Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,149
November 10, 2009
Chuo kikuu kimoja nchini Brazili kimemfukuza chuo kikuu mwanafunzi wake wa kike aliyejaribu kuingia darasani akiwa amevaa sketi fupi sana na kusababisha mtafaruku mkubwa sana chuoni hapo.
Chuo kikuu binafsi cha Bandeirante University cha mjini Sao Bernardo do Campo, nje kidogo ya jiji la Sao Paulo, kimemsimamisha masomo mwanafunzi wake wa kike Geisy Arruda mwenye umri wa miaka 20 ambaye alisababisha mtafaruku mkubwa sana chuoni hapo mwezi uliopita baada ya kujaribu kuingia darasani akiwa amevaa kimini kifupi sana cha rangi ya pinki.
Taarifa iliyotolewa na chuo hicho ilisema kwamba Arruda alifanya kitendo ambacho kipo nje ya maadili ya jamii na misingi ya taaluma.
Arruda alikuwa gumzo kwenye vyombo vya habari mwezi uliopita baada ya kuokolewa na polisi kutokana na kipigo na mashambulio ya kijinsia aliyokuwa akifanyiwa baada ya kuingia darasani akiwa amevaa kimini kilichokaa kimitego mitego.
Ilimbidi Arruda ajisitiri kwa kutumia koti la profesa wake huku akisindikizwa na polisi kutoka nje ya chuo hicho kufuatia matusi na mashambulio ya kijinsia aliyokuwa akifanyiwa na wanafunzi wenzake wenye hasira.
Baada ya tukio hilo la oktoba 22, Arruda amekuwa akitokea kwenye televisheni mbali mbali za Brazili akisema kuwa anapata tabu sana kurudia maisha yake ya kawaida baada ya kudhalilishwa.
Uongozi wa chuo kikuu hicho ulibandika tangazo la kumsimamisha masomo Arruda siku ya jumapili.
Tangazo hilo lilisema kuwa Arruda amesimamishwa masomo kwa kuingia darasani akiwa amevaa vazi lisilofaa na lisiloendana na mazingira ya chuo kikuu.
Akielezea kusimamishwa kwake masomo kwasababu ya kimini alichovaa, Arruda alisema kuwa ameonewa.
"Mimi ndiye niliyedhalilishwa, imekuwaje nifukuzwe chuo?", alisema Arruda.
Arruda alisema kuwa amezisoma habari za kufukuzwa kwake chuo kwenye magazeti lakini hadi sasa bado hajapokea barua ya kusimamishwa masomo.
Arruda amesema kuwa uongozi wa chuo kikuu hicho ulimwambia kuwa utamruhusu aendelee na masomo yake chuoni hapo lakini aambatane na mlinzi wake wakati wote.
Chuo kikuu kimoja nchini Brazili kimemfukuza chuo kikuu mwanafunzi wake wa kike aliyejaribu kuingia darasani akiwa amevaa sketi fupi sana na kusababisha mtafaruku mkubwa sana chuoni hapo.
Chuo kikuu binafsi cha Bandeirante University cha mjini Sao Bernardo do Campo, nje kidogo ya jiji la Sao Paulo, kimemsimamisha masomo mwanafunzi wake wa kike Geisy Arruda mwenye umri wa miaka 20 ambaye alisababisha mtafaruku mkubwa sana chuoni hapo mwezi uliopita baada ya kujaribu kuingia darasani akiwa amevaa kimini kifupi sana cha rangi ya pinki.
Taarifa iliyotolewa na chuo hicho ilisema kwamba Arruda alifanya kitendo ambacho kipo nje ya maadili ya jamii na misingi ya taaluma.
Arruda alikuwa gumzo kwenye vyombo vya habari mwezi uliopita baada ya kuokolewa na polisi kutokana na kipigo na mashambulio ya kijinsia aliyokuwa akifanyiwa baada ya kuingia darasani akiwa amevaa kimini kilichokaa kimitego mitego.
Ilimbidi Arruda ajisitiri kwa kutumia koti la profesa wake huku akisindikizwa na polisi kutoka nje ya chuo hicho kufuatia matusi na mashambulio ya kijinsia aliyokuwa akifanyiwa na wanafunzi wenzake wenye hasira.
Baada ya tukio hilo la oktoba 22, Arruda amekuwa akitokea kwenye televisheni mbali mbali za Brazili akisema kuwa anapata tabu sana kurudia maisha yake ya kawaida baada ya kudhalilishwa.
Uongozi wa chuo kikuu hicho ulibandika tangazo la kumsimamisha masomo Arruda siku ya jumapili.
Tangazo hilo lilisema kuwa Arruda amesimamishwa masomo kwa kuingia darasani akiwa amevaa vazi lisilofaa na lisiloendana na mazingira ya chuo kikuu.
Akielezea kusimamishwa kwake masomo kwasababu ya kimini alichovaa, Arruda alisema kuwa ameonewa.
"Mimi ndiye niliyedhalilishwa, imekuwaje nifukuzwe chuo?", alisema Arruda.
Arruda alisema kuwa amezisoma habari za kufukuzwa kwake chuo kwenye magazeti lakini hadi sasa bado hajapokea barua ya kusimamishwa masomo.
Arruda amesema kuwa uongozi wa chuo kikuu hicho ulimwambia kuwa utamruhusu aendelee na masomo yake chuoni hapo lakini aambatane na mlinzi wake wakati wote.