Dhambi ni lazima ikemewe,
Dhambi ikiachwa humgusa kila mtu,
Ubaya wa dhambi,
ni tabia yake ya kupatiliza,
huwaingiza waliokuwemo,
na wasio kuwemo.
Dhambi ya mtu mmoja,
ina uwezo wa kuangamiza taifa zima,
chuki ya mtu mmoja,
ina uwezo wa kuangamiza taifa zima,
Hasira ya mtu mmo in uwezo wa,
kuleta chuki taifa zima.
Ona dhabi ya rushwa,
inavyotufanya kwa nguvu kila siku,
tunadharirishwa katika nchi yetu.
Ona dhambi ya uongo ituangamizavyo,
uongo ni mtaji wa utajiri,
uongo ni dira ya taifa,
uongo una abudiwa na viongozi wetu?
ona dhambi ya wizi itutuavyo umasikini,
kuiba ni ujanja,
kuiba ni kuchngamka,
maaskofu wanaiba,
masheikh wanaiba,
rais anaiba,
mawaziri wanaiba,
Wengi wanatamani kuiba ili waukate.
ona dhambi ya uchoyo,
Magari 20 ya nini,
wakati barbara zenyewe hakuna?
mtu ana vimada 100,
lakini bado anatongoza wake za watu?
Unaiba pesa,
huwekezi popote,
unazificha Ulaya,
sasa uliiba za nini??
utazitumia lini?
Unamkataba na Mungu?
Dhambi,
inavyotafuna maendeleo yetu.
Ni lazima tukemee dhambi,
tena tukemee,
kwa nguvu na akili zetu zote,
au tuwe tayari kumwaga damu,
za wakosefu na wema pia.
Dhambi mkataba wake unasainiwa kwa damu.