kiba sio mchezo ujue!,
Jamani,hao huwajui wewe!!ivi hawajui kuwa kuna mitindo mingi ya video!!sio lazima video iwe ya kufatisha kilichoimbwa tuu!!Hao wakiona video ya jay z kaimba mwanzo mwisho kaegemea ukuta watakuja waponde,ushamba mzigo!!hawana exposure jamani hawaelewii!Huu sio ushauri kabisa ni kejeli...
Bora ungejikalia zako kimya kuliko huu utumbo uliouandika hapa.
Ni exposure ndogo na ufahamu mdogo unaowasumbua haters,jamani so walitaka afanye maigizo kwenye ile video!!Mdakuzi upo wapi!!Wanaosema video haiendan na alichoimba kiba watofautishe music video na movie au filamu.... ukitaka story angalia muvi au series.... kiba amejitahd sana....
Nimetumia muda wa kutosha kufuatilia mjadala hapa kuhusu video mpya ya Mwana, nashukuru wapo watu wanaoelewa muziki wamekuwa wakitoa maelezo mazuri kuhusu uzuri na kufanikiwa kwa lengo la video yenyewe. Kiukweli ni video bora sana yenye matukio yasiyochosha, kiasi kwamba unaweza kuhisi wimbo ni mfupi (lol).
Kuna kitu ambacho watu wengi hawaelewi, kwamba kutengeneza video si kipaji (pekee) ila ni taaluma yenye misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, mwanamuziki hatengenezi video bali hutengenezewa video, aidha kulingana na aina ya wimbo wake ama ujumbe wa wimbo wake na mambo mengine kama hayo.
Kama ilivyo kwa aina za muziki kama vile Reggae, R&B, Zouk, Soul, Afro Pop na nyinginezo, ieleweke kuwa video nazo zina aina kadhaa, na zina misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, kama ambavyo huwezi kusema umepiga Reggae wakati muziki wako uko kwenye misingi Zouk au Charanga ama Salsa.
Kulingana na mjadala unaoendelea nimegundua kwamba, wengi hawajui kama kuna aina kadhaa za video za muziki, lakini kuna kuu tatu za video za muziki (ambazo zimekuwa zikitumiwa zaidi ulimwenguni kote), ambazo ni Performance Video, Narrative Video na Conceptual Video. Nitazielezea tofauti zake.
Performance video, aina hii hurekodiwa kwa kuonesha bendi au msanii anavyoimba tu wimbo husika. Ni aina ya video inayohitaji kiasi kikubwa cha shots zitakazokuwa zikiingia na kutoka mfululizo na kwa haraka ili kuifanya video kuvutia, kwani ikiwa na shots chache kuna hatari video inaweza kuboa, kwani hurekodiwa katika eneo moja.
Mfano wa video za mtindo huu ni ya wimbo No Woman No Cry (live) wa Bob Marley (RIP), kwa kiasi kikubwa video hii imefanikiwa sana, kwa sababu ina vipande vingi vya video na shots za kutosha, camera angles ndio usiseme, lakini pia ni kitu kimoja cha kuvutia ambayo ni uingizaji vipande vya video wa ghafla ili kudumisha umakini wa mtazamaji.
Conceptual Video, aina hii ya video huegemea zaidi utunzi au wazo la wimbo husika. Huwa vipande vingi vya matukio ya kuigizwa ili kujenga uhusika la wazo la wimbo husika, na mara nyingine huwa ni vipande vya filamu (sound track), nyingi kati ya video hizi hukamilishwa kwa kufanyiwa Special FX ili kuleta uhalisia wa matukio ya wazo la wimbo husika. Ni miongoni mwa video ghali zaidi.
Mfano wa video za mtindo huu Thriller ya Michael Jackson (RIP), Otis wa Jay Z & Kanye West na nyingine zinazofanana nazo. Na ziko baadhi ya video za mtindo huu zinaweza kuwa na vipande vya video vya matukio matupu bila ya kuonekana hata mara moja kwa muimbaji husika.
