5,000 wanasubiri visu na nyembe!!!!...hii mbaya kabisaa...!!!!!!!!!

Thansk Mwalimu... langu haswa lilikua swali la kama kutahiri wanaume pia ni ukatili au ni wanawake tu

Nafikiri inategemea na namna zoezi zima linavyoendeshwa.

Hospitali wanakuwekea ganzi kwa hiyo husikii maumivu wakati ule at least.

Hizi zinazofanywa na ngariba kavu kavu ni ukatili wa aina yake ( nionavyo) na pia kuna suala la usalama wa zana zinazotumika na mambo mengine ya infection.

Serikali walau ingechukua jukumu la kutoa mafunzo ya kiafya kwa wahusika (Kama hawafanyi hivyo sasa)
 
Si madogo!

Katika suala zima serikali inatuhakikishia vipi usalama wa kiafya wa hao wanao tahiriwa?

Serikali imehakikisha vipi suala la kuzuwia maradhi ya kuambukiza?
serkali ipi? iliyo chini ya ccm ama iliyochini ya CHADEMA na wananchi?
kama ni li ya ccm, ukeketaji hiyo ni moja ya sera yao
 
Nafikiri inategemea na namna zoezi zima linavyoendeshwa.

Hospitali wanakuwekea ganzi kwa hiyo husikii maumivu wakati ule at least.

Hizi zinazofanywa na ngariba kavu kavu ni ukatili wa aina yake ( nionavyo) na pia kuna suala la usalama wa zana zinazotumika na mambo mengine ya infection.

Serikali walau ingechukua jukumu la kutoa mafunzo ya kiafya kwa wahusika (Kama hawafanyi hivyo sasa)


Hakuna ukatili hapo, hapo kuna suala la kupima ujasiri wa kijana. Kwakuwa mtu anavuka toka kundi la utoto kuingia kundi la vijana ambalo ndilo linalotegemewa kulinda jamii husika, ni lazima kupitia huu mtihani. Kwa mfano wamasai wao kabla ya kutahiriwa kijana anatakiwa kuua simba au kuiba ng'ombe toka kabila shindani, baada ya hapo ndipo sasa anakumbana na kisu kavu kavu. Kwa upande wetu wengi siku hizi wakishatoka kukabiliana na kisu huwa wanakwenda hospitali kwa ajili ya kupata matibabu ili iwasaidie kupona haraka zaidi.

Na usalama siku hizi unazingatiwa sana, kwani wakati wa tohara huwa kunakuwepo na wataalamu wa afya wanashirikiana kwa karibu sana na hawa mangariba ili kuona kwamba visu vinavyotumika vina usalama wa kutosha.
 
hili limekugusa sana eeeh? mie sio mwanaharakati! mie ni mchaga na mama yangu ni mkurya,
mama yangu aliachika kwa sababu she was circusmcised...
na najua ndugu zangu wengine wenye matatizo na ndoa zao kwa sababu walikuwa circumsised..!
mila potofu ni mila potofu tu,haijalishi mmeifanya kwenye kabila lenu tangu mwanzo wa dunia!
ulipo bold niliona documentary BBC ONE,sikumbuki ni kabila gani..kama sio ethiopia ni sudani ambako wanakata mashavu ya uke na kajisehemu kadogo tu ka clitoris...ila hawaking'oi chote,halafu wanakushona na uzi!sasa kama kwenu mnfanya tofauti ni nyie!...hio haimaanishi watu wote wanaocircumsise wanafanya kama nyie....

kuhusu swala la takwim hata kama angekuwa anafanyiwa mtu mmoja,hii kitu ningeipinga,...ni mbaya,ukiukaji wa haki za binadamu..period!

Fab,

Usitumie kisingizio cha mama yako kuachika kuwa sababu ni kukeketwa. Wakati baba yako anamuoa mama yako bila shaka alijua kwamba mama kapigwa kiwembe lakini bado tu aliendelea nae hadi ukazaliwa. Kama kuna dada zako nao wana matatizo kwenye ndoa zao bado nasema usisingizie ukeketaji, inawezekana wao wenyewe ndo wameshindwa kuzitunza ndoa zao, na bila shaka hao waume zao walipoanzana nao hadi kufikia kuwaoa walijua kwamba wamepigwa viwembe. Halafu kitu kingine manka, mimi nimekaa moshi miaka 7, ninawafahamu vizuri sana wachaga, kwahiyo huwezi kunidanganya kuhusu sababu za wanawake wa huko kuachika, there are number of issues!!

