Uru wapata Kituo cha Afya cha kisasa

Ndagullachrles

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2023
Posts
205
Reaction score
215
WANANCHI wa kata ya Uru Kusini wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro wameondokana na adha upatikanaji wa hudumu za afya baada ya serikali kujenga kituo cha afya ha kisasa

Kukamilika kwa kituo hicho ni jitihada za Mbunge wa Jimbo hilo, Prof. Patrick Ndakidemi pamoja na Diwani wa kata hiyo kwa jinsi walivopambana kuwaletea kituo cha Afya.

Andrew Lyimo alisema kuwa, awali walikuwa wakilazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya na kuishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hasani kwa jinsi ambapo wanasogeza huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi.

"Tunampongeza sana Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hasani pamoja na Mbunge wetu Prof. Patrick Ndakidemi na Diwani kwa jinsi ambavyo wanajitolea kututumikia sisi wananchi wa kata ya Uru kusini na kutuletea miradi mbalimbali ya maendeleo" Alisema Lyimo.

Alisema kuwa, kituo hicho cha Afya pia kinahudumia wananchi wa kata za jirani na kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma
 
Mama Samia Suluhu HOYEEEE....!
[emoji1787]
 
Hongera serikali ya chama cha mapinduzi
 
Mimi niko hapa URU hebu tueleze ni eneo gani hasa na utuwekee picha. Si ajabu ni cha kawaida sio cha kisasa!
 
Subiri uone kenge wa chadema watakavyopinga
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…