Watu wa Dar bhana....

Tatizo hawaelewi kama unawasalimia kutokana na lafudhi yako ngumu ya mikoani huko, wanaamua tu kukupotezea.......
 
Mimi mgeni huku dsm, ukiachana na tabia ya wakazi wa huku kichukulia chips kavu kama mlo wa siku, bonanza kuchezwa mpaka na mabinti, madela kwa wingi!!

Kuna hii tabia ya kutokuitikia salamu. Inanikera, unakutana na mmama umri umeenda, unamwamkia, anakwambia kashike ya kwako, kamsalimie mama ako, unaamua kukaa kimya.

Juzi kuna mmama kanikuta barazani home, nikamwangalia tu, akawa ananangalia sana, nikajistukia nikamwambia, zas'aiz, akanambia kuwa na adabu!!

Mara watake salamu, mara hawataki!! Hadi mtu unashindwa ufanye nini, kupita kwa watu unaona balaa!!

Wenyeji wa huku tupeni mwongozo.....
heri waislam wao salam yao ni asalamaleyko kwishne hiyo.

afu shkamoo huwa ni salam nzito sana na wengi kabla ya kuitoa huwa wanajifkiria sana, sijui ni kwanini.

mtu nae akipewa hiyo anajiuliza, inakuwaje apewe shkamoo mpaka na wazee?

ko unakuta wengine wanaipenda wengine hawaitaki.
 
Hadi leo sijaona umuhimu wa salamu asee, naonaga kama shobo tu i wish kila mtu angefuata mambo yake tusiongeleshane hadi mtu awe na shida ndo amuongeleshe mwenzake.
 
Back
Top Bottom