Airbus A380 kwa mara ya kwanza imetua Tanzania uwanja wa JNIA

A380 imetua JNIA kwa dharura kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya huko Mauritus ilikokuwa ikielekea.

---------
Ndege kubwa aina ya Airbus A380 mali ya Shirika la Ndege la Emirates imetua kwa dharura katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) uliopo jijini Dar es Salaam, baada ya kushindwa kutua Mauritius kutokana na hali mbaya ya hewa.

Mauritius wanatulisha ndege kubwa hivyo sisi tunashindwa? Kha! Kazi mapangaboy tu.
 
Dar
IMG-20180424-WA0016.jpg
IMG-20180424-WA0015.jpg
IMG-20180424-WA0013.jpg
 
Mkuu unaambiwa ni mara ya kwanza airbus 380 kutua Tanzania.
Sasa we huoni kuwa ni maendeleo kwenye awamu hii ya tano.
Tulikuwa tukisikia yanatua huko kwa wenzetu sasa leo limetua hapa hapa Tz hapa naandika hii msg nikielekea Airport kuomba walau nipige selfie nimegusa tairi.

Ngoja na mm nishangilie maana nimeona juhudi za JPM kufanya hali ya hewa kua mbaya Mauritius. Tunaomba aendelee kukaza uzi hali izidi kua mbaya ziendelee kutua na zingine kwa wingi. Naunga mkono juhudi za Raisi
 
Mkuu unaambiwa ni mara ya kwanza airbus 380 kutua Tanzania.
Sasa we huoni kuwa ni maendeleo kwenye awamu hii ya tano.
Tulikuwa tukisikia yanatua huko kwa wenzetu sasa leo limetua hapa hapa Tz hapa naandika hii msg nikielekea Airport kuomba walau nipige selfie nimegusa tairi.
sasa niambieni jamani kuna mzee mmoja wa jiji yeye kazi yake kukagua hasa ndege za nje. hakuenda kuishuhudia kweli na kuikagua?maana imetua kwenye mkoa wake
 
Bombardier?!! Acha utani mzee kulinganisha vitu tofauti.
Kuna kipofu mmoja alipata kutibiwa macho akaona siku hiyo alipoona kitu cha kwanza kukiona ilikuwa ni punda, Baada ya kuona kwa muda mfupi akarudi kwenye hali yake ya kawaida.

Alipokuwa anaambiwa kuwa gari ni kubwa alikuwa analinganisha na ukubwa wa punda kwa kila kitu hadi nyuma.
 
Back
Top Bottom