Ushauri wangu kwa CHADEMA

Wakuu nawasalim.

CHADEMA,nawaomba mtambue kwamba wananchi wamechoka na siasa za majukwaani,masikio hayapo tayari tena kusikia juu ya Operesheni Sangara wala M4C zisizo na matokeo ya moja kwa moja kwa Mtanzania.

Kama chama,badala ya kutumia millions of money majukaani,hebu tujaribu kufanya haya..

1. Tufanye harambee nchi nzima tuchangishe fedha tununue madawa na tusambaze mahospitalini.
2. Tutumie muda mwingi kujishughulisha na mambo ya maendeleo kama kuwanunulia na kuwasambazia wakulima mbolea
3. Tushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kijamii kama usafi wa miji na majiji.
4. Tuhakikishe tunapata fedha na tunaboresha zahanati na ward za wajawazito kwa kuongeza vifaa na vitanda.
5. Kuhakikisha vitabu vya kiada na ziada vinapatikana kwenye mashule
6. Wakati wanachangisha waalimu ili kujenga maabara sisi tuje kivingine na tuhakikishe zinapatikana kwa msaada wetu

Tuache kuwachamba ccm bila vitendo..tutende ..tuwaoneshe wananchi kuwajali na hakika watatuelewa...
kama una ushauri zaidi karibu...

ALUTA CONTINUA
 
Ushaifu wa upinzani ndiyo sababu cha msing cdm iache ubinafsi ili kiwenze kuaminiwa na si mgogoro ya kugombea vyeo na mambo mengine kama utawala usio na kikomo nami ntashawishika kuwaamini na raisa wengi wenye mtizamo kama wangu

Hebu rudia kusoma ulichoandika uone kama kinaendana na mada, nyankundo!
 
ngoja waje wenye chama chao,but jiandae kuitwa gamba au msaliti au sio mwana Chadema
ushauri mzuri na kila la kheri
 
Ushaifu wa upinzani ndiyo sababu cha msing cdm iache ubinafsi ili kiwenze kuaminiwa na si mgogoro ya kugombea vyeo na mambo mengine kama utawala usio na kikomo nami ntashawishika kuwaamini na raisa wengi wenye mtizamo kama wangu

Wewe ndugu yangu yanatoka kikiyu au yatoka wipi
 
Ford ranges iko poa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…