Narrative Video, hii ni aina ya video ambayo inakuwa na msimuliaji (au wasimuliaji) ambaye ndiye muimbaji wa kisa cha muziki wake. Yenyewe itakuwa na vipande vingi vya video vinavyomuonesha msimuliaji (wasimualiaji) akiwa kwenye movements zake, katika maeneo mbalimbali ama eneo moja ila katika camera angles tofauti.
Aina hii ya video hutoa nafasi kwa wahusika wa video kuonesha uwezo wa kucheza, na hata kutambulisha style zao za kucheza, ni aina za video ambazo hutumiwa na wanamuziki wengi wenye uwezo wa kucheza, mfano wake ni wimbo mpya wa Chris Brown wa New Flame, na hata wimbo wa Nassib wa Number 1 (Remix).
Kwa hiyo sio kila video lazima iwe Performance Video, Narrative Video au Conceptual Video, inaweza kutengenezwa kwa kufuata mojawapo na ikawa video bora kabisa. Hivyo, kama umeitazama video ya Mwana utaona kama imekaa katika Narrative Video na Performance Video kidogo, na hii kutokana na aina ya muziki husika, kwani Mwana unaweza kuiita ni Half Dance.
Ni video nzuri iliyofanikiwa katika malengo yake, kwanza ilimfaa Kiba kwa kumpa nafasi ya kuonekana zaidi, hasa kwa kuwa alikuwa kimya kwa kipindi cha miaka mitatu. Pia, ubora wa picha ni wa kuvutia sana, hata uchaguzi wa mazingira ulikuwa wenye umakini.
Isitoshe hata utumiaji wa Extras ulikuwa mzuri sana, rejea Kiba alipokuwa ukumbini na alipokuwa akitembea mtaani. Haikuwa na vipande vya kukaa kwenye TV yako kwa muda mrefu, matukio yalikuwa yakihama vizuri, na kwa kiasi kikubwa ilitulia kwenye mingi ya aina za video zilizotumiwa.
Ova
Nimetumia muda wa kutosha kufuatilia mjadala hapa kuhusu video mpya ya Mwana, nashukuru wapo watu wanaoelewa muziki wamekuwa wakitoa maelezo mazuri kuhusu uzuri na kufanikiwa kwa lengo la video yenyewe. Kiukweli ni video bora sana yenye matukio yasiyochosha, kiasi kwamba unaweza kuhisi wimbo ni mfupi (lol).
Kuna kitu ambacho watu wengi hawaelewi, kwamba kutengeneza video si kipaji (pekee) ila ni taaluma yenye misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, mwanamuziki hatengenezi video bali hutengenezewa video, aidha kulingana na aina ya wimbo wake ama ujumbe wa wimbo wake na mambo mengine kama hayo.
Kama ilivyo kwa aina za muziki kama vile Reggae, R&B, Zouk, Soul, Afro Pop na nyinginezo, ieleweke kuwa video nazo zina aina kadhaa, na zina misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, kama ambavyo huwezi kusema umepiga Reggae wakati muziki wako uko kwenye misingi Zouk au Charanga ama Salsa.
Kulingana na mjadala unaoendelea nimegundua kwamba, wengi hawajui kama kuna aina kadhaa za video za muziki, lakini kuna kuu tatu za video za muziki (ambazo zimekuwa zikitumiwa zaidi ulimwenguni kote), ambazo ni Performance Video, Narrative Video na Conceptual Video. Nitazielezea tofauti zake.
Performance video, aina hii hurekodiwa kwa kuonesha bendi au msanii anavyoimba tu wimbo husika. Ni aina ya video inayohitaji kiasi kikubwa cha shots zitakazokuwa zikiingia na kutoka mfululizo na kwa haraka ili kuifanya video kuvutia, kwani ikiwa na shots chache kuna hatari video inaweza kuboa, kwani hurekodiwa katika eneo moja.
Mfano wa video za mtindo huu ni ya wimbo No Woman No Cry (live) wa Bob Marley (RIP), kwa kiasi kikubwa video hii imefanikiwa sana, kwa sababu ina vipande vingi vya video na shots za kutosha, camera angles ndio usiseme, lakini pia ni kitu kimoja cha kuvutia ambayo ni uingizaji vipande vya video wa ghafla ili kudumisha umakini wa mtazamaji.
