30% Tu ya Samsung Galaxy S4 Kuwa na Core 8

ManiTek TV

JF-Expert Member
Jun 3, 2011
410
159
Samsung Galaxy S4 ndio simu ya kwanza kuwa na prosesa aina ya Exynos 5 yenye core 8 (Octa), ambayo ndio prosesa yenye nguvu kuliko zote katika soko la simu kwa sasa, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na jarida pamoja na mtandao wa teknolojia T3 ni asilimia 30 tu ya simu hizo ndio zitakuwa na prosesa hyo, na ni simu ambazo zitauzwa kwenye soko la UK, Marekani walishahakikishiwa kwamba Galaxy S4 za bara la Amerika ya Kaskazini zitakuwa na prosesa aina ya Snapdragon yenye kasi ya 1.9 GHz na core nne.

Samsung wanakhofia kwamba hawana muda wa kutosha wa kuzalisha aina hiyo ya prosesa na mauzo ya wapinzani kama vile HTC One na Sony Xperia Z yanapamba moto, hivyo ili kuongeza kasi ya uzalishaji Samsung watatumia prosesa za Snapdragon kwenye 70% ya simu hizo, zikiwemo pia zile zitakazouzwa mabara ya Ulaya na Asia.


Wadau wengi wanapata hisia kwamba Samsung wametoa tangazo la kutumia prosesa ya core 8 ikiwa kama ni sehemu ya kivutio cha mauzo ya simu yao, wakati mpango wao tangu awali si kutoa simu nyingi zikiwa na prosesa zenye core nne. Soko la Uingereza ni soko linalolipa sana hivyo Samsung wanamudu kutoa simu za gharama kubwa katika nchi hiyo. Kwa kawaida wengi kati ya wanaonunua simu za hali ya juu Uingereza hununua kwa njia ya mkataba, ambapo simu kama Galaxy S4 hutolewa bure iwapo mteja atakubali kulipa zaidi ya £30 kwa 3G au hata maradufu ya hizo kwa EE yenye huduma ya 4G kwa mwezi mmoja tu kwa muda wa miaka miwili.

Mteja huyo atanufaika kwa kuzungumza dakika kama baina ya 1000 au zaidi katika mtandao wowote, message mpaka ashindwe mwenyewe na data kwa ajili ya internet pia hazina kikomo kwa upande wa 3G ambapo 4G hupewa 8GB au pungufu kwa kila mwezi. Kampuni ya EE ambayo ni pekee ambayo inatoa huduma ya 4G nchini UK kwa sasa wameshatoa tangazo la simu ya Samsung S4 ambapo wateja watakao toa oda sasa hivi watailipia simu hiyo £79, mkataba wa miaka 2 na watapata vifaa (accessories) zenye thamani ya £54, mkataba ni miaka miwili kwa £41 kwa mwezi.

Wateja hao wataruhusiwa kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi pasipo na kikomo lakini data itaishia 1GB kwa mwezi. Hivyo mkataba huu si kwa ajili ya wenye kutmia intaneti zaidi, na hivyo faida halisi ya kutumia 4G haipo, lakini huu ni mtego kwani watakapopiliza kiwango cha data walichopewa basi watalazimika kulipia ziada ya data walizozitumia.

Hivyo bila ya shaka Samsung wanaelewa kuwa UK ni soko lenye faida kubwa ndio maana huko wanapeleka simu zenye core nane na masoko mengine ni core nne za kawaida huku wakijivunia kuwa ni simu yenye prosesa yenye kasi zaidi kama kwamba zote zina prosesa hiyo. Biashara inahitaji ujanja.

Kiutendaji tofauti baina aina mbili hizi za prosesa ni vigumu kuigundua kwa upande wa kasi au ufanisi, lakini kwa upande wa betri Exynos 5 yenye core nane inasadikiwa kuwa na ufanisi mkubwa kutokana na prosesa hiyo kuweza kutumia core zinazohitajika tu kwa aina mbali mbali za matumizi. Hii kinyume na matarajio ya kawaida ambapo ongezeko la core kimantiki ilikuwa iwe inakula betri zaidi. Hivyo ni matarajio kuwa watakaokuwa na SAmsung Galaxy S4 yenye Exynos 5 ya core nane hawatakuwa na matatizo ya kuishiwa betri kwa haraka ukilinganisha na wale watakaokuwa na S4 zenye Snapdragon.

