Gharama za kutumia miamala ya simu zinabadilika lika kukicha na hakuna taatifa kwa watumiaji. Kwa sasa ukituma 70,000 kwa tigopesa unakatwa 3,100, hapo kwanza kiwango kilikuwa chini sana nadhani 350 kwa mtumaji na mpokeaji ndio anakatwa zaidi wakati wa kutoa. kwa sasa si mtumaji wala mpokeaji wote ni kuchinjwa fungu refu.!
Swali la kujiuliza; Ni sahihi kwa mtumaji na mpokeaji kulipishwa tozo kubwa kiasi hiki?
Twaelekea wapi na maisha haya magumu kila kona??
Lazima tupige kelele kwa kweli, maaana speed ya lori inaongezeka na barabara ina makorogesheni kibao!!
Basi kuna wizi wa chini kwa chini. Nimetuma 70,000 na nimekatwa shs 3100.[emoji30] [emoji30] ! Uchakachuaji wa juu kwa juu!!Hebu tueleweshane...kutoa kwa wakala ndio gharama ziko juu sana ila kutuma tigo-tigo 70,000 haifiki 3,100/-
Nimettuma 280,000 ada 1,000
Nimmetuma 150,000 ada 800
Nimetuma 10,000 ada 300
Nimetuma 25,000 ada 350.
Nimetoa 700,000 ada 7,500
Nimetoa 350,000 ada 6,000
Nimetoa 250,000 ada 5,000
Hapo unaweza kuona kutuma gharama sio kubwa kulinganisha na kutoa. Kutuma 70,000 haifiki 3,100.
Kuliko kwenda kwenye ATM wacha niitume kwa tigo pesa tu. Sio kila mtu yuko karibu na ATM ambazo hazina uhakika wa kuwa na hela vile vile hasa weekend.Mpango mzima ni kutumia Bank... natumia MILLIONI moja yangu kwenye Ac yangu ya crdb kutoka kwenye tigo pesa yangu CRDB nakatwa buku na tigo pesa then naenda kweny ATM natoa Mara tatu nakatwa 1800 hapo nimeokoa zaid ya buku sita,
Bora turudi kwenye ATM hzi simu pesa zinatufilisi bila kujijua
Hivi branch ya NMB maeneo ya Mwembe Mdogo Kigamboni iko wapi?NMB ipo kila sehemu ya nchi hii.
Hawa mitandao ya simu ni wezi sana.