Akinyi Must Die (Ni lazima Akinyi Afe)

UMUGHAKA

JF-Expert Member
Sep 1, 2021
2,157
10,718
AKINYI MUST DIE (NI LAZIMA AKINYI AFE) - 01


Mvua kubwa iliyoambatana na ngurumo,radi na upepo mkali zilikuwa zikilindima Kaskazini mashariki mwa Tanzania katika jiji la Mwanza,maeneo ya Buswelu.Ilikuwa ni mvua kubwa kiasi kwamba kila raia alishitushwa na namna mvua ile ilivyokuwa ya kuogofya kwasababu haikuwahi kutokea mvua kubwa kama ile kwa miaka ya karibuni!

Sauti ya kike "Mama Deoooooooo....!,mama deoooooo....!,jamani mama deo njoo uone!"

Ilikuwa ni sauti ya mwanamke mmoja aliyekuwa akikinga maji ya mvua akimuita mwenzie.

Mama deo " Jamani Jeny kuna nini?"

Jeny " Hebu tizama!"

Mama deo " Nitizame nini!?"

Mama deo " Aahh jamani,mbona wanawake wanakuwa katili na wenye roho mbaya kiasi hiki!"

Aliendelea " Huyu si mtoto?"

Jeny " Ndiyo maana nimekuita mwenzangu uje uangalie maana nimeshituka kukiona hichi kichanga"

Mama deo " Aliyekiweka hapa nani?"

Jeny " Mimi sijui,nilipotoka nje kukinga maji nimekuta kimenyeshewa halafu kinalia"

Mama deo " Hebu ingia ndani kwangu niletee kitenge changu kipo nyuma ya mlango"

Alikuwa ni mtoto kichanga ambaye alikuwa ametelekezwa kando ya nyumba ya mzee Masumbuko ambako kwa muda huo Jeny na mama Deo walikuwa miongoni mwa wapangaji,haikujulikana ni nani alimtelekeza mtoto huyo na kwanini alifanya hivyo.

Mama Deo " Jamani halafu kazuri!"

Aliendelea kusema " Ngoja nimsubiri Baba deo akirudi twende kwa mjumbe tukaripoti"

Haikuchukua muda Baba Deo aliporudi kutoka kwenye mihangaiko yake ya kila siku,mke wake alimueleza kila kitu kuhusu kichanga kile na walishauriana kwa jioni hiyo kuelekea kwa mjumbe ili kutoa taarifa.

Kwakuwa mama Deo alikuwa na mtoto mmoja wa kiume ambaye aliitwa Deogratius,alimueleza mjumbe kwamba angekaa na huyo mtoto kama binti yake na angemlea,na endapo mzazi wake angepatikana basi wangemrejeshea.
Mpaka wakati huo hakuna aliyekuwa akifahamu mama wa kichanga hicho ni nani na kwanini ametelekeza mwanaye!.Mjumbe alimruhusu mama deo amchukue yule kichanga na endapo kungetokea sintofahamu basi ilipaswa wampe taarifa mjumbe.

Ilipofika usiku wa saa 3 mvua ikiwa imekata,basi ilisikika sauti ya bwana mmoja ambaye kwa namna alivyokuwa akiongea hapana shaka ungefahamu alikuwa amelewa chakali.

Mlevi "Nyieee watu wa nyumba hii,nifungulieni mlango"

Aliendelea kugonga mlango wa ile nyumba huku akitukana matusi ya nguoni.

Aliendelea "Nyie nguruwee,fungua mlango haraka"

Haikuchukua muda mlango wa nyumba ulifunguliwa na mmoja wa wapangaji wa ile nyumba!

Jamaa mpangaji "Unasemaje?"

Mlevi "Wewe ni nani?"

Jamaa mpangaji "Nimekuuliza unasemaje?"

Mlevi "Nataka mtoto wangu"

Jamaa mpangaji "Mtoto wako?,mtoto wako yupi?"

Sasa wakati wanajibishana pale mlangoni,Baba deo alifungua mlango wa chumba chake maana ilikuwa usiku na kelele zilimshitua.

Baba Deo "Alex mambo vipi,mbona kuna kelele?"

Alex "Huyu jamaa sijui katokea wapi,halafu kalewa kishenzi!"

Baba Deo "Anasemaje?"

Alex "Hebu njoo umsikilize"

Baba deo alisogea mpaka pale mlangoni na kutaka kufahamu ni nini kilikuwa kikiendelea.

Baba Deo aliuliza "We mzee unasemaje?,mbona unasumbua watu wamelala?"

Mlevi "Nahitaji mtoto wangu"

Yule Jamaa aliyekuwa amelewa alikuwa mtu mzima wa makamo na aliendelea kusema kwa sauti ya ulevi.

Baba Deo "Hebu ondoka hapa umelewa"

Japo alikuwa amelewa lakini alionekana kumaanisha alichokuwa akizungumza!.

Mlevi "Nimesema nataka mwananguuuu!"