Ni dhahri kwamba kwa mtu kama mimi kuja hapa kutetea hii mila wengi wetu hawawezi kunielewa, lakini hao wasionielewa ni kwakuwa wanaangalia upande mmoja tu pasipo kutaka kujua na upande wa pili. Ukeketaji hauwezi kumalizika kwa siku moja, ni suala la muda mrefu kidogo. Kwahiyo kinachofanyika ni kuendelea kutoa elimu kadri inavyowezekana, na hiyo imesaidia kuboresha mazingira ya zoezi lenyewe na baadhi ya wasichana kuona hakuna sababu ya kutokeketwa na at the same time wanaume nao kufahamu kwamba hata mwanamke asiyekeketwa bado anafaa na anaweza kuwa mke bora. Kwa maana kwamba inahitajika muda ili wazee wetu wa mila kuona na kutafakari njia mbadala kwa hawa dada zetu kuweza kupatiwa mafunzo haya ya kuwavusha rika, toka utoto na kuingia ujana pasipo kupitia ukeketaji. Kwa kuwa wazee bado wanaamini kwamba ni muhimu kila msichana akapitia huo mtihani na kwa kuzingatia elimu na ushirikiano na wataalamu wa afya ndio sababu ukeketaji wa sasahivi ni kama kiashiria tu, kwakuwa wanakata ile kitu kidogo sana kiasi ambacho haina athari yoyote kwa msichana. Bahati mbaya hii kitu watu wengi tunaijadili kiushabiki zaidi pasipo kujua undani wake na ukweli wake.

Mwisho, Fab bado nakusubiri unithibitishie kwamba hawa wanawake hawafiki kileleni!!:teeth:
 
Hakuna ukatili hapo, hapo kuna suala la kupima ujasiri wa kijana. Kwakuwa mtu anavuka toka kundi la utoto kuingia kundi la vijana ambalo ndilo linalotegemewa kulinda jamii husika, ni lazima kupitia huu mtihani. Kwa mfano wamasai wao kabla ya kutahiriwa kijana anatakiwa kuua simba au kuiba ng'ombe toka kabila shindani, baada ya hapo ndipo sasa anakumbana na kisu kavu kavu. Kwa upande wetu wengi siku hizi wakishatoka kukabiliana na kisu huwa wanakwenda hospitali kwa ajili ya kupata matibabu ili iwasaidie kupona haraka zaidi.

Na usalama siku hizi unazingatiwa sana, kwani wakati wa tohara huwa kunakuwepo na wataalamu wa afya wanashirikiana kwa karibu sana na hawa mangariba ili kuona kwamba visu vinavyotumika vina usalama wa kutosha.

Haya jamani ......nashukuru hiyo mila kwetu haipo manake mtoto wangu hasa wa kike sitaweza kumpa pain ya kuchezea kiwembe kavu kavu.
 
Fab,

Usitumie kisingizio cha mama yako kuachika kuwa sababu ni kukeketwa. Wakati baba yako anamuoa mama yako bila shaka alijua kwamba mama kapigwa kiwembe lakini bado tu aliendelea nae hadi ukazaliwa. Kama kuna dada zako nao wana matatizo kwenye ndoa zao bado nasema usisingizie ukeketaji, inawezekana wao wenyewe ndo wameshindwa kuzitunza ndoa zao, na bila shaka hao waume zao walipoanzana nao hadi kufikia kuwaoa walijua kwamba wamepigwa viwembe. Halafu kitu kingine manka, mimi nimekaa moshi miaka 7, ninawafahamu vizuri sana wachaga, kwahiyo huwezi kunidanganya kuhusu sababu za wanawake wa huko kuachika, there are number of issues!!

Ni dhahri kwamba kwa mtu kama mimi kuja hapa kutetea hii mila wengi wetu hawawezi kunielewa, lakini hao wasionielewa ni kwakuwa wanaangalia upande mmoja tu pasipo kutaka kujua na upande wa pili. Ukeketaji hauwezi kumalizika kwa siku moja, ni suala la muda mrefu kidogo. Kwahiyo kinachofanyika ni kuendelea kutoa elimu kadri inavyowezekana, na hiyo imesaidia kuboresha mazingira ya zoezi lenyewe na baadhi ya wasichana kuona hakuna sababu ya kutokeketwa na at the same time wanaume nao kufahamu kwamba hata mwanamke asiyekeketwa bado anafaa na anaweza kuwa mke bora. Kwa maana kwamba inahitajika muda ili wazee wetu wa mila kuona na kutafakari njia mbadala kwa hawa dada zetu kuweza kupatiwa mafunzo haya ya kuwavusha rika, toka utoto na kuingia ujana pasipo kupitia ukeketaji. Kwa kuwa wazee bado wanaamini kwamba ni muhimu kila msichana akapitia huo mtihani na kwa kuzingatia elimu na ushirikiano na wataalamu wa afya ndio sababu ukeketaji wa sasahivi ni kama kiashiria tu, kwakuwa wanakata ile kitu kidogo sana kiasi ambacho haina athari yoyote kwa msichana. Bahati mbaya hii kitu watu wengi tunaijakidili kiushabi zaidi pasipo kujua undani wake na ukweli wake.