Conceptual Video, aina hii ya video huegemea zaidi utunzi au wazo la wimbo husika. Huwa vipande vingi vya matukio ya kuigizwa ili kujenga uhusika la wazo la wimbo husika, na mara nyingine huwa ni vipande vya filamu (sound track), nyingi kati ya video hizi hukamilishwa kwa kufanyiwa Special FX ili kuleta uhalisia wa matukio ya wazo la wimbo husika. Ni miongoni mwa video ghali zaidi.
Mfano wa video za mtindo huu Thriller ya Michael Jackson (RIP), Otis wa Jay Z & Kanye West na nyingine zinazofanana nazo. Na ziko baadhi ya video za mtindo huu zinaweza kuwa na vipande vya video vya matukio matupu bila ya kuonekana hata mara moja kwa muimbaji husika.
Narrative Video, hii ni aina ya video ambayo inakuwa na msimuliaji (au wasimuliaji) ambaye ndiye muimbaji wa kisa cha muziki wake. Yenyewe itakuwa na vipande vingi vya video vinavyomuonesha msimuliaji (wasimualiaji) akiwa kwenye movements zake, katika maeneo mbalimbali ama eneo moja ila katika camera angles tofauti.
Aina hii ya video hutoa nafasi kwa wahusika wa video kuonesha uwezo wa kucheza, na hata kutambulisha style zao za kucheza, ni aina za video ambazo hutumiwa na wanamuziki wengi wenye uwezo wa kucheza, mfano wake ni wimbo mpya wa Chris Brown wa New Flame, na hata wimbo wa Nassib wa Number 1 (Remix).
Kwa hiyo sio kila video lazima iwe Performance Video, Narrative Video au Conceptual Video, inaweza kutengenezwa kwa kufuata mojawapo na ikawa video bora kabisa. Hivyo, kama umeitazama video ya Mwana utaona kama imekaa katika Narrative Video na Performance Video kidogo, na hii kutokana na aina ya muziki husika, kwani Mwana unaweza kuiita ni Half Dance.
Ni video nzuri iliyofanikiwa katika malengo yake, kwanza ilimfaa Kiba kwa kumpa nafasi ya kuonekana zaidi, hasa kwa kuwa alikuwa kimya kwa kipindi cha miaka mitatu. Pia, ubora wa picha ni wa kuvutia sana, hata uchaguzi wa mazingira ulikuwa wenye umakini.
Isitoshe hata utumiaji wa Extras ulikuwa mzuri sana, rejea Kiba alipokuwa ukumbini na alipokuwa akitembea mtaani. Haikuwa na vipande vya kukaa kwenye TV yako kwa muda mrefu, matukio yalikuwa yakihama vizuri, na kwa kiasi kikubwa ilitulia kwenye mingi ya aina za video zilizotumiwa.
Ova
salute kwako Mimi nimejitahid kukuelewa but quality ya video nimeipenda san
Wewe mtu una miakili hadi sipendi ujue?....lol
Keep it up
Nimetumia muda wa kutosha kufuatilia mjadala hapa kuhusu video mpya ya Mwana, nashukuru wapo watu wanaoelewa muziki wamekuwa wakitoa maelezo mazuri kuhusu uzuri na kufanikiwa kwa lengo la video yenyewe. Kiukweli ni video bora sana yenye matukio yasiyochosha, kiasi kwamba unaweza kuhisi wimbo ni mfupi (lol).
Kuna kitu ambacho watu wengi hawaelewi, kwamba kutengeneza video si kipaji (pekee) ila ni taaluma yenye misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, mwanamuziki hatengenezi video bali hutengenezewa video, aidha kulingana na aina ya wimbo wake ama ujumbe wa wimbo wake na mambo mengine kama hayo.
Kama ilivyo kwa aina za muziki kama vile Reggae, R&B, Zouk, Soul, Afro Pop na nyinginezo, ieleweke kuwa video nazo zina aina kadhaa, na zina misingi yake ambayo ni lazima ifuatwe, kama ambavyo huwezi kusema umepiga Reggae wakati muziki wako uko kwenye misingi Zouk au Charanga ama Salsa.
