Meli kubwa zaidi duniani inayoitwa "Icon Of The Seas" iko karibu kuanza safari Januari 2024.
Meli hiyo iliyotengenezwa nchini Finland na kampuni ya kutengeneza meli iitwayo Royal Caribbean International itabeba abiria 5610 na wafanyakazi 2350.
Icon Of The Seas ni kubwa mara 5 na nzito kuliko Titanic yenye uzito wa tani 250,800 huku Titanic ikiwa na uzito wa tani 50,210.
Maelfu ya watu wamekata tikiti ili kuwa miongoni mwa abiria wake wa kwanza.