Siku kama ya leo tarehe 9 November 1990 Ukuta wa Berlin uliangushwa.
Picha hiyo hapo chini nilipiga kama kumbukumbu yangu ya Ukuta wa Berlin nilipofika Berlin pale ulipokuwapo ukuta huo maarufu uliokuwa ukifahamika kama Berlin Wall.
Picha hiyo ya sanamu ya watu waliobeba sanduku niliikuta karibu na kituo cha treni Berlin na pameandikwa kuwa ni kumbukumbu ya kuwakumbuka watu waliokuwa katika hekaheka ya kusafirishwa huku na huko kwa tabu na dhiki kubwa wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia.
Picha hiyo nyingine ilikuwa ndani ya bustani ndogo karibu na mtaa niliokuwa nikiishi Berlin na kila asubuhi nikienda ofisini kwangu na kurudi jioni nikipita ndani ya bustani hiyo nikipenda kuiangalia na kilichokuwa kinanivutia ni huyo mpiga piano.
Trump na Netanyahu wako busy kusimika hizo kuta tena, wakati huku kuna mtu anajenga kuta mioyoni mwa watu. Nineshangaa kuanza kusikia mama mmoja anamtimua mpangaji wake kisa anaunga juhudi za upande anaouona yeye ni wakidhalimu.
Shukran Mzee wetu kwa bandiko na hasa hizo picha muruwa, je unaweza kutukumbusha japo kwa uchache busara ya ujenzi wa ukuta huo na maamuzi ya kuamua kuvunja ukuta wa gharama hivo.