Zaharani - Maisha na mashairi

NGAYANIMO

Member
Joined
Feb 17, 2026
Posts
43
Reaction score
60
ZAHARANI - MAISHA NA MASHAIRI.

Verse..1.

Hizi mbio sio za Baiskeri , Haiwezi kabiri Kasi/
Tahadhari usije Ukaferi , Mbuzi Amzindi Farasi/
Usiwambie Watu watakucheka/
😄 🤣 "hahaha "
Wengi wameishia Sakafuni/

Chunga usipige mweleka , Usafi wa Nafsi sio Sabuni/
Unapozungumzia Hip hop , Lazima Utaniorodhesha/
Me ni postive Hip hop, Na Hii inajionyesha/
Ushairi kwangu ni Dhati, Sanaa sifanyii njaa/
Nadumu na Hizi harakati, Kila siku ,Kila saa/
Haimanishi Ukimya siandiki, Mwandishi Haishiwi Hati/
Walipo wanapatwa kwikwi, wanapagawa na Hi Dhati/
Makusudi najaza Hofu, hawaamini Mpaka wanajamba/
Wanapapaza ka vipofu hawaoni pakushika na Vaba/
Ubora sio wa kichina , Usioshe Fikra zako/
Sio tu ilimradi eti Vina, Wazi Me sio Mwenzako/
Utapotea usifuate nyayo , Yingine hasifatiki/
Ni Bora Tupige Miayo , hata ukibebwa haufiki...

Chorus:
Ni maisha na Mashairi , Mtaani ndivyo Navyoishi/
Nitaacha vipi kuwa mahiri , Na hizi " Mic" hazinitishi/
Ni maisha na Mashairi , Mtaani ndivyo Navyoishi/
Nitaacha vipi kuwa mahiri , Na hizi " Mic" hazinitishi..!

Verse..2

Wanashtuka Huu Muziki , Akili zinawaruka/
Wanaulizana itakuwa Vipi? , Na Mara Wameshaanza Kuanguka/
Wanaona Haya , wanajificha Nafsi zinawasuta/
Wanabaki kufutia Picha, Ninavyo Penya kwenye Ufa/
Najua wanakuna Vichwa, Huku Wanaona/
Ha.!!
Na Sikio alizindi kichwa, Vinywa Wazi wanashangaa/
Yes.!
Ng'ombe Hazeeki Maini , Na Maana Naitwa Run/
Ni ngumu Kunishusha Chini , Sio Rahisi kaa Ulidhani/
Hahitaji Kuumiza Fikra , Ukijua level Ya kweli/
Ni Heri Utulize Fikra , Utaumbuka kwa Hizi Ng'eri/
Jisitiri Usipate Aibu , Basi utadhalilika/
Unamudu Ngono Unaharibu , ukiambiwa unakadhilika/
Level yako ni Ya kitaifa , Bado ukizi Viwango/
Una ng'ang'ana Kimataifa , Ni Bure Tu Ubebe Bango/
Usijipigie Debe kiti , wazi Najua unajua /
Basi Pisha nikizi Beat , We ulokaa Unazingua..

Chorus:

"Ni maisha na Mashairi , Mtaani ndivyo Navyoishi/
Nitaacha vipi kuwa mahiri , Na hizi " Mic" hazinitishi/
Ni maisha na Mashairi , Mtaani ndivyo Navyoishi/
Nitaacha vipi kuwa mahiri , Na hizi " Mic" hazinitishi..!

Verse..3

Kwanza Nakuona Fara , Hip hop Wapi Bila Nguzo/
Huna unachojua , harafu mbishi Kwetu Gumzo/
Mpaka watoto Wadogo , wanajua hujui kitu/
Bado Tuna ng'ang'ana , Upo Tu kila Siku/
Dukani Kwenyewe Hauzi , Harafu Bado Makuzi /
Najua unauza Sura , Ulingoni Wewe haina Ujunzi/
Unashusha Hadhi ya Hip hop , Bado una dhalilisha/
Auendi bila kubebwa , Poyoyo Unasikitisha/
Hip hop imejaa uchafu , Tungo hazina Umahiri/
Ufanisi wenyewe umekopa / Harafu huna Ushairi/
Unataka hadhi ya umarenga , wakati Yupo Zaharani/
Ninajua unajua , Sisemi ni Jinsi Gani/
Weka Mic kado , huna hadhi yakuwa kinara /
Hata upige kelele , Bora u change Tu Biashara/
Hip hop sio Bongo fleva , utavaaje Suti na Dala/
Huna unachojua , Badirisha kila idara..

Ukwaju wa kitambo
0767 542 202
 
Verse ..3 ( zaharani)

Yo! Watu wanaathirika lakini Bado hawajali/
vipi? Mnakosa fikira za kuweza kufikiria mbali/
watu wanapata shida sio siri Bado ni hatari/
mifano mingi tumeona vipi kuhusu tahadhari/
kila siku watu wanaonya ni wagapi wanajali/
nusura hakuna kupona mapema mjihadhari/
maambukizi juu ya sindano watumiaji mjihadhari/
ukimwi nao umeshika pande zote hatari/
vipi sindano mnadunga hamjui kwamba ni hatari/
Tena moja inazunguka masikani tena bila ya tahadhari/
nyani ndio kwamba hamjari /
au ndio basi ufahari/
Zaharani nini nitasema na hakuna anayejali/
wengi wamekufa masikani kisa wamekosa Gari/
wamekufa KWA kujidunga na madawa ambayo ni hatari/
Ni vipi hauchi starehe Gani hatari/
utumiaji Bado unazindi ifanye nini serikali/
na kuacha watu wakaidi na jela hawajali/
labda ingetekwa sekta nadhani ingekuwa afadhali/
watumiaji wa madawa serikali ingewapa hifadhi/
Pindi wanapoacha madawa/
wapewe matuzo safi/
Kazi na Elimu ya kutosha/
Kuhusu utaraji, nadhani wengi wangeacha/
hata wale wasiotaraji .. ..

( msanii zaharani kwenye Wimbo wa Crazzy Buffa unaitwa " Muelimishaji"

Ukwaju wa kitambo
0767 542 202..

Iweke hii ngoma

Zaharani mzee wa vina, aliteleza vizuri sana kwenye ile ngoma ya ab skills
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…