ITEGAMATWI
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 5,362
- 4,125
Nimekuwa na tatizo hili kwa muda sasa, huwa linakuja na kuondoka lakini kwasasa naona linataka kuwa sugu. Kuna wakati nikiwa nimelala tu usiku basi misuli inakaza kwa nguvu na kuleta maumivu makali sana hasa misuli ya paja na ile ya nyuma ya ugoko, naomba ushauri wa kitabibu kujua hiki ni kitu gani na tiba yake ikoje. Mimi si mtu wa mazoezi sana na nikifanya mazoezi basi ni ya kunyanyua vitu vizito mara chache.