Wachache wanaelewa hiliKama mwanadam unajua hasa hatari ya kuongoza watu na jukumu ulionalo daima ungalikumbia uongozi
Uongozi ni Amana Nzito
Mtume Muhammad (S.A.W.) alisema:
"Hakika, uongozi ni amana. Na Siku ya Kiyama, itakuwa ni fedheha na majuto, isipokuwa kwa yule aliyechukua jukumu lake kwa haki na akatekeleza kwa usahihi."
(Sahih Muslim, Hadith 1825)
Maana: Uongozi ni dhamana kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na mtu anayeshindwa kuutimiza kwa haki ataangamia.
---
2. Mtume alikataa Kutafuta Uongozi
Mtume Muhammad (S.A.W.) alionya kuhusu kutamani nafasi ya uongozi. Alisema:
"Ewe Abu Dharr! Hakika wewe ni dhaifu, na uongozi ni amana. Siku ya Kiyama, utakuwa ni sababu ya fedheha na majuto isipokuwa kwa yule anayeutekeleza kwa haki."
(Sahih Muslim, Hadith 1826)
Maana: Mtume alimfundisha Abu Dharr kwamba uongozi ni jukumu kubwa ambalo si kila mtu anaweza kulimudu.
---
3. Kukatazwa Kutamani Uongozi
Mtume Muhammad (S.A.W.) alisema:
"Usitafute uongozi, kwa kuwa ikiwa utakutafutia mwenyewe, utapewa bila msaada wa Mwenyezi Mungu. Lakini kama uongozi utakufikia bila kutafuta, utasaidiwa (na Mwenyezi Mungu)."
(Sahih Bukhari, Hadith 7149)
Maana: Kutamani au kutafuta uongozi kunadhihirisha tamaa ya kibinafsi, ambayo mara nyingi husababisha kushindwa kutekeleza jukumu hilo kwa uadilifu.
---
Hatari za Uongozi
1. Uwajibikaji Mkubwa: Kiongozi ataulizwa kuhusu kila alilowasimamia watu wake, hata mambo madogo.
Mtume alisema:
"Kiongozi ni mchungaji wa watu wake, naye ataulizwa kuhusu uchungaji wake."
(Sahih Bukhari, Hadith 893)
2. Dhambi za Kutenda Isivyohaki: Kiongozi anayefanya maamuzi yasiyo ya haki hujichumia dhambi kubwa. Qur'an inasema:
"Na mwenye kudhulumu atakuwa na adhabu kubwa."
(Surah Ash-Shura, 42:42)
3. Majaribu ya Dunia: Uongozi unaweza kumjaribu mtu kwa kupenda mali, sifa, au madaraka zaidi ya kumtegemea Mwenyezi Mungu
KWA HALI KUNA HAJA YA KUUMIZANA?
Wengi tunaamini uongozi ni ujanjaWachache wanaelewa hili
Uongozi wa kukimbia na sio wa kuwaania hata kwa kudhuru wengine. Uongozi ni mtihani SanaWatawala wanaongoza nchi kupitia ulimwengu wa giza ndio maana ni ngumu kuona Wana hofu ya kuua raia wao!!
Sio yeye tu, kila kiongoziUJUMBE MZURI SAMIA ASIKIE
Mbona huyu kiongozi aliyeamin ni mtesaji wa wapinzani wake kisiasa?Kama mwanadam unajua hasa hatari ya kuongoza watu na jukumu ulionalo daima ungalikumbia uongozi
Uongozi ni Amana Nzito
Mtume Muhammad (S.A.W.) alisema:
"Hakika, uongozi ni amana. Na Siku ya Kiyama, itakuwa ni fedheha na majuto, isipokuwa kwa yule aliyechukua jukumu lake kwa haki na akatekeleza kwa usahihi."
(Sahih Muslim, Hadith 1825)
Maana: Uongozi ni dhamana kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na mtu anayeshindwa kuutimiza kwa haki ataangamia.
---
2. Mtume alikataa Kutafuta Uongozi
Mtume Muhammad (S.A.W.) alionya kuhusu kutamani nafasi ya uongozi. Alisema:
"Ewe Abu Dharr! Hakika wewe ni dhaifu, na uongozi ni amana. Siku ya Kiyama, utakuwa ni sababu ya fedheha na majuto isipokuwa kwa yule anayeutekeleza kwa haki."
(Sahih Muslim, Hadith 1826)
Maana: Mtume alimfundisha Abu Dharr kwamba uongozi ni jukumu kubwa ambalo si kila mtu anaweza kulimudu.
---
3. Kukatazwa Kutamani Uongozi
Mtume Muhammad (S.A.W.) alisema:
"Usitafute uongozi, kwa kuwa ikiwa utakutafutia mwenyewe, utapewa bila msaada wa Mwenyezi Mungu. Lakini kama uongozi utakufikia bila kutafuta, utasaidiwa (na Mwenyezi Mungu)."
(Sahih Bukhari, Hadith 7149)
Maana: Kutamani au kutafuta uongozi kunadhihirisha tamaa ya kibinafsi, ambayo mara nyingi husababisha kushindwa kutekeleza jukumu hilo kwa uadilifu.
---
Hatari za Uongozi
1. Uwajibikaji Mkubwa: Kiongozi ataulizwa kuhusu kila alilowasimamia watu wake, hata mambo madogo.
Mtume alisema:
"Kiongozi ni mchungaji wa watu wake, naye ataulizwa kuhusu uchungaji wake."
(Sahih Bukhari, Hadith 893)
2. Dhambi za Kutenda Isivyohaki: Kiongozi anayefanya maamuzi yasiyo ya haki hujichumia dhambi kubwa. Qur'an inasema:
"Na mwenye kudhulumu atakuwa na adhabu kubwa."
(Surah Ash-Shura, 42:42)
3. Majaribu ya Dunia: Uongozi unaweza kumjaribu mtu kwa kupenda mali, sifa, au madaraka zaidi ya kumtegemea Mwenyezi Mungu
KWA HALI KUNA HAJA YA KUUMIZANA?
Quran imeenda mbali zaidiYesu Kristo alisema " kuongoza Watu ni Kuwa Mtumishi Wao"
Naunga mkono hoja 🌹
Hapa hajakusudiwa yeye tu, kila kiongozi mwenye dhamana ya anaongoza watu anaingia hapoMbona huyu kiongozi aliyeamin ni mtesaji wa wapinzani wake kisiasa?
InshallahHapa hajakusudiwa yeye tu, kila kiongozi mwenye dhamana ya anaongoza watu anaingia hapo
Hujafahamu, ukisoma huku ukiwa na bia mdomoni ndio athari yake.Kwanini "Mtume" alikataza uongozi wakati tayari yeye ni kiongozi,,,,,,,,,,?
Mtume Muhammad (S.A.W.) aliomba:Kwanini "Mtume" alikataza uongozi wakati tayari yeye ni kiongozi,,,,,,,,,,?
Lkn wote wanaoapa hutumia Quran au bibliaTatizo kubwa ni kwamba "uwepo wa Mungu ni dhana ambayo si kila mwanadamu anaiamini".