Albert Msando ‘amwaga’ vifaa vya Corona kwa wanahabari Arusha, adai hali ni mbaya sana

Arusha tunajifia tu na ugonjwa wa kukosa kupumua. Oh! Lord have Mercy

Kuna kisa kile cha Njiro, pia kuna kingine nimesikia jioni hii kuna maiti juzi kati imechukuliwa usiku Sakina walioona wameona
Poleni sana watu wa Arusha, hili janga kila mmoja ajizatiti kivyake bila kuogopa tukajifanya ngangari hakika watu watakufa sana. Serikali haiwezi kushindwa kuzika itazika hata tukifa milioni 7, kikubwa ni sisi kujilinda wenyewe.
 
Kada huyu amewaasa waandishi wa habari kuandika ukweli kuhusu Hali halisi ya ugonjwa wa CORONA nchini ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa huu. Amesema Kama waandishi wa habari watakaa kimya Basi watakuwa wanalikosea taifa kwani taifa linawategemea katika kufikisha habari Hizi.

Je habari hii ya Msando inatosha kukubari kuwa Arusha Hali Ni mbaya ingawa Hadi Sasa kila kitu kinaonekana Ni shwari kwa upande wa Tanzania bara?
 
Hawa ccm siyo wa kuwaamini kabisa waandishi wanaweza kuwa wanatengenezewa zengwe au yupo mmoja wao anawindwa apewe kesi ya uhujumu,asitoe taarifa waziri mwenye dhamana anaelipwa mshahara na ulinzi anapewa wakatoe taarifa waandishi?

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
jembejembe,
Anaweza kututajia idadi ya wagonjwa arusha?
Na umri wa wagonjwa husika

Na hali zao za afya kabla ya mwaka huu au toka corona imeingia.

Au ndio umbea wa kike unofanywa na mwanaume
 
Arusha tunajifia tu na ugonjwa wa kukosa kupumua. Oh! Lord have Mercy

Kuna kisa kile cha Njiro, pia kuna kingine nimesikia jioni hii kuna maiti juzi kati imechukuliwa usiku Sakina walioona wameona
Kwa kweli Arusha vifo vipo. Naskia Rama wa Raha advertising nae ni mgonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanasheria Alberto Msando, asema hali ni mbaya, kuna wagonjwa wengi wa CORONA awatake waandishi waseme ukweli wasiogope.

 
Waandishi wanapenda kwani kupewa kesi za kuhujumu uchumi?
Serikali ilisem wao ndo watahusik n taatifa zote waandishinwanazipnda familia zao musoma wiki imepita sasa kuna kifo cha korona awajasem watu mpk video tunazo ila una mute kimya


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Si aseme yeye... ana Twitter, Instagram, Youtube, Facebook Tiktok. Nani kamzuia kusema?
 
Wakili wa Kijitegemea, Alberti Msando ametoa msaada wa barakoa 100 pamoja na vitakasa mikono 100 kwa waandishi wa habari Mkoa wa Arusha ili kujikinga na maambukizi ya Covid-19 kutokana na kazi yao kuwa na mwingiliano wa watu.

Akikabidhi msaada huo leo kwenye Ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha(APC) kupitia kwa Mwenyekiti wa chama hicho, Claud Gwandu, Msando alisema wanahabari ni watu muhimu katika kutafuta habari hivyo hatua ya kuwapatia barakoa na vitakasaa mikono itawawezesha kupambana na ugonjwa huo.

Alisema wanahabari ni watu muhimu katika kutoa taarifa sahihi za kudhibiti ugonjwa huo ikiwemo kuelimisha jamii juu ya maambukizi ya ugonjwa wa Korona ikiwemo kuhakikisha wanafuata taratibu zote zinazotakiwa katika kujikinga na ugonjwa huo.

Alisema wanahabari wananchango mkubwa katika utoaji wa taarifa zao ikiwemo kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi licha ya ugonjwa huu wa Korona kuwepo kwa jamii.

"Lazima mchukue tahadhari ya ugonjwa huu wa Corona kwa kuandika habari sahihi na kutoa habari kwa wananchi hivyo ni lazima muandike habari ili wananchi wajue "

Naye Mwenyekiti wa APC, Gwandu alishukuru kwa msaada huo kwa wanahabari ambao utawasaidia kujikinga na ugonjwa huo na kutoa rai kwa wadau wengine kujitoa kusaidia wanahabari katika kupambana na ugonjwa huu wa Corona.

Pia wanahabari wengine wa Mkoa wa Arusha Lillian Joel Uhuru na Cynthia Mwilolezi wa Nipashe walishukuru kwa msaada huo ambao utawasaidia kujikinga na maambukizi ya Covid - 19.

Ends....


View attachment 1433259View attachment 1433260View attachment 1433261

Sent using Jamii Forums mobile app
Barakoa 100...

Barakoa 1=Tshs 250.

Vitakasa mikono 1= 350.

Amejitahidi kwa waandishi wetu hao wa bahasha za kupigia brush viatu vyao.

Sent using iphone pro max
 
acheni siasa chafu...ebu msikilize hoja zake
Hana hoja badala ya kujiuliza ni nini kimefanya waandishi wamekuwa waoga analeta story za kuwapa moyo, wakipata matatizo atawasaidia? Serikali ya chama chake ndio imekandamiza uhuru wa habari mpaka tumefika hapa. Hakuna habari, ni sifa tu kwa serikali. Watu wakijaribu kutafuta na kutupatia habari wanapigwa kesi zisizo na dhamana. Afanye yeye, uzuri siku hizi channel za kufikia wananchi ni smartphone na internet yako.

Kila mtu anapenda kurudi jioni nyumbani kukutana na familia yake.
 
Back
Top Bottom