The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,696
- 18,366
Mr Zero, bwana Sumaye, ambaye pengine haeleweki kuliko waziri mkuu yeyote, sasa amekuwa betri ya mgombea wa UKAWA mzee Lowasa.
Kuingia Sumaye katika UKAWA hakuna mantiki au maelezo yenye maana, zaidi ya kuongelea mageuzi na mabadiliko ambayo wakuu hawa hawayaelezi wala kufafanua.
Kama UKAWA walitegemea kuwa wamelamba dume kwa kumchukua Lowasa sasa ni dhahiri, kama alivosema Dr Slaa, wote wawili ni liability toka CCM.
Lowasa ni mtu ambaye katika miaka zaidi ya nane kuwa backbencher bungeni, hana mawazo wala mchango wowote wa kukumbukwa bungeni.
Lowasa alikuwa bubu na mtu asiye na mawazo yoyote kiitikadi hata kwa chama kilichomtosa.
Tumeona sasa kuwa muendekezo wa ububu wa Lowasa katika UKAWA ni katika hotuba ambazo hazina maana wala kina kisiasa. Hotuba zote za Lowasa ni utu.mbo mtupu kisiasa na anaongea kama mwana CCM aliyechoka na ambaye Baba wa Taifa alisema ni wa kuogopwa kama Ukoma!
Kuingia kwa Sumaye katika UKAWA, zaidi sana sana ni kumuokoa Lowasa na aibu ya kutoweza kujieleza kiufasaha.
Sumaye anaongea mambo mengi ambayo si sera wala dira mpya inayotakiwa kama mbadala wa CCM.
Sumaye anamwaga radhi tu maana Sumaye is not a thinker and has never been one.
Miaka yote Sumaye amekuwa mtu wa kutumwa na kutekekeza, na si kupanga na kustrategize.
Hivyo basi huu ubetri wa Sumaye kwa Lowasa, kama alivyosema Mkapa, ni kama malofa wawili waliopotea njia.
Mtu amshauri tu Sumaye kuwa kulaumu mfumo uliopo kila lofa anaweza, na kina Mbowe wamefanya kazi hiyo vizuri zaidi.
Kinachotakiwa ni kuonyesha njia, kule UKAWA wanakofikiri kina Sumaye na Lowasa wanataka watanzania waende.
Mkuu swala la Mapa na wanaMtandao ni kitendawili ambacho hakijateguliwa bado.Labda ungetueleza pia kwa nini Mkapa alituwekea mtu bogus kwa miaka kumi kama mtendaji mkuu wa serikali. Alikuwa na nia gani kwa Taifa letu.
Kama waliweza kutuwekea bogus kwa miaka yote hiyo ni kwa nini tuwaamini leo kwa chaguo lao Magufuli, chaguo la kitengo!?
Mkuu propaganda CCM hatuko , maana hizo I maneno matupu.Hahahahahaa kwahiyo mlitakaje? Sumaye arudi CCM au mbona hamueleweki? Sumaye yupo kwenye timu ya kampeni ya ukawa au wewe unajisikia wivu?
Watanzania tumemwelewa vizuri sana Lowassa na tumempenda na mwishowe tutamchagua ifikapo tarehe 25 Oktoba
Lowassa ni jiwe mlilolikataa waashi leo limekuwa jiwe kuu la msingi, hivyo tulieni dawa iwaingie.
Mmebakiza siku 36 Ikulu ya magogoni mnaiachia japokuwa hampendi huo ndio ukweli mchungu, bora mjiandae kisaikolojia kuliko kujifanya mnajitutumua mtapata presha siku hiyo.
Ndio maana mgombea wenu anatapatapa kuiba mpaka slogan ya chadema, kwakuwa hajui sheria inakataza sasa tunampeleka mahakamani kwa wizi
Nimekujibu kipropaganda kwakuwa umeandika kipropaganda, hapa propaganda ndio makao makuu
Ni hayo tu
#MabadilikoLazima2015
#MabadilikoNiLowassa
Piiiipoooooz ...........
Naona wapo nguoni mwa CdmDah ila MAGUFULI FOR CHANGE inanogaa
Ando shifa yenu wana Ukawa, bendera fuata upepo.Umeandika rubish, rubish.... Nineona tu Mzee Mwanakijiji kalike
Endelea kutukana na kujifariji tu hapa, wenzenu UKAWA wanasonga mbele kwa kasi ya ajabu, muda si mrefu utawakuta ikulu, Lowassa anateka majiji, miji na vijiji kila anapofika.
Mkuu propaganda CCM hatuko , maana hizo I maneno matupu.
Siye tunamwaga nondo za uhakika.
Sasamwambieni mzee Zero akae chini kwanza na afikirie cha kuongea chenye manufaa kwa mkulima na mfanyakazi.
Hatujasahau Sumaye kaingia fasta UKAWA baada ya Lowassa kuongea u.tumbo wa kusema atawaachia kina Babu Seya, ati ndo sera!!!
Sumaye hayuko tofauti, upinzani si kumwaibisha Magufuli, upinzani ni kuleta sera mbadala za kutawala na kumletea mwananchi maendeleo.
Sasa kama kote kwa Sumaye wala Lowasa hakuna sera mbadala mnategemea nini?
Yule jamaa kweli ni betri!!!!Mkuu Sumaye ni opportunist na tena zero kweli! Yaani alidhani Lowassa ataanguka ndani ya wiki na ye achukue nafasi yake. Na mpaka sasa hivi hana chama. Lakini anataka kutuaminisha eti anafaa. Haeleweki na hajielewi!
Katika muda mchache ambao Magufuli amekuwa mtendaji, ameonyesha kutozembea viongozi wabovu chini yake na ni mfuatiliaji.
Lets give him a chance.
Uwe unajisafisha ukitoka chooñi....!!!!
Unaonyesha njia kama unaifahamu hiyo njia. Njia wanayoifahamu kina Sumaye na Lowassa ni CCM way!
Sumaye alisema ameingia UKAWA ili kuwafundisha kina Mbowe namna ambavyo serikali inafanya kazi kwa sababu hawana uzoefu.
Kwa maana nyingine, yaliyokuwa yanafanywa na serikali ni mazuri sana ndiyo maana ameenda kuwafundisha UKAWA. Ikumbukwe hakuna serikali nyingine ambayo Sumaye amepata uzoefu zaidi ya serikali ya CCM.