Mwisho, Fab bado nakusubiri unithibitishie kwamba hawa wanawake hawafiki kileleni!!:teeth:

nahisi wewe ndio unajadili kishabiki kwa sababu ni kabila lako...
kuhusu kuachika i blame,uwezo l(lack ofexperience)...ya baba when it comes to sex!!!by the time anamuoa mama hakujua tofauti...kati ya mwanamke aliyekeketwa na asiyekeketwa!.....siku alipoijua tofauti(alicheat of course)....hakutaka kumrudia mama tena,ameoa mpare kwa sasa...
huyo ndugu yangu mwingine,nilisikia mashitaka....kuwa hamu yake ya kufanya tendo la ndoa na mumewe hakuna,kwa sababu kila mara akifanya hafikishwi anapotaka......ndoa yao iko matatizoni,sasa walijua consenquences za wao kuoana ilhali mke amekeketwa?hilo sijui...

sijui nikuthibitishieje kuwa mwanamke aliyekeketwa hafiki kileleni,naona umezama kny mila yako,kiasi hutaki kuuuona ukweli uliopo mbele yako,...sehemu yenye nerves na senstive kwa mwanamke inayomfanya afike kileleni..ndiyo hio wanaikata during circumscion,...kama haipo utuambie ukiwa kama mwanaume unasugua wapi ili mkeo afike kileleni???
 
Fab

Labda hawa wenzetu wana utaalamu wa kufikia Gspot ya ndani all the time

Anyway kwa nilivyomuelewa Mwita ni kuwa ukeketaji wa sasa sio kama wa zamani, sasa wanakata kidogo tu (sijui kidogo ni kiasi gani) na pia kuna wataalamu wa afya wanakuwepo.

Mtazamo wangu binafsi ni kuwa sioni sababu ya kuwapa watoto pain isiyo na lazima (hata kama hawakati, wanachinja tu), tufanye nini mpaka tufike kwenye kuondoakana nayo hasa ikiwa wazee wanaona ni lazima, na wanaume wanafikiri mwanamke alokeketwa ndio bora (inayopelekea na mwanamke mwenyewe kutaka kutahiriwa)
 
Gspot ya ndani,mshindo wake hauna nguvu kama ule wa clitoris...
hata wanawake ni wachache sana wameweza kuufeel...
kumuwekea mwanao wa kike,complications kama hizi ni kumuonea...hata kama wanakata kidogo,wanapunguza surface area...ya hio sehemu inayotakiwa kuwa hit!what for?

tuendeleee tu kuelimishana taratibu...naamini watu kama wakina mwita,wakikombolewa kifikra...wataelimisha wenzao..juu ya mila hii potofu!:embarrassed::embarrassed:
 
akina kyekue wa kilimanjaro hawatahiri...
afu sio kwa vile mikoa mingine inafanya tohara na nyie mfanye..
hili jambo linatakiwa kupigwa vita kwa nguvu zote...,
mie namjua mtu ameshindwa kuolewa sababu ya hii kitu...
its soo unfair...
acha uongo,tena akina kyekue wanakutahiri ukiwa mkubwa maana wanaimani kuwa ukitahiriwa mdogo kinakua
 
acha uongo,tena akina kyekue wanakutahiri ukiwa mkubwa maana wanaimani kuwa ukitahiriwa mdogo kinakua

acha uongo,nimekaa moshi sijawahi kuona hiyo...kitu,anyway wenyewe watasema hapa!
 
nahisi wewe ndio unajadili kishabiki kwa sababu ni kabila lako...
kuhusu kuachika i blame,uwezo l(lack ofexperience)...ya baba when it comes to sex!!!by the time anamuoa mama hakujua tofauti...kati ya mwanamke aliyekeketwa na asiyekeketwa!.....siku alipoijua tofauti(alicheat of course)....hakutaka kumrudia mama tena,ameoa mpare kwa sasa...
huyo ndugu yangu mwingine,nilisikia mashitaka....kuwa hamu yake ya kufanya tendo la ndoa na mumewe hakuna,kwa sababu kila mara akifanya hafikishwi anapotaka......ndoa yao iko matatizoni,sasa walijua consenquences za wao kuoana ilhali mke amekeketwa?hilo sijui...

