nakushukuru kwa ushauri na pendekezo lako. Nakubaliana nawekuhusu suala la Academy za Soka zenye ubora wa Kimataifa. Binafsi napendekeza academy hizo ziwe za kikanda. Kanda moja iwe ya mikoa mitatu. Naamini hapo tutafika.
Asante kwa Maoni yako.na maswali uliyouliza. Kinadharia inaweza kuonekana hivyo. labda katika kuboresha hilo pendekezo, tuunde kanda za mikoa mitatu mitatukutafuta wachezaji wa timu ya taifa na kila kanda itupatie wachezaji wasiopungua 22 ambao wanaamini wanastahili kuchezea timu ya taifa. Hili...
Wakuu,
Napendekeza tubadilishe mfumo unaotumiwa na Kocha wa Taifa Stars kupata wachezaji wa timu yetu ya taifa ya mpira wa miguu.
Mfumo ninaopendekeza ni huu
Kila mkoa upewe jukumu la kutoa idadi ya wachezaji watatu bora zaidi kwa namba watakayokuwa wamepewa.
Kwa mfanoi mkoa wa Lindi unaweza...
Wakuu,
Katika juhudi cha kujenga utamaduni wa kuwekeza katika vitabu na kuvisoma katika ngazi ya familia, naomba utusaidie kujua vitabu visivyozidi vitano vilivyoandikwa na Watanzania kwa lugha ya Kiswahili ambavyo unaamini kuwa kama kila familia ikivisoma, basi familia zetu zitafaidika na...
Ni muhimu CCM na Makada wake watambue kuwa mapato ya Kampuni moja tu ya Marekani ya amazon.com kwa mwaka 2011 ni USD 48.08 bn. Hii ni zaidi ya mara mbili ya GDP yetu kwa mwaka 2011.
Bila kuwekeza ipasanyo katika Hisabati tusitegemee mabadiliko yoyote ya maana kwa vijana wetu. Pia tunahitaji kuwa na Mkakati wa Kitaifa kwa kila somo kuanzia Msingi mpaka Sekondari.
Waziri Mulugo anatakiwa alieleze taifa ni kiasi gani cha fedha kwa kila mwanafunzi wa sekondari kilipelekwa shuleni kwa mwaka wa fedha uliopita. Hizi ni ngonjera. Nendeni katika hizo shule ndiyo mtajua hali halisi ikoje.
Asante kwa maoni yako, Kitalo.
Ni muhimu sana kama taifa , kama familia na mtu mmoja mmoja kuwekeza katika vitabu na kutekeleza kwa vitendo yale tuyapatayo toka katika vitabu husika.
Ni lazima usome. Acha kukubali kushindwa kirahisi katika kutafuta ujuzi na maarifa. Soma sana vitabu na utaona matunda yake ukiwa chuoni na ukiwa umemaliza chuo. Pindi umalizapo chuo shule ndiyo inaanza rasmi.
Wakuu
Napendekeza kipindi cha mtu kuwa rais wa nchi yetu kiwe kimoja tu cha miaka mitano tu. Pendekezo hili linatokana na uzoefu tulioupata katika nchi yetu. Uzoefu unaonyesha kuwa nchi yetu haifaidiki na rais mmoja kutuongoza kwa awamu mbili. Hali halisi ya utendaji wa Marais wetu katika...
Wakuu,
Katika kuhakikisha kuwa tunaienzi Lugha yetu ya Kiswahili na kuieneza dunia nzima, nashauri tuanzishe kama taifa televisheni maalum ya Kiswahili kwa ajili ya kutimiza ndoto hiyo. Televisheni hiyo inapendekezwa iitwe MWALIMU NYERERE KISWAHILI TELEVISION.
Moja ya lengo lake kuu liwe ni...
Wakuu,
Napenda kuwajulisha kuwa Mtanzania wenzetu ametoa kitabu kizuri sana kiitwacho SUPU YA ELIMU.
Kitabu hiki ni Muongozo, Dira na Barabara anayotakiwa kupita mtu ili aweze kupata mafanikio makubwa katika kuielekea Elimu na kuhakikisha kuwa kazi yake ya kusoma kwa ngazi zote za elimu...
Nafikiri soko la walimu hapa si hoja ya msingi. Suala la msingi zaidi ni kuwa kama taifa tunaongeza idadi ya vijana ambao watajiunga na vyuo vyetu vikuu wakiwa na background ya sayansi. Pia vyuo vyetu vitapata fursa ya kupata vijana ambao vichwa vyao vinachemka vilivyo. Asikudanganye mtu nguvu...
King,
Umuhimu upo na ni mkubwa. jaribu kukaa chini na kufikiri kwa undani naamini utakubaliana na uamuzi wa wizara husika kuongeza hizo combinations. Pia nafikiri itakuwa muhimu kwenda mbele zaidi na kuanzisha shule maalum kwa kila combination hasa zenye angalau masomo mawili ya sayansi...
Asante kwa taarifa hii Kimbori. Inatia moyo kuona kuwa hatimaye Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wameliafiki wazo la kuongeza Combinations mpya hasa zilizo na Masomo ya Fizikia, Uchumi, Hisabati, Kemia na Biolojia. Natumaini EPM na ECM nazo zitakuwemo bila kusahau EBM na PBM.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.