Issue ni kwamba hata World Bank na International Monetary Fund wanaisifia Tanzania kuwa sasa hivi iko katika kundi la Group B as a "Good student". Ila ukweli ukiangalia Tanzania kwa sasa inakuwa kulingana na GDP tu lakini upande wa elimu na afya bado tuko nyuma sana kama Mkuu ulivyoongelea hapo juu. Ila kama mtu ni mchumi mzuri utagundua kuwa taarifa zote zitolewazo na zserikali na Millenium Development goals huwa sio za ukweli sababu serikali inataka kuwaridhisha hawa wanaotoa misaada ili misaada iongezeke, sasa ukweli ni kwamba tunao wachumi wazuri sana Tanzania na wanalijua hilo kwamba Neo liberal haifanyi kazi bila kuwa na government intervention. Ila mpaka sasa tumekwisha potea na hii serikali yetu iliyojaa wala rushwa.
Kwa nini tusiigie mfano wa wenzetu wa China na Korea wameweza kuendelea bila hata kuwa na huu mfumo wa soko huria sio zuri kabisa kwa maendeleo ya nchi. Au tuwe na soko huria na government intervention pia lakini tukiwaachia hawa ma capitalists kutuamulia kila kitu matokeo yake hata taarifa pia wanatuamulia namna ya kuandika, wakati umasikini unaongezeka wao wanasema umasikini unapungua.
jamani tuamke wananchi tuchague viongozi wanaofaa.