Today is World Wildlife Day

Zurie

JF-Expert Member
Joined
Jul 6, 2014
Posts
2,059
Reaction score
5,778
Leo ni maadhimisho ya siku ya kimataifa ya viumbe hai wa porini na majini ambayo huadhimishwa kila mwaka mnamo Machi 3 ili kueneza uelewa wa mimea na wanyama mwituni

Mwaka huu, siku hii imefanywa mahususi ya kueneza uelewa kuhusu viumbe hai wa majini na umuhimu wao kwa maendeleo ili kuhakikisha wanatunzwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Tanzania imebarikiwa kuwa na viumbehai lukuki walio nchi kavu na majini. Wanyamapori walio katika mbuga mbalimbali wamekuwa vivutio kwa watalii na kuleta ukuaji wa pato la taifa.

Mwaka 2018, hifadhi ya wanyamapori ya Serengeti iliibuka kuwa bora kuliko zote Afrika ikiipita Mala Mala ya Afrika Kusini na Mana Pools ya Zimbabwe katika utafiti uliofanywa na kampuni ya utalii ya Safari Bookings.
 
Wakati tuna adhimisha siku ya leo tuendelee kupiga vita ujangii huu uliowekwa kisheria.

Hivi inakuaje unaruhusu kuwinda tembo, chui au simba wakati inafahamika kabisa hawa wanyama wanakaribia kutoweka?
 
Binadamu tuna kazi sana hao wanaofanyiwa hata hawana habari yoyote hlf utakuta sisi ndo tunakula mvinyo na nyama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…