DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
MGOMBEA nafasi ya udiwani wa Kata ya Mbweni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulkadir Mgheni, ameendelea na kampeni zake leo akishirikiana na vigogo wa chama hicho wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mstaafu Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, na Mjumbe wa Kamati ya Ushindi Mkoa, Shyrose Bhanji.
Viongozi hao kwa pamoja wameungana na Viongozi, wanachama wengine wa ngazi za Wilaya, Tawi na Shina kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba, maarufu kama 'chocho kwa chocho,' ili kuhakikisha kura za CCM zinapatikana kwa nafasi zote - udiwani, ubunge na urais - kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.
Viongozi hao kwa pamoja wameungana na Viongozi, wanachama wengine wa ngazi za Wilaya, Tawi na Shina kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba, maarufu kama 'chocho kwa chocho,' ili kuhakikisha kura za CCM zinapatikana kwa nafasi zote - udiwani, ubunge na urais - kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.
Your browser is not able to display this video.