tamu 3
Member
- Dec 11, 2024
- 88
- 216
UPENDO UDUMISHWENI
Beti nimetunga, sikio ziwakune,
Kwa hiyari mmepanga, muoane muoane,
Kibwebwe mmejifunga, pamoja mshikamane,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
2.
Ndoa ni uvumilivu, hili mwapaswa tambua,
Mjue mbichi na mbivu, vinaweza kutokea,
Mwenye wivu na anaiharibu ndoa,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
3.
Mkawe mfano bora, kwenu hawo majirani,
Waige zenu ishara, zitumie maishani,
Kitabia mking'ara, wao kwenu taigeni,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
4.
Watoto kibahatika, muwafunze yalo mema,
Waombeeni baraka, waje wawe na heshima,
Wote shuleni peleka, wakajifunze kusoma,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
5.
Kauli nzuri tumia, mke kwa wako mmeo,
Sauti ya kupepea, iwe kwako mkazio,
Kiburi takuumbua, utaishia kilio,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
6.
Mume nawe vile vile, mke ni faraja yako,
Uache mambo ya kale, kupiga kwa teke lako,
Mpe kanga na mchele, huko ndiko apendako,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
7.
Msilete chokochoko, mawifi nawaambia,
Silete mvurugiko, ndoa kuitia doa,
Yamekushinda ya kwako, ya wifi unadandia,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
8.
Mwovu atapata hamu, wanandoa kiachana,
Ndoa yenu itadumu, pamoja kishikamana,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
9.
Mwenza wa ndani mepata, wa nje wa kazi gani,
Huko maradhi tapata, majuto hayo ya nini,
Ujumbe huu fuata, mshinde ya duniani,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
10.
Shime metoa nasaha, mwapaswa kuzingatia,
Ombaneni msamaha, kati yenu kikosea,
Ndoa iwe ya furaha, mkono nawapungia,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
Denny Jeremias kitumbika
Mtunzi wa mashairi na ngano za Kiafrika
Mufindi Tanzania 13.4.2016
Beti nimetunga, sikio ziwakune,
Kwa hiyari mmepanga, muoane muoane,
Kibwebwe mmejifunga, pamoja mshikamane,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
2.
Ndoa ni uvumilivu, hili mwapaswa tambua,
Mjue mbichi na mbivu, vinaweza kutokea,
Mwenye wivu na anaiharibu ndoa,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
3.
Mkawe mfano bora, kwenu hawo majirani,
Waige zenu ishara, zitumie maishani,
Kitabia mking'ara, wao kwenu taigeni,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
4.
Watoto kibahatika, muwafunze yalo mema,
Waombeeni baraka, waje wawe na heshima,
Wote shuleni peleka, wakajifunze kusoma,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
5.
Kauli nzuri tumia, mke kwa wako mmeo,
Sauti ya kupepea, iwe kwako mkazio,
Kiburi takuumbua, utaishia kilio,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
6.
Mume nawe vile vile, mke ni faraja yako,
Uache mambo ya kale, kupiga kwa teke lako,
Mpe kanga na mchele, huko ndiko apendako,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
7.
Msilete chokochoko, mawifi nawaambia,
Silete mvurugiko, ndoa kuitia doa,
Yamekushinda ya kwako, ya wifi unadandia,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
8.
Mwovu atapata hamu, wanandoa kiachana,
Ndoa yenu itadumu, pamoja kishikamana,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
9.
Mwenza wa ndani mepata, wa nje wa kazi gani,
Huko maradhi tapata, majuto hayo ya nini,
Ujumbe huu fuata, mshinde ya duniani,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
10.
Shime metoa nasaha, mwapaswa kuzingatia,
Ombaneni msamaha, kati yenu kikosea,
Ndoa iwe ya furaha, mkono nawapungia,
Upendo udumishweni, i ngao ya familia.
Denny Jeremias kitumbika
Mtunzi wa mashairi na ngano za Kiafrika
Mufindi Tanzania 13.4.2016