Kwanza nakupongeza kwa kumsapoti rafiki yako kwