Tukutane Oktoba

yero

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2015
Posts
471
Reaction score
425
Hapa tunazungumzia yale ambayo chama Tawala (CCM) kimefanya kinachoweza kumshawishi mtu yeyote akipigie kura ifikapo Oktoba 2015.

Yale ambayo UKAWA wanataka kufanya vinavyoweza kumshawishi mtu yeyote afikirie kupiga kura kuiondoa CCM madarakani na kuwaweka UKAWA.

Yale ambayo vyama vingine vya upinzani ikiwemo ACT Wazalendo wanataka kufanya ili kuleta maendeleo kwa ajili ya nchi yetu ya Tanzania.

Zingatia: Mzee wa magogoni kasema kazi ya kuongoza nchi haina shukrani “thankless” akimaanisha amefanya vingi watu wanakuwa wagumu kuona.

Naamini uchangiaji kwenye uzi huu utawafungua macho wale ambao huwa hawana kawaida ya kupiga kura na wale wapiga kura kwa mara ya kwanza kufanya maamuzi ya kujiandikisha na kupiga kura.
 
Mwaka huu UKAWA nampa, ila sijajua wanataka kufanya nini lakini naona vitu vingi wako tofauti na CCM kuanzia masuala ya ufisadi, ukosefu ajira kwa vijana, kuua sekta ya viwanda TZ, Kuongezeka kwa umaskini baina ya waTZ wengi n.k. ACT wazalendo sijawahi hata kufikiria kuwapigia kura.
 
UKAWA mwanzo mwisho, nishachoka na CCM. Miaka 50 mingi sana kwa chama kimoja kukaa madarakani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…