Ukweli kuhusu mieleka/wrestling, mchezo au maigizo

Nilitaka kusema, wengi wenu hapa inaonekana mmezaliwa hivi karibuni.
Kwa wale wahenga nadhani mnakumbuka enzi za mieleka hapa Tanzani.
Kwa sasa mieleka imeshindwa kuchezwa kwakuwa Bodi ya mieleka imeshindwa kutimiza masharti ya mieleka kama kuwa na jukwaa maalum, ambalo ni ghali sana na jukwaa la mieleka moja linafikia thamani ya Tsh, zaidi ya Bilioni moja.
Wakati ule wa mieleka akina Power Bernado. Power Mwanza. Power Chaka. Power Vurumroma, Power Mabura walikuwa wanacheza Mieleka ya Ukweli hapa Tanzania.
Viti vilikuwa vinatumika lakini sio kila kiti, ni viti maalum vya kupigania. Ukiangalia WWE utaona viti vyao wanavyo pigania vinafanana na sio kila kiti.
Katika mapambano ya Mieleka kuna mapambano ya kutumia silaha maalum, zinapitishwa kutumika kama Meza Viti, Rada yaani ngazi nk, na kuna aina ya upigaji wake, hata ile nyundo anayetumia mpinzani wa Underteker (nimemsahau jina) ina aina yake ya utumiaji, ndio maana huioni ikitumika kumtwanga nayo mtu kichwani au kwenye uti wa mgongo.
Kuna mapambano hayatakiwi kutumia silaha, na kuna mapambano hayatakiwi kuingiliwa, wachezaji wanacheza ndani ya wavu wa chuma.
Maana kuna wakati fulani ilikuwa mkicheza pambano na kama kuna mtu kaingilia kumpiga mchezaji X, basi Mchezaji Y anapewa ushindi.
Lakini wajanja wakaingiza hila ya kwamba adui wa mchezaji X anaingilia pambano na kumpiga mchezaji Y ili mchezaji X anyang'anywe ushindi.
Hivyo WWE ikaaamua kuwafunika wachezaji kwenye wavu wa chuma kama wanataka mshindi apatikane bila kusaidiwa na mchezaji mwingine.

MAIGIZO KATIKA MIELEKA.
Kuna kuigiza ndani ya mieleka lakini maigizo yale yanakuwa wakati wa kupanga pambano fulani ili kuvutia mashabiki, kwa mfano.
John Cena anataka kucheza na Rand Orton pambano la ukweli.
Ili kunogesha pambano John Cena ataandaliwa pambano na Rey Masterio, pambalo ambalo linakuwa la ushindani kama kawaida na mshindi atachukua zawadi yaani fedha kama kawaida.
Katikati ya pambano Cena bila kijua, Rand Orton ataingilia Pambano kumpiga John Cena na kumsaidia Ray kushinda pambano hilo, hivyo kuamsha hasira kwa Cena kutaka kulipa kisasi kwa Rand Orton, hapo sasa Pambano halisi linaandaliwa kati ya Cena na Orton.
Mfano hakisi ni pale WWE ilipotaka kuwapambanisha wacheaji ndugu Mart na Jeff hard.
Jeff alikuwa anagoma kucheza na ndugu yake lakini pesa nyingi iliyoandaliwa na WWE ambayo ilimvutia Mart na kutaka kumlazimisha Jeff akubali kupigana naye ili wavute ule mkwanja ama yeye Mart au ndugu yake Jeff.
Hivyo WWE wakafanya Njama kwa kumshirikisha Mart, wakaanda pambano kati ya Jeff na mchezaji mwingine, Jeff akiwa hana habari, katikati ya mchezo ambao Jeff alikalibia kushinda Mart akaingilia kati, akampiga Jeff na kumtolea maneno mengi ya kashfa hadi Jeff akakasirika na kukubali kucheza na kaka yake Mart hard, na wakacheza pambano ambalo liliingiza pesa nyingi kwakuwa liliandaliwa kwa jinsi hiyo, Mart mbaye ni yule kama anachechemea alishinda pambano.
Mieleka ni mchezo halisi ila unambwebwe wakati fulani ili kuhamasisha washabiki na kuingiza pesa nyingi

UHALISIA
Mzungu au mtu mwingine hawezi kupoteza muda wa kwenda kupoteza pesa yake kuangalia utapeli wa michezo wa watu mahali fulani.
Michezo ni kitu halisi, kama Komedi inaandikwa kabisa hii ni Komedi. Kama Bongo Muvi itawajulisha watazamaji wake kuwa hii ni Bongo Muvi.
Na wakati ule wa mieleka ya hapa Tanzania mimi nilikuwa naenda kuangalia na ilikuwa inacheza sawasawa na tunavyoona leo katika WWE, Viti vilitumika pia tena ni vilevile vya WWE, sema sasa hivi wenzetu wameboresha mambo mengi sana.
Kama kuna waliowahi kucheza mieleka, wapo humu JF wanaweza kututhibitishia zaidi ukweli huu.
Kukosolewa kunaruhusiwa.

Mkuu umeandika ukweli kabisa lakini kuna issue moja hujaijua.. hiyo issue ni kwamba wale jamaa hawapigani kabisa mfano orton vs cena pale hamna anayempiga mwenzie hata kidogo labda kwa bahati mbaya, zile ngumi mateke ni brush tu hazimfikii mtu zile zinarushwa kijanja sana . Chunguza hilo ingia you tube angalia hawa jamaa wame fool watu kibao kwa mda mrefu
 
. Unakuta mtu kama stone cold anaingia na tractor /caterpillar tena limejaa zege anaingia nalo mpaka ndani bila kuonekana, ile anafika anaanza kuharibu vitu jamaa ndo wanajifanya kushtuka na kumzuia inakuwa too late , hii ni joke ya mwaka.
babu ndio maana nikasema kuna script na wanapigana...damu we huielewi na si muangaliaji huwezi sema damu wanapewa kwenye package....watu wanapigan ana wanauima damu zinatoka live package ya damu wanaiweka wapi au wanaitoa ndio wajipake......elewa what is scripted na nini wanafanya...nadhani unaongea tu ilimradi hapa kwenye damu......hizo za tractor ndio script ambazo mshabiki huju nini kitakuja na hilo ndio kuufanya mchezo unoge zaidi mwisho wa siku kutakuwa na mpambano etc. ......huyo maywheater siju katika miaka 20 kaenda WWE mara ngapi..so usichukue kipande kimoja au cha siku moj aau wiki ukaanza kusema au kujudge ...huwezi mtumia meyweahte ambaye alienda kama mgeni kwa wiki hiyo...kina GIG SHOW wapo miak yote na wamekuwa na mapambano memgi mpaka wanaumia wanakaa pembeni....gigshow mwenyewe aliumia tena sababu ya Braun Strowman....na kuna mapambao mengi sana acha hizi ambazo unaona kam amasihara script zinasaidia wasiumizene...mipambani ipo mikali na wanaumizana sana vile vile...yani ukiielewa unaon kipi scripted sana kipi kinavuka ..mwisho wa siku wanapigana na wanaumia kama kawa......hizo za mayweather blahblah ni burudani tu........kwa watu

all in all we nimekuelewa kabisa hivo hivo vipande havibebi yote kuna mechi kubwa saa kila mwezi mabpao ndio unaona balaa la mechi....extreme rule, wrestlemania,, royal rumble, summerslam, money in the bank..etc..acha hizi za kila wiki monday raw and smackdown....
 
Mkuu umeandika ukweli kabisa lakini kuna issue moja hujaijua.. hiyo issue ni kwamba wale jamaa hawapigani kabisa mfano orton vs cena pale hamna anayempiga mwenzie hata kidogo labda kwa bahati mbaya, zile ngumi mateke ni brush tu hazimfikii mtu zile zinarushwa kijanja sana . Chunguza hilo ingia you tube angalia hawa jamaa wame fool watu kibao kwa mda mrefu
Asante ila kuna kitu hujakifahamu vizuri hapa katika usemi wako.
Ni hivi.
Katika mchezo wa mieleka kuna aina zake za upigaji.
Hairuhusiwi kupinga ngumi kama za kwenye ndondi.
Ngumi za kwe ndondi ni silaha kali na inabidi mchezaji avae Groves.
Kwenye mieleka inabidi umpige mpinzani wako kama unavyoona wanavyo piga akina Cena.
Zile sio ndondi ni mieleka ambayo inabidi umgonge mpinzani ili kumchosha tu halafu umbane chini asifurukute ndipo upate ushindi.
Angalia hata mateke yao, sio kama yale yanayotumika kwenye Kick-Boxing. Hayaruhuiwi katika mieleka.
Mieleka unatumia, labda niseme mapigo ya vifuti vya mkono au mguu, na sio viwiko au visigino vyake.
Hayo mapigo unayoyatake wewe hayaruhusiwi katika mieleka. Ni sheria za mieleka.
Hayo mapigo unayo yataka wewe yanatumika katika mchezo mwingine unaitwa " Free Boxing" nadhani unaujua ambao watu wanapigana kwa staili yoyote ile na kuangushana na kukabana, yaani tumia mbinu yoyote ile ilimradi ushinde.
Mchezo huo sio kick-boxing wala Wrestling bali unaitwa free- boxing, ambao wachezaji wake wengi wanachora tatoo mwilini mwao nadhani ushawahi kuuona katika tv.
Mieleka ina sheria zake za upigaji na ndio unaona kama wanatania kwakuwa hawapigi ngumi halisi au teke ni kwamba vinakatazwa kisheria, inamaana ungehama kutoka Wrestling na kuwa Free-boxing.
Wewe unataka wapigane kama free-boxing huo ni mchezo mwingine kaka.

Kuhusu kujirusha.
Kabla ya kuanza kucheza mieleka kuna hatua ambazo inabidi upitie yaani mazoezi ya awali.
Ila kwanza inabidi ujue kupata point katika mieleka hakutokani na kupiga, yaani ngumi au teke halikuongezei pointi.
Sasa kule wanako jifunza mieleka wanajifunza pia mbinu ya kumdanganya mpinzani wako kama vile unaelekea kupigwa au kuchoka.
Mchezaji anaweza kusukumwa kidogo tu akaanguka sana au kujirusha ili umwone kuwa amechoka au kalegea ili uingie kingi ya kujiaamini halafu ndio akushike vizuri.
Wakati mwingine unatathmini nguvu ya mpinzani wako, hivyo watazamaji wanaona kama ubapigwa sana na unaeleke kushindwa kumbe ni hadaa tu ya kumiliki pambano.
Mieleka sio ngumi ni kufanya juhudi za kumlegeza mpinzani wako hadi achoke ili umwangushe na umbane na ahesabiwe hati tatu bila kufurukuta ndipo unapopata pointi.
Wewe unachanganya michezo.
Ungekuwa unaniuliza kipengele kimoja kimoja ningekufafanulia vizuri zaidi.
Ila kaa ukijua mieleka sio ngumi wala mateke.
 
Asante ila kuna kitu hujakifahamu vizuri hapa katika usemi wako.
Ni hivi.
Katika mchezo wa mieleka kuna aina zake za upigaji.
Hairuhusiwi kupinga ngumi kama za kwenye ndondi.
Ngumi za kwe ndondi ni silaha kali na inabidi mchezaji avae Groves.
Kwenye mieleka inabidi umpige mpinzani wako kama unavyoona wanavyo piga akina Cena.
Zile sio ndondi ni mieleka ambayo inabidi umgonge mpinzani ili kumchosha tu halafu umbane chini asifurukute ndipo upate ushindi.
Angalia hata mateke yao, sio kama yale yanayotumika kwenye Kick-Boxing. Hayaruhuiwi katika mieleka.
Mieleka unatumia, labda niseme mapigo ya vifuti vya mkono au mguu, na sio viwiko au visigino vyake.
Hayo mapigo unayoyatake wewe hayaruhusiwi katika mieleka. Ni sheria za mieleka.
Hayo mapigo unayo yataka wewe yanatumika katika mchezo mwingine unaitwa " Free Boxing" nadhani unaujua ambao watu wanapigana kwa staili yoyote ile na kuangushana na kukabana, yaani tumia mbinu yoyote ile ilimradi ushinde.
Mchezo huo sio kick-boxing wala Wrestling bali unaitwa free- boxing, ambao wachezaji wake wengi wanachora tatoo mwilini mwao nadhani ushawahi kuuona katika tv.
Mieleka ina sheria zake za upigaji na ndio unaona kama wanatania kwakuwa hawapigi ngumi halisi au teke ni kwamba vinakatazwa kisheria, inamaana ungehama kutoka Wrestling na kuwa Free-boxing.
Wewe unataka wapigane kama free-boxing huo ni mchezo mwingine kaka.

Kuhusu kujirusha.
Kabla ya kuanza kucheza mieleka kuna hatua ambazo inabidi upitie yaani mazoezi ya awali.
Ila kwanza inabidi ujue kupata point katika mieleka hakutokani na kupiga, yaani ngumi au teke halikuongezei pointi.
Sasa kule wanako jifunza mieleka wanajifunza pia mbinu ya kumdanganya mpinzani wako kama vile unaelekea kupigwa au kuchoka.
Mchezaji anaweza kusukumwa kidogo tu akaanguka sana au kujirusha ili umwone kuwa amechoka au kalegea ili uingie kingi ya kujiaamini halafu ndio akushike vizuri.
Wakati mwingine unatathmini nguvu ya mpinzani wako, hivyo watazamaji wanaona kama ubapigwa sana na unaeleke kushindwa kumbe ni hadaa tu ya kumiliki pambano.
Mieleka sio ngumi ni kufanya juhudi za kumlegeza mpinzani wako hadi achoke ili umwangushe na umbane na ahesabiwe hati tatu bila kufurukuta ndipo unapopata pointi.
Wewe unachanganya michezo.
Ungekuwa unaniuliza kipengele kimoja kimoja ningekufafanulia vizuri zaidi.
Ila kaa ukijua mieleka sio ngumi wala mateke.

Mkuu rudi kuangalia isee , ur one way to understanding their fake acting .
Hayo mambo ya hawapigani ngumi za kawaida ni story tu za kutetea mieleka ambazo hazina mashiko.

Mbona vichwa wanapigana na hawavimbi? Unajua ngumi na kichwa kipi kinaumua haraka?
Kumbamiza mtu kwenye angle ya ulingo na vyuma ni zaidi ya kumpiga ngumi na hapo hapo inabidi aumuke au apasuke lakini akiinuka uso kama haujaguswa...

Narudia tena wale jamaa hawapigani hata kidogo ngumi zinaishia tu hewani na mateke hayawapigi bali yanarushwa kijanja mpaka karibia na mwili then aliyepigwa ana act kama kafa na hii ni kwa mechi zote hata wrestemania .

Chek hii mechi ilikuwa serious lakini angalia walichokifanya ni ngumu kugundua hasa kama hautazami kwa umakini


Na hiyo unasema siyo mechi serious ...

Muangalie triple h hapa chini utaelewa kinachofanyika na hapa anaonyesha jinsi ya kupiga ngumi ambazo wewe unasema haziruhusiwi..



Usipoelewa hii video mkuu basi itakuwa hutaki kuelewa
 
Ndio.maana ikaitwa ENTERTAIMENT yaani ikawekwa daraja moja na MOVIE NA MUSIC NA MATV SHOWS..MAANA HIZO NDIO ENTERTAIMENTS......SIO SPORTS KAMA SOKA RUGBY UKITAKA KUONA.MIELEKA YA UKWELI NI ILE YA OLYMPIC.....HUWEZI MKUTA JOHN CENA OLYMPIC
 
Mkuu rudi kuangalia isee , ur one way to understanding their fake acting .
Hayo mambo ya hawapigani ngumi za kawaida ni story tu za kutetea mieleka ambazo hazina mashiko.

Mbona vichwa wanapigana na hawavimbi? Unajua ngumi na kichwa kipi kinaumua haraka?
Kumbamiza mtu kwenye angle ya ulingo na vyuma ni zaidi ya kumpiga ngumi na hapo hapo inabidi aumuke au apasuke lakini akiinuka uso kama haujaguswa...

Narudia tena wale jamaa hawapigani hata kidogo ngumi zinaishia tu hewani na mateke hayawapigi bali yanarushwa kijanja mpaka karibia na mwili then aliyepigwa ana act kama kafa na hii ni kwa mechi zote hata wrestemania .

Chek hii mechi ilikuwa serious lakini angalia walichokifanya ni ngumu kugundua hasa kama hautazami kwa umakini


Na hiyo unasema siyo mechi serious ...

Muangalie triple h hapa chini utaelewa kinachofanyika na hapa anaonyesha jinsi ya kupiga ngumi ambazo wewe unasema haziruhusiwi..



Usipoelewa hii video mkuu basi itakuwa hutaki kuelewa
Wewe ndio naona ni mgumu kuelewa.
Nimeshakuambia purukushani Unazo ziona katika mchezo wa mieleka zinalenga kumchosha mpinzani na sio kumuumiza.
Ivi mbona huulizi kwenye ngumi kwanini hawapigi ngumi kwenye kitovu au kwenye pum.bu na maeneo mengine nyeti ?
Ni kwa sababu wanafuata sheria za mchezo wa ngumi.
Mieleka pia ina sheria zake maalum.
Tuanze na Clip ya Undertaker,
Undetaker hapo unapoona nia yake ni kumlegeza mpinzani wake tu kwa kumkita kwenye miguu yake na sio kumvunja shingo kwa kumkita kwenye sakafu ya jukwaa kama unavyotaka wewe.
Wewe unachotaka hapo ni amtwange kichwa chini na lazima shingo itavunjike.
Hii sio sheria ya Mieleka, kama inavyokatazwa kupiga ngumi halisi.
Hao wana mieleka wanasaini mikataba ya kuheshimu kanuni na taratibu za mchezo wa mieleka.
Na huo ni mchezo tu kama mpira wa miguu ambao una aina yake ya kuucheza.
Wachezaji wa Mieleka wanaheshimiana kama kawaida tofauti yao inakuwa kwenye mchezo tu.
Ukitazama vizuri kila mchezaji wa mieleka ana namna yake ya kumaliza pambano ni kama symbol yake, akishaona tayari mpinzani wake ameshalegea na kusalim amri.
Undertaker anamnyanyua na kumkita kwenye miguu na kumlaza chini na kukunja mikono yake kifuani.
Cena, Orto, na wengine wote wana namna zao za kumaliza pambao, hiyo ktk mieleka inaitwa The final touch, yaani kabali ya kumaliza pambano.
Kila mchezaji ana kabali yake na anaweza kuwa na kabali zaidi ya moja.
Hiyo ni stali ya The Dead Man Undertaker. hizo staili zinazingatia kanuni na sheria za mieleka.
Twende kwa Triple H
Hapo anawakochi underground mchezo wa mieleka.
Kwenye mchezo wa mileka kuna jinsi yake ya kucheza ili kuunogesha au kuuitikia inavyopasika.
Kwamfano mpinzani akikunyanyua ukiona kakushika pabaya basi elekea kadri anavyokupekeka, kwani ukiacha kufuata uelekeo unaweza kuvunjika kirahisi kwa ule ukinzani wa jitu lililoshiba.
Kwahiyo hapo Triple H anafundisha jinsi ya kuitikia pigo la kwenye mieleka, yaani ukipigwa nawewe unafuata kwa kama kushtuka, ili kuonekana kuwa pigo limekuingia sawasawa na watazamaji au mpinzani wako.
Kwa ujumla hizo ndizo ladha za mieleka ambazo H anazifundisha, kama unaangalia mashindano ya nguvu basi utathibitisha kuwa katika kila aina ya mapambano kuna staili zake za kupiga na kudansi au kunepanepa kwa mpigaji au mpigwaji.
Angalia Judo, Kaleti, Ngumi, Sumo nk. Utaona sio kuna mapigo tu, lakini ladha ya mchezo inavyochukuliwa na mnepo wa mwili.
Hayo ndiyo manjonjo ya mieleka ndugu yangu.
Mieleka nimchezo na sio ugomvi wa kutaka kukomoana au kuvunjana viungo.
Wengi wanashindwa kuufahamu mchezo wa mieleka kwakuwa tu hawajui jinsi unavyochezwa.
Hapo zamani za kale mchezo wa mieleka ulichezwa bila kugonganagongana au kusukumana.
Yaani mnapanda jukwaani na kuanza kushikana mieleka.
Ikaonena wachezaji wanaweza kushikana na kuwa kimya bila hata kuyumba yumba kwa muda mrefu sana hata kupoteza ladha ya mchezo, ndipo wakaruhusu kuingiza mapigo yenye kuweza kuchoshana tu na sio kuvunjana shingo kama unavyotaka afanye Undertaker.
Ndipo wakaingiza hiyo misukumo, migusano, miminyano na hata mapigo yenye lengo la kumchosha mpinzani ili aweze kuanguka kirahisi na kubanwa na kushindwa pambano.
Humo kwenye jumba la WWE kuna Polisi maalum wanaoangalia mapambano yote.
Ukimpiga mpinzani kinyume na taratibu na unaendelea kumpiga wanaitwa na unatiwa pingu na unapelekwa polisi kufunguliwa mashataka ya kukiuka sheria za mieleka.
Mjomba mieleka sio ugomnvi na una namna yake ya kuucheza kama unavyoona wenyewe wavyoucheza.
Staili zenye nia ya kuvunjana viungo haziruhusiwi, la sivyo kwa hiyo miguvu yao kila siku wachezaji wangekuwa wanavunjana mifupa.
Ushanifahamu ndugu yangu
 
Ndio.maana ikaitwa ENTERTAIMENT yaani ikawekwa daraja moja na MOVIE NA MUSIC NA MATV SHOWS..MAANA HIZO NDIO ENTERTAIMENTS......SIO SPORTS KAMA SOKA RUGBY UKITAKA KUONA.MIELEKA YA UKWELI NI ILE YA OLYMPIC.....HUWEZI MKUTA JOHN CENA OLYMPIC
Ule wa kwenye Olympic ni aina ya mieleka kavu, hauna manjonjo kama ya akina Cena.
Mieleka ya akina Cena inaitwa
Free Style Wrestling na haichezwi kwenye olympic kwakuwa maandalizi yake ni makubwa na una Risk kubwa.
Ni kama mchezo wa Boxing.
Huwezi kuuona Free Style Boxing kwenye Olympic. Ule ambao wachezaji wake wengi wanachora tatoo mwilini na wanavaa Gloves nyepesi.
 
MTU anapigwa ngumu lakini havimbi.
Mieleke imenishinda kuangalia.naona kama wanatufunga kamba vile
 
MTU anapigwa ngumu lakini havimbi.
Mieleke imenishinda kuangalia.naona kama wanatufunga kamba vile

Hakuna Entertainment (Uburudishaji) mtamu kama mieleka unaondo stress maana utacheka utachukia kisha utakuwa unapenda kuangalia, Tatizo sisi watanzania tunataka mieleka iwe sports kama vile Ngumi, mpira nk
 
Back
Top Bottom