CHANZO: http://www.gajetek.com/2013/03/30-tu-ya-samsung-galaxy-s4-kuwa-na-core.html

 
Tupe maoni yako kuhusu FM Radio kutokuwepo kwenye S4 .. batterry efficciency au nao wanataka kuwa na Music Store???
Pia, vipi kuhusu 4G?? Nasikia S4 haina hiyo capability.

Galaxy S4 inayo 4G capability, lakini huenda zile ambazo zitauzwa kwenye nchi ambazo hazina 4G zikawa hazina uwezo huo, kwa mfano Galaxy S3 zilizouzwa UK kabla ya EE kuanza kutoa huduma ya 4G zilikuwa hazina 4G.

Kuhusu betri ni vigumu kulizungumzia hili bila ya kuitumia simu, kwa hiyo sasa hivi si rahisi kusema chochote isipokuwa tu tunachoweza kuzungumzia ni uwezo au nguvu ya betri iliyotumika nayo ni 2600 MAh, baadhi ya specs za S4:
Gajetek Table.png
Source: Gajetek
Hata hivyo GSM Arena wameijaribu betri ya S4 na kuilinganisha na simu nyingine angalia table ya chini:
Screen Shot 2013-03-30 at 21.16.58.png
Source: GMS Arena

Kuhusu FM Radio ni kwamba S4 inao uwezo huo, Chip iliyotumika kwenye simu hiyo ni Broadcom BCM4335 ambayo ina
802.11ac WiFi, Bluetooth 4.0 na FM radio.

Ikiwa unalenga kununua simu hiyo basi toleo la UK ndio litakuwa poa kuliko US au Mainland Europe.
 
It Means Hapo Kwa watakao nunua s4 yenye snap dragon kuna punguzo?? aubei Ile Ile?
 
nimependa specs zake ,ila kutokuwa na fm ni drawback kwa nchi kama Tanzania, maana zaidi ya asilimia 90 tunapata habari kupitia radio.

General 2G Network GSM 850 / 900 / 1800 / 1900
3G Network HSDPA 850 / 900 / 1900 / 2100
4G Network LTE
SIM Micro-SIM
Announced 2013, March
Status Coming soon. Exp. release 2013, April 26th
Body Dimensions 136.6 x 69.8 x 7.9 mm (5.38 x 2.75 x 0.31 in)
Weight 130 g (4.59 oz)
Display Type Super AMOLED capacitive touchscreen, 16M colors
Size 1080 x 1920 pixels, 5.0 inches (~441 ppi pixel density)
Multitouch Yes
Protection Corning Gorilla Glass 3
- TouchWiz UI
Sound Alert types Vibration; MP3, WAV ringtones
Loudspeaker Yes
3.5mm jack Yes
Memory Card slot microSD, up to 64 GB
Internal 16/32/64 GB storage, 2 GB RAM
Data GPRS Yes
EDGE Yes
Speed HSDPA, 42.2 Mbps; HSUPA, 5.76 Mbps; LTE, Cat3, 50 Mbps UL, 100 Mbps DL
WLAN Wi-Fi 802.11 a/b/g/n/ac, dual-band, DLNA, Wi-Fi Direct, Wi-Fi hotspot
Bluetooth Yes, v4.0 with A2DP, EDR, LE
NFC Yes
Infrared port Yes
USB Yes, microUSB v2.0 (MHL 2), USB On-the-go, USB Host
Camera Primary 13 MP, 4128 x 3096 pixels, autofocus, LED flash, check quality
Features Dual Shot, Simultaneous HD video and image recording, geo-tagging, touch focus, face and smile detection, image stabilization, HDR
Video Yes, 1080p@30fps, dual-video rec., check quality
Secondary Yes, 2 MP,1080p@30fps, dual video call
Features OS Android OS, v4.2.2 (Jelly Bean)
Chipset Qualcomm APQ8064T Snapdragon 600
CPU Quad-core 1.9 GHz Krait 300
GPU Adreno 320
Sensors Accelerometer, gyro, proximity, compass, barometer, temperature, humidity, gesture
Messaging SMS(threaded view), MMS, Email, Push Mail, IM, RSS
Browser HTML5, Adobe Flash
Radio No
 
Back
Top Bottom