Verkys vs Luambo. Nani zaidi?

Ziroseventytwo

Platinum Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
9,397
Reaction score
17,784
Nimesikiliza miziki/nyimbo zao nikagundua hawa jamaa walikuwa wakali sana.

Franco Luambo Makiadi akiwa na TP OK JAZZ alirekodi miziki mingi iliyotamba si Africa tu bali mpaka bara ulaya. Alifanikiwa kupiga muziki akiwashirikisha baadi ya wanamuziki nguli (si wasanii) wakiwemo Tabu Ley roucherou, Nyiboma Mwandido Sam Mangwana na wengine wengi. Anatajwa kuwa ndio mwanamuziki bora kabisa kutoke nchini congo zamani zaire. Moja ya vibao vyake vilivyompatia umaarufu ni pamoja na Mario.

Kyambomana Matete Yazelambongo maarufu Verkys yeye alikuwa anamiliki bendi zaidi ya 3. mojawapo ni orchestra veve. Hii bendi nayo ilitamba miaka ile ya mwisho ya 70. hawa jamaa walikuwa ni nourma linapokuja swala la alla za upepo. Verkys na veve walitamba na vibao vyao vilivyotikisa na vinavyoendelea kutikisa. Mikolo mileki mingi, Baluti, ndowe na vingine kibao.

Kwangu mimi verkys ndio alikuwa mkali kuliko Lwambo Makiadi.

Tusemezane.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…