Kulingana na mjadala unaoendelea nimegundua kwamba, wengi hawajui kama kuna aina kadhaa za video za muziki, lakini kuna kuu tatu za video za muziki (ambazo zimekuwa zikitumiwa zaidi ulimwenguni kote), ambazo ni Performance Video, Narrative Video na Conceptual Video. Nitazielezea tofauti zake.
Performance video, aina hii hurekodiwa kwa kuonesha bendi au msanii anavyoimba tu wimbo husika. Ni aina ya video inayohitaji kiasi kikubwa cha shots zitakazokuwa zikiingia na kutoka mfululizo na kwa haraka ili kuifanya video kuvutia, kwani ikiwa na shots chache kuna hatari video inaweza kuboa, kwani hurekodiwa katika eneo moja.
Mfano wa video za mtindo huu ni ya wimbo No Woman No Cry (live) wa Bob Marley (RIP), kwa kiasi kikubwa video hii imefanikiwa sana, kwa sababu ina vipande vingi vya video na shots za kutosha, camera angles ndio usiseme, lakini pia ni kitu kimoja cha kuvutia ambayo ni uingizaji vipande vya video wa ghafla ili kudumisha umakini wa mtazamaji.
Conceptual Video, aina hii ya video huegemea zaidi utunzi au wazo la wimbo husika. Huwa vipande vingi vya matukio ya kuigizwa ili kujenga uhusika la wazo la wimbo husika, na mara nyingine huwa ni vipande vya filamu (sound track), nyingi kati ya video hizi hukamilishwa kwa kufanyiwa Special FX ili kuleta uhalisia wa matukio ya wazo la wimbo husika. Ni miongoni mwa video ghali zaidi.
Mfano wa video za mtindo huu Thriller ya Michael Jackson (RIP), Otis wa Jay Z & Kanye West na nyingine zinazofanana nazo. Na ziko baadhi ya video za mtindo huu zinaweza kuwa na vipande vya video vya matukio matupu bila ya kuonekana hata mara moja kwa muimbaji husika.
Narrative Video, hii ni aina ya video ambayo inakuwa na msimuliaji (au wasimuliaji) ambaye ndiye muimbaji wa kisa cha muziki wake. Yenyewe itakuwa na vipande vingi vya video vinavyomuonesha msimuliaji (wasimualiaji) akiwa kwenye movements zake, katika maeneo mbalimbali ama eneo moja ila katika camera angles tofauti.
Aina hii ya video hutoa nafasi kwa wahusika wa video kuonesha uwezo wa kucheza, na hata kutambulisha style zao za kucheza, ni aina za video ambazo hutumiwa na wanamuziki wengi wenye uwezo wa kucheza, mfano wake ni wimbo mpya wa Chris Brown wa New Flame, na hata wimbo wa Nassib wa Number 1 (Remix).
Kwa hiyo sio kila video lazima iwe Performance Video, Narrative Video au Conceptual Video, inaweza kutengenezwa kwa kufuata mojawapo na ikawa video bora kabisa. Hivyo, kama umeitazama video ya Mwana utaona kama imekaa katika Narrative Video na Performance Video kidogo, na hii kutokana na aina ya muziki husika, kwani Mwana unaweza kuiita ni Half Dance.
Ni video nzuri iliyofanikiwa katika malengo yake, kwanza ilimfaa Kiba kwa kumpa nafasi ya kuonekana zaidi, hasa kwa kuwa alikuwa kimya kwa kipindi cha miaka mitatu. Pia, ubora wa picha ni wa kuvutia sana, hata uchaguzi wa mazingira ulikuwa wenye umakini.
Isitoshe hata utumiaji wa Extras ulikuwa mzuri sana, rejea Kiba alipokuwa ukumbini na alipokuwa akitembea mtaani. Haikuwa na vipande vya kukaa kwenye TV yako kwa muda mrefu, matukio yalikuwa yakihama vizuri, na kwa kiasi kikubwa ilitulia kwenye mingi ya aina za video zilizotumiwa.
Ova