Anapasawa kukumbukwa kwa mengi tu. Ila nadhani siasa haikuwa anga zake lakini kwa taaluma yake ni balaa. Hapo namvulia kofia maana ile Plant Physiology kwa kweli akikuchapa shule hapo utamwaminia mambo magumu lakini anavyoyafundisha kilaini huwezi amini. Ukimstua usingizini ukamwambie akushushie Kreb's Cycle (kwa wale scientists specifically biologists nadhani tunaelewana mangwini mtanisamehe) ni kama sala ya baba yetu. Nakumbuka hata alipokwenda kugombea ubunge na akashinda aliahidi kuendelea kufundisha pale Botany Department mlimani maana alikuwa the only Prof. of Plant physiology. Lakini naona huko kwenye siasa utamu ulizidi hakuonekana tena. Labda sasa ndio anatekeleza ile ahadi yake ya kupiga taalum Mlimani ndio maana haonekani.