samsolo the great
JF-Expert Member
- Jul 9, 2021
- 692
- 1,030
Hata mimi binafsi nashangazwa na tabia hii ya kuingia na mabango ya kusifia viongozi wa kisiasa ambayo imeota mizizi hasa kwenye timu niipendayo ya yanga. Kukiwa na mechi mara asante Rais kwa kufanya hiki au kile! Kuna vitu vizuri vingi amefanya Rais na serikali yake na watu wameviona au wanaviona kuna sababu gani ya msingi watu mnaanza kuingia na mabango uwanjani ambako kila mtu huko ana itikadi yake. Je akina Rungwe mzee wa ubwabwa wafuasi wao wakianza kuingia na mabango ya kuhusu ubwabwa Wallace Karia na wenzio mtavumilia?