Timu ikiwa inapata matokeo kamwe kwa mashabiki mandazi hawawezi kuona mapungufu yao ndivyo ilivyokuwa kwa Simba ya Mo na yanga ya Manji, tofauti ya Mo na Manji ni kuwa Manji alikuwa na love na football na pia na yanga aliweka pesa yeyote muda wowote bila kupepesa macho.
Hakuikopesha club Kama Mo, halafu anagomea mkataba wa Azam wa bilion 41 kwa miaka 10 na Azam na anaenda kusaini mkataba wa milion 400 huu si ukichaa bali ni siasa ya mpira.
Ule utapeli wake tuliowaambia mashabiki wa Simba kwamba jamaa Ni tapeli ndio utajionyesha Sasa
Maana kenge uwa hasikii mpaka damu itoke masikioni.
Sasa Mambo yamebadilika timu limeanza kuchezea za uso je Kama Simba ilitengeneza faida champions ligue pesa zilienda wapi mpaka wauze wachezaji ambao ni key players?
Billion 20 ziko wapi mkafanye usajili dilisha dogo? Yaani tulivyowaambia Mo ni tapeli mliziba pamba masikio.
Hii aibu pesa zilizotengezwa champions ligue ilitakiwa kuwapa mikataba key players.
Lakini akauza Tena wachezaji halafu Sasa hivi anajiuzulu baada ya kuona timu Ina wazee kibao.
Mo anatakiwa kulipa gharama za haya matokeo Ni yake msimwangushie zigo kocha Wala wachezaji.
Wachezaji ni wazee na wengine Ni watoto wa shule .
Mambo mengi umeandika kwa uelewa mdogo sana.
Mpaka hapo sijaona mapungufu ya Simba uliyoyabaini na kuyaorodhesha.
Kuuza wachezaji Ni biashara na Simba imefikia level za kufanya biashara ya wachezaji.Hili Ni la kupongeza.
Simba haikuwa na uwezo wa kumbakisha mtu km Miquisone.Simba haina uwezo wa kiuchumi wa kumlipa Miquisone milioni 80.Pia simba wangeacha vipi dau nono km lile?
Chama umri ulishaenda , hilo dau ungekuja kulipata wapi. pia inasemwa alilazimisha kuuzwa japo utanambia alikuwa na mkataba.
Kumbuka pia Kwamba bado vilabu vya ukanda wa Afrika Mashariki,kati na kusini sisi Ni walishaji wa Afrika Kaskazini. Tunatengeneza wanaonekana wanachukukiwa.sababu hatuna misuli ya kifedha.
Kumbuka shabiki anachohitaji Ni furaha tu hakuna kingine anachonufaika nacho.Na hakuna timu isiyofanya vibaya au kupoteza mechi.
MAPUNGUFU labda ungechambua kwamba hela iliyopatikana ilitumikaje, na km walinunuliwa wachezaji Ni wachezaji viwango vya juu? Wanakidhi level za Simba kimataifa?
NB:
Kifupi huujui mpira ila nawe ni shabiki kitumbua.
Sent from my Infinix X680 using
JamiiForums mobile app