Tanzania Vs Morocco

Tbc, tbc,, tbc, tumewatafuta saaana hamkuonyesha mpira kwa sisi wa mikoani, mmeonesha mwishoni mwa kipindi cha kwanza na HT mkaanza uchambuzi ilipoanza kipindi cha pili mkahamia DIA kwa kuwasili kwa rais wa China, ama kweli mnatakiwa mjitadhimini zaid, at least muwe na channel zaidi ya 5 kwa jinsi watazamaji wenu walivyo na hobi zao. eg Music, sports, news, dramas, etc etc etc kweli leo mmetuangusha Watanzania wenzenu. Tulikuwa tunaisubiri mechi hii kuishuhudia kwa macho lakini wapi??????? sisi wa mikoani, kama msingeweza basi mngewaachia wengine watuoneshe mwanzo mwisho kuliko kutuchanganyia habari!! Ama kweli Tanzania kuna mengi.
 
Samatta na Thomas wakiwapelekesha wamanga na kisha Samatta akifanya vitu vyake tena

source: xavier belleVue But 3 pour Maroc (3-0) Tanzanie 24-03-2013 مباراة المغرب ـ تانزانيا
 
Last edited by a moderator:
Waarabu wa Maghreb hawaamini macho yao

Source: xavier belleVue Maroc (3-0) Tanzanie 24-03-2013 مباراة المغرب ـ تانزانيا
 
Last edited by a moderator:
Huyu Dogo ni hatari sana, pale Msongamanoni alikuwa anasugua benchi, ajabu! Anatakiwa aende Arsenal haraka sana, ni mkali zaidi ya DEMBA BA.

Mkuu,
Ni kweli kabisa vijana kama Samatta , Ulimwengu na wengineo Taifa Stars ya sasa mpira wanaocheza ni wa kiwango cha juu kama timu yoyote ya Ulaya, South America, Africa magharibi/kaskazini jinsi wanavyojipanga, mashambulizi , uchu wa ushindi na professionalism ya uchezaji mpira.

Goli la kwanza la Taifa stars kupitia kwa Ulimwengu:

Source: xavier belleVue Goal 1 Tanzania (3-0) Maroc مباراة المغرب ـ تانزانيا 24 /03/2013
 
Last edited by a moderator:
Somo muhimu ambalo Watanzania hatuna budi kujifunza leo ni kuwa; ikiwa tutaamua kwa dhati kabisa kutoka ktk sakafu za mioyo yetu, tunaweza kuibadilisha kabisa nchi yetu:
1. Kushinda ufisadi na rushwa
2. Kupaa kiuchumi
3. nk nk....
 
Standings
Team MP GF GA Pts
CIV 3 7 2 7
TAN 3 5 4 6
MAR 3 4 6 2
GAM 3 2 6 1

Results
Date Venue Matches
24/03/13 15:00 Dar Es Salaam Tanzania 3:1 (0:0) Morocco
23/03/13 17:00 Abidjan Ivory Coast 3:0 (0:0) Gambia
10/06/12 16:00 Dar Es Salaam Tanzania 2:1 (0:1) Gambia
09/06/12 21:00 Marrakech Morocco 2:2 (1:1) Ivory Coast
02/06/12 17:00 Abidjan Ivory Coast 2:0 (1:0) Tanzania
02/06/12 16:30 Bakau Gambia 1:1 (1:0) Morocco

FIXTURES
07/06/13 TBA Gambia - Ivory Coast
07/06/13 TBA Morocco - Tanzania
14/06/13 TBA Morocco - Gambia
14/06/13 TBA Tanzania - Ivory Coast
06/09/13 TBA Gambia - Tanzania
06/09/13 TBA Ivory Coast -Morocco
 
Tanzania vs Maroc 3-1 All Goals & Full HighLights 24.03.2013 HD


Source: LigaHDBut

Hawa waarabu eti Thomas odemweige! kweli Thomas Ulimwengu, Samatta na timu nzima ya Taifa stars ni ya viwango vya kimataifa
 
Last edited by a moderator:
match kati ya star vs Morocco nani kashinda na kwa bao ngapi nipe jibu uliye shuhududi mechi
 
kwa tusio Bongo wapi tunaweza kutazama hili game? Nipeni links.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars.
Angalia magoli mkuu

 
Last edited by a moderator:
WA-UKENYENGE,kuna jamaa mmoja alikuwa ananiambia bhasukuma ku-nyo nolo okosataga bhoyi bhatogilwe doho!!sijui ina maana hani ila nikiangalia hiyo avatar yako mmmh labda kweli!!
Hahahahah teh teh teh teh Mkuu Zamaulid, umeona mkuu eeeh yaani huku kwetu ukiona hivyo basi ng'ombe zizi zima zinakwenda. Lakini siku hizi imepungua, zamani ndo usiseme.
 

Kuna watu wengine wana damu ya kunguni. Kaseja kazi aliyofanya jana ni kubwa kuliko wengi tunavyoweza kujua. Hata goli alilofungwa ukiangalia vizuri, mpira ulikuwa ni shuti la kushtukiza, la chini tena liliokwenda pembeni kiasi ilikuwa n ni ngumu kuukamata vizuri.

Kiufundi na utekelezaji wa majukumu yake, he is by far the best goalie we have in Tz currently.
 
Hongera sana Stars! Jana mmecheza mpira mzuri sana. Morroco walitaka kupambana lakini hatimaye walikubali kushindwa na wakabaki wanakaba kwa macho! kwa tuliokuwa uwanjani tunajua almanusra ziwe tano jana! Ilikuwa siku nzuri sana kwa Tanzania na Mungu aendelee kutubariki hivi hivi! Kwa hakika tunao uwezo wa kuongeoza hili kundi. Hata Ivory Coast tukijipanga vizuri na kuwapa motisha wa kutosha vijana na kuwatuliza kisaikolojia, lazima tutawafunga hapa kwetu huo mwezi wa sita. Morroco kwao wala hawatatusumbua kihivyo kama ambavyo tulihofia. kwa sisi tuliocheza mpira ni wachezaji very average sana. Tukitulia, hasa kwenye midfield, na hivi wanatujua tulivyo wabaya kwenye counter attacks, lazima tutawafunga kwao! na hapo ndo kiama kitakapowashukia Ivory Coast watakapotua hapa! Mungu Ibariki Tanzania tena na tena!!!
 
Nilifarijika sana kumwona Juma Pondamali akilisakata rumba pale uwanjani. kwa kweli furaha niliyokuwa nayo, nilitamani kujiunga nae ktk kucheza na kusheherekea ushindi huu mtamu na muhimu! sijui wapi ntapata caption yake nimcheki tena akifurahia utanzania wake na ushindi kwa watanzania!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…