ADHABU gani zinafaa kwa watoto?

Naungana nawe binhai,angalia sisi tulivyokuwa tunachapwa enzi zetu,na hapa tulipo sasa,viboko vinasaidia sana kwa watoto watukutu!!!

...........Fimbo muhimu jamani kwa watoto, haswa wale wenye umri mdogo.
Mie mwenyewe hadi kufika hapa fimbo zimenisaidia sana, nilivyokuwa mdogo nilikuwa mtundu mno baba alikuwa ananichapa na baada ya kunichapa ananiambia kwa nini amenichapa na niache kurudia hilo kosa.

Hivyo ni muhimu kuwaonya watoto kwa fimbo, samaki mkunje angali mbichi.
Kuna baadhi wazazi huwa wanakosea, mtoto anapokuwa mdogo haamchapi, ila akishakua mkubwa ndio hapo wanaanza kumpa viboko, mtoto ukija kumuonya kwa fimbo ukubwani huyu lazima atakuwa sugu tu.
Mithali 29:15A Fimbo na maonyo hutia hekima.
 
...........Fimbo muhimu jamani kwa watoto, haswa wale wenye umri mdogo.
Mie mwenyewe hadi kufika hapa fimbo zimenisaidia sana, nilivyokuwa mdogo nilikuwa mtundu mno baba alikuwa ananichapa na baada ya kunichapa ananiambia kwa nini amenichapa na niache kurudia hilo kosa.

Hivyo ni muhimu kuwaonya watoto kwa fimbo, samaki mkunje angali mbichi.
Kuna baadhi wazazi huwa wanakosea, mtoto anapokuwa mdogo haamchapi, ila akishakua mkubwa ndio hapo wanaanza kumpa viboko, mtoto ukija kumuonya kwa fimbo ukubwani huyu lazima atakuwa sugu tu.
Mithali 29:15A Fimbo na maonyo hutia hekima.
Pretty,
Pole kwa fimbo za utotoni.
Wazo lako kuhusu muhimu wa kutumia fimbo umelielezea kwa makini sana.
Nadhani hapa utapata upinzani mkubwa sana kwani kampeni kuhusu kukomesha matumizi ya fimbo ni kubwa sana.
Naona umetumia maandiko pia.
Tuone wadau wengine wata-react vipi.
 
Ukitaka kufaham umuhim wa viboko angalia watoto wa Kizungu wazazi wanahangaika hadi wanatafuta supanani awasaidie. Wakati fulani inakuwa ni ishu ya kusolve kwa vibao viwili vya haraka. Maana unamkuta mama wa kizungu analia eti mwanae wa miaka 2 hamsikii. Ohps, mueleweshe haiwezekani unamchapa tuvibao tuwili twa haraka then anatulia. Sasa km mama unalia mtoto afanyaje?
Ila nakubaliana na wengine pia kwenye ishu ya ulezi hakuna formula inatakiwa katoto bado kadogo ukaonyeshe huwa unakasirikaje na unakasirishwa na nini
 
Ukitaka kufaham umuhim wa viboko angalia watoto wa Kizungu wazazi wanahangaika hadi wanatafuta supanani awasaidie. Wakati fulani inakuwa ni ishu ya kusolve kwa vibao viwili vya haraka. Maana unamkuta mama wa kizungu analia eti mwanae wa miaka 2 hamsikii. Ohps, mueleweshe haiwezekani unamchapa tuvibao tuwili twa haraka then anatulia. Sasa km mama unalia mtoto afanyaje?
Ila nakubaliana na wengine pia kwenye ishu ya ulezi hakuna formula inatakiwa katoto bado kadogo ukaonyeshe huwa unakasirikaje na unakasirishwa na nini

Kusema ile kweli fimbo zinasaidia sana tu kwa mtoto,suala ni kwa mchapaji anachapaje.Mie nakumbuka pale mwanza kulikuwa na mwalimu anaitwa mwalimu Aron alifundisha Nyamagana kisha akaamia Nyakabungi,nasikia sasa yuko Nyakato primary school,wenyewe tulikuwa tunampenda kumuita Mr Aron.Huyu jamaa katika Tuition yake alikuwa anachapa bakora za maana tuu na bado darasa lilikuwa linajaa mpaka watu wanakaa chini.To me this is my best teacher of my life time.Huyu amenijengea msingi wa kupenda kusoma na kuwa makini pia ingawa alinifundisha tuition tuu.Alikuwa mwalimu mzuri sana wa hesabu,mcheshi sana ila rafiki yangu ukafanya ndivyo sivyo ni lazima atakuchapa na fimbo zake mbili tuu lakini zilikuwa zinauma week nzima na alikuwa awezi kukuchapa bila ya kosa.

Bado nakumbuka yale maneno yake mpaka leo,"Katoto mimi siwezi kula 1000 ya baba yako halafu wewe unaleta upumbavu hapa,hapa ni bakora kwa kwenda mbele,utaamua mwenyewe kusuka au kunyoa"
 
Mtandao wa Kisheria wa Watoto umetishia kuishitaki serikali iwapo itatengua maamuzi ya kufutwa kwa matumizi ya viboko kwa watoto mashuleni.

Hii imekaaje wakuu.
 
Back
Top Bottom