sijui nikuthibitishieje kuwa mwanamke aliyekeketwa hafiki kileleni,naona umezama kny mila yako,kiasi hutaki kuuuona ukweli uliopo mbele yako,...sehemu yenye nerves na senstive kwa mwanamke inayomfanya afike kileleni..ndiyo hio wanaikata during circumscion,...kama haipo utuambie ukiwa kama mwanaume unasugua wapi ili mkeo afike kileleni???
Fab samahani kusema hili,basi mamako ndio alikuwa na tatizo kitandani maana wapare WANAKEKETWA,so huyo stepmother wako amekeketwa
 
Fab samahani kusema hili,basi mamako ndio alikuwa na tatizo kitandani maana wapare WANAKEKETWA,so huyo stepmother wako amekeketwa

wewe kila kabila tanzania linakeketa?!!...get your facts right!
 
Gaijing ni kweli kabisa,siongelei ushabiki hapa nazungumzia jambo ambalo nina uhakika nalo kwa 100%

Kwa ufupi ni kuwa makabila mengi yanaendelea na suala hilo (au at least mpaka generation moja nyuma walikuwa wakifanya).

Nadhani hapa kinachojadiliwa sio kabila gani linafanya, kinachotakiwa kujadiliwa ni kile kitendo chenyewe. Ni sahihi? na kama si sahihi tutawezaje kukiondoa kwa njia za amani bila ya kuporomosheana matusi au kunyooshea vidole kwa kabila fulani.
 
Gspot ya ndani,mshindo wake hauna nguvu kama ule wa clitoris...
hata wanawake ni wachache sana wameweza kuufeel...
kumuwekea mwanao wa kike,complications kama hizi ni kumuonea...hata kama wanakata kidogo,wanapunguza surface area...ya hio sehemu inayotakiwa kuwa hit!what for?

tuendeleee tu kuelimishana taratibu...naamini watu kama wakina mwita,wakikombolewa kifikra...wataelimisha wenzao..juu ya mila hii potofu!:embarrassed::embarrassed:

Kwa taarifa yako mimi ni mtu niliye huru sana, labda wewe ndiye unahitaji kukombolewa. Hivi vitu dada yangu huvijui kabisaa, umekalia mambo ya kuambiwa sijui kusimuliwa ukichanganya na mama na dada zako kuachika basi umejaa ma-stress. Na ndio sababu sasa umekuwa embarrassed!! any way pole sana bibie.

Mimi ndiye naufahamu uzuri na ubaya wa mila zetu, sio wewe mchaga mama yangu. Gaijin amenielewa vizuri ninachozungumza, labda atakusaidia kukuelewesha. Nataka nikuhakikishie kwa mara nyingine, when it comes kwenye mila na utamaduni wangu ninaufahamu ubaya wake na uzuri wake wala huwezi kunidanganya katu. Na hata hatua zilizofikiwa katika issue hii ni kubwa sana. Serikali yenyewe ilianza kwa kutunga sheria kwenye wilaya ili kuwadhibiti watu lakini ilishindwa baada ya kutambua nguvu ya mila na wenye mila wenyewe, je unajua kilichofuata? je umejiuliza kwanini OCD alikuwa anashangaa? Elimu imekuwa ikitolewa hatua kwa hatua na huko mbeleni hii kitu itaisha tu lakini si haraka kama unavyotaka wewe. nilimwambia Gaijin mahalikwamba siku hizi wanakata ki-ccm, kama ukitaka kujua nini maana ya ki-ccm, tafuta muda wako uende Mara ukajifunze, najua moshi mnakeketa lakini ya kwenu ni tofauti na sisi! wakurya tuna waheshimu sana wazee wa mila, utasema mila potofu, sawa, lakini hizo ndizo zimetufikisha hapa tulipo leo. wakurya tunazidi kuongezeka kama yalivyo makabila mengine. Tuna familia zetu kizazi hadi kizazi na afya tele, na wakurya tunajua kutunza familia na tunaheshimu na kutambua ndoa na familia za wengine, upo hapo? tunayatambua mazingira yetu na tunakabiiana nayo vilivyo na tuna furahia Mungu kutuumba wakurya!!

i'm out for now, kama kuna issue zaidi tuonane jumatatu, naenda kusakata "litungu", unaifahamu hiyo kitu Fab?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom