Aliyekuwa diwani wa kata ya Namilembe wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza Innocent Joseph Lusato kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ametangaza kujiudhuru na nafasi zake zote ndani ya chama hicho na kutangaza kujiunga na chama cha Mapinduzi CCM.
Akitangaza maamuzi hayo Lusato ameeleza kuwa CHADEMA hakuna maendeleo zaidi ya malumbano huku akisisitiza hajanunuliwa.
Mara nyingi tunaamini wanasiasa wanaweza kutatua matatizo yetu lakini tunasahau ni haohao wanasiasa wanaleta MATATIZO, kwa mfano kwenye kampeni zake aliahidi ,huduma bora za elimu, afya, miundombinu nk kwa kuhama kwake kodi zetu inabidi zitumike kufanya uchaguzi badala kuendelea kuboresha huduma kwa wananchi