Yule mzee alibwata kwa ukali kidogo mpaka wapangaji wa vyumba vingine ilibidi waamke kuja kutazama ni nini kilikuwa kikiendelea.Baada ya jamaa kuwa mkali na kukomalia mlangoni,Baba deo alitaka kufahamu na kumsikiliza yule jamaa kwa makini.

Baba Deo "Mwanao yupi unaye mtaka?"

Jamaa baada ya kuona wapangaji wengine wametoka nje kuja kuona ni mtu gani aliyekuwa akiwapigia kelele usiku huo,ilibidi awasimulie namna ilivyokuwa.

Mlevi " Wakati natoka kwa mama Ntalama kunywa pombe,nilipita uchochoroni kukojoa,wakati nakojoa ghafla nilisikia mtoto analia alikuwa kwenye sandarusi"

Aliendelea kusema " Ilibidi nisogee kufunua ili nione kulikuwa na nini,nilipofungua nikakuta ni mtoto mchanga analia,sasa kwakuwa mvua ilikuwa inataka kunyesha nikambeba na kuondoka nae,sasa mimi nakumbuka nilimuweka hapa nje,hivyo naombeni mtoto wangu"

Baada ya kusimulia kisa chote namna ilivyokuwa,kila mtu pale ndani alishangaa.

Baba Deo "Sasa wewe ulimuacha hapa wewe ukaenda wapi?"

Mlevi "Nisingeweza kupanda kule juu ninapoishi na yule mtoto kwakuwa nilikuwa nimelewa,nilimuacha hapa ili niende kwa mama Kichikutula kumwambia aje amchukue mtoto"

Baba Deo "Huyo mama Kichikutula ni nani?"

Mlevi "Ni mpenzi wangu"

Mama deo " Sasa kama wewe ndiye ulimuweka hapa huyo mtoto,kwanini ulimuacha hapa na hiyo mvua au ulitaka afe halafu tupewe mada kesi?"

Mlevi " Wakati nipo kwa mama Kichikutula mvua ilianza kunyesha na sikuweza kutelemka tena huku chini kwasababu mvua ilikuwa kubwa"

Jamaa aliongea kwa kujiamini kulikosindikizwa na sauti ya kilevi yenye dharau na jeuri ya kutosha.Kwakuwa ile familia ya mama deo haikutaka makuu ilibidi wamueleze kwamba yule mtoto walimchukua na wamesharipoti kwa mjumbe na kama ikiwezekana yeye akapumzike pombe zimuishe kichwani na kesho yake wangeamkia kwa mjumbe tena!.Kila mtu alitaka kufahamu mama wa yule mtoto ni nani na kwa nini alimtelekeza mwanaye aliyekuwa binti mzuri asiyekuwa na hatia.

Asubuhi na mapema yule jamaa aliyekuwa Mlevi ule Usiku na mpenzi wake aliyekuwa akiitwa mama Kichikutula walidamkia pale kwenye nyumba ya mzee Masumbuko ili kuangalia uwezekano wa kumpata yule mtoto.Waliondoka wakaongozana wote pamoja na mtoto kuelekea kwa mjumbe wa mtaa.Walipofika kwa mjumbe walieleza namna ilivyokuwa,mjumbe alishauri kulikuwa na ulazima wa kwenda polisi ili taratibu nyingine za kisheria zifuate mkondo.Hawakuchukua muda wakaondoka kuelekea kituo cha Polisi cha Nyakato ili taratibu za kipolisi zichukue nafasi.

Baada ya kuchukuliwa maelezo muda mrefu,polisi walishauri yule mtoto aendelee kutunzwa na mama Deo huku wakiendelea na upelelezi wa kujua mama wa mtoto ni nani na kwanini alitupa mtoto wake!.Polisi walisema upepelezi ungechukua muda wa siku kadhaa na ikiwa ungekamilika wangejulishwa.Polisi walisema yule jamaa aliyemuokota mtoto wangebaki nae kwa masaa kadhaa kwa ajili ya mahojiano na kisha wangemruhusu aondoke.

Siku 72 zilitosha kabisa kwa maafisa upelelezi wa Jeshi la polisi kitengo cha makosa ya jinai kutoka kituo kikuu cha polisi Jijini Mwanza kukamilisha upelelezi na uchunguzi wa uhalifu wa kutelekezwa kwa binti mchanga aliyetupwa na mama yake katika kata ya Buswelu,wilaya ya Ilemela,jijini Mwanza,Tanzania.

Mwenyekiti "Nimepokea wito kutoka kituo cha Polisi cha wilaya,nami nimewaiteni yatupasa tuongozane".

Ilikuwa ni sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Bulola "A" aliyekuwa akiwapa taarifa mjumbe wa eneo husika pamoja na wahusika akiwemo mama Deo na yule jamaa aliyemuokota mtoto.

Hawakutaka kupoteza muda waliongozana kwa pamoja mpaka kituo cha polisi wilaya ya Ilemela.

Afande "Jina langu ni Cosmas Mchumajanga ,nina Cheo cha Constable wa Polisi pia ni mpelelezi wa makosa ya Jinai katika Kanda ya kipolisi ya Wilaya ya Ilemela pamoja na Nyamagana"

Aliendelea "Wewe uliyemuokota mtoto Ndiye Stephano?"

Jamaa aliyemuokota mtoto "Ndiyo afande,ni mimi"

Afande Cosmas " Ok,hebu kaa hapo"

Afande Cosmas "Sasa kulingana na upelelezi uliyofanywa na askari wetu mahiri,unaonyesha mama wa mtoto alifariki siku ileile ambayo wewe ulimukota yule mtoto,nadhani hapo awali unakumbuka tulikujoji na ukatoa ushirikiano"

Stephano "Ndiyo afande"

Afande Cosmas "Taarifa nilizopokea mpaka sasa hivi kwenye kabrasha zangu hizi nikiwa kama mkuu wa kitengo cha upelelezi kituoni hapa ni kwamba,yule mwanamke alikuwa na watoto mapacha,mtoto mmoja hajulikani alipo,bado tunaendelea kufuatilia kwa karibu na hivi karibuni tutapata taatifa rasmi"

Mwenyekiti wa Mtaa "Kwahiyo afande waharifu wa mauaji wamekamtwa?"

Afande Cosmas "Hapana,ila bado askari wangu wanaendelea kufuatilia kwa ukaribu,unajua baada ya upelelezi inaonekana yule mwanamke alikuwa ametekwa,sasa watu tuliyowahoji kwenye maeneo husika wanasema lile eneo ambalo huyu bwana Stephano alilomuokota yule mtoto,walikuja watu wakiwa wamevaa vinyago (mask) usoni wakiwa wawili akiwemo na mwanamke mmoja ambaye yeye hakuvaa kinyago,sasa wanasema baada ya kushuka kwenye gari aina ya Prado lisilokuwa na namba za usajili walimshusha mwanamke mmoja aliyekuwa na watoto wadogo wakaanza kumpiga,na namna alivyokuwa dhaifu inasemekana walianza kumpiga kabla ya kuletwa pale"


Afande Cosmas aliendelea "Sasa nadhani wale jamaa walipoona watu wameanza kuwa wengi wakishangaa kilichokuwa kikiendelea wakamchukua yule mama wakampakia kwenye gari wakaondoka naye,nadhani lengo lao ilikuwa kumuua yeye na watoto wake, nadhani wakati wanaondoka hawakujali kwamba kuna mtoto mmoja wa yule mwanamke walimuacha pale chini na lengo lao walidhani angekufa lakini kama mjuavyo ya Mungu huwa ni mengi "

Mama Deo "Kwahiyo afande yule mtoto mwingine hajapatikana?"

Afande Cosmas "Kiukweli yule mtoto hatujampata,ila kama nilivyosema bado askari wangu mahiri wanaendelea kulifuatilia hili tukio kwa ukaribu na kila kitu kitaenda sawa,naomba tu mnipe ushirikiano wenu kila ninapowahitaji"

Mwenyekiti wa Mtaa "Kwahiyo Afande yule mwanamke ndugu zake wameuchukua mwili wake?"

Afande Cosmas "Hapana,kwa namna alivyokuwa ameharibika imebidi jeshi la Polisi kwa kushirikiana na manispaa wameona iwe busara kuuhifadhi ule mwili,unajua mwili wenyewe sisi tuliukuta kule Nyashishi,kiukweli ulikuwa umeharibika sana,hao washenzi tutawapata tu maana mkono wa serikali ni mrefu na lazima sheria itachukua mkondo wake,wala msiwe na hofu"

Mama Deo "Ni kweli huyo mwanamke ndiye mama wa huyu mtoto afande?"

Afande Cosmas "Sisi tuna mkono mrefu sana na tumehakikisha ndiye,siwezi kusema hapa kila kitu ila kwa taarifa za kiiterejensia siwezi kueleza tumepata wapi taarifa,kama nilivyosema msiwe na wasiwasi nyie subirini tu mtaona namna jeshi lenu linavyofanya kazi kwa weledi na umakini mkubwa"

Afande Cosmas aliendelea "Basi sawa,nyie kaendeleeni na shughuli zenu na tutakapowahitaji nadhani tutawajulisha ili mtupatie ushirikiano"

Haikuwa siku nzuri sana kwa mama deo maana kama mwanamke alikuwa na kila sababu ya masikitiko.

Mama Deo "Daaah!,kuna watu wana roho mbaya kama shetani"

Mjumbe wa mtaa "Wala hata usijali shemeji watajulikana tu,hii serikali iko makini"


Waliianza safari ya kurejea makwao asubuhi hiyo,njiani kila mtu alikuwa akisema lake ilimradi tu kunogesha maongezi.

Kadiri siku zilivyosonga ilimlazimu mama deo kumlea yule binti kama mwanae.


Itaendelea ..............
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom