Yaliyonikuta Leo


Itabidi nianze kuangalia ze comedi sasa , sikuwa nimeiona!
 
Pole mie nilikutana na maswahiba kama hayo yako Pale Magomeni Karibu na Nyumbani Kwa Marehemu Sheikh Yahaya,bahati kuna mdada mmoja anamjua huyu mzee alikuwa amevaa kanzu,akajigongesha Akawa analalamika mgu wake wenye chuma nimeivunja tena wakati sikumgonga na ata speed ya gari langu ilikuwa kama 20 KMm kwa saa.

Yule dada akinipa signal kuwa nnatapeliwa,so nilimwambia ngoja nipaki gari vizuri upande twende hospital then nikaweka speed nikatokomea.

Pole sana
 
Pole sana kwa mkasa huo, maisha yamekuwa magumu sana ndio maana watu wanatafuta namna ya kuishi..
 
Sipati picha ungeamua kukomaa hadi hospitali halafu ijulikane hajaumia. Ila jamani kariakoo, kweli twende kwa uangalifu, kuna watu ndiyo kazi yao hiyo, pole sana Nata
 
ulimuuliza nini baada ya kumkuta? au ulikaa kimya kama ni hivyo nyie ndio mnaofuga maradhi.
 
jamani sijui hali hii tutaendelea nayo mpaka lini. Unaweza ukamwona kuwa alikuwa jeuri, lakini ukitafakari, ni heri afanye hivyo ili aine siku pamoja na wenzake ingawa inaumiza wasiohusika. Mungu atusaidie
 
ulimuuliza nini baada ya kumkuta? au ulikaa kimya kama ni hivyo nyie ndio mnaofuga maradhi.

Ndugu yangu we, nilikaa kimya kama nimemwagiwa maji na kumpita kama cjawahi muona
 
Siku nyingine ikitokea hivyo usikubali kumpa chochote paki gari lako pembeni ita Trafiki mweleze kilichotokea, kama kuna kesi ya kujibu mahakama ndiyo nitakayofafanua kosa lako na ikitoea kuna haja ya kumpeleka Hospitalini wewe kama mwenye gari huwajibiki kumtibia majeruhi, vinginevyo hiyo insurance yako itakuwa haina kazi kwenye gari.

Hao madapeli dawa yao ni hiyo maana ukilegea hapa mjini utaonewa kila kukicha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…