Majeshi ya waasi yamefanya mashambulizi makubwa Kaskazini-Magharibi mwa Syria, na kuyateka maeneo ya wanajeshi wa Rais Bashar al-Assad, huku wapiganaji 180 wa pande zote mbili wakiuawa kwenye mapigano pamoja na raia 19.
Kundi hilo la Hayat Tahrir al-Sham (HTS) tayari limechukua vijiji kadhaa vilivyokuwa chini ya majeshi ya serikali pamoja na kambi moja ya kijeshi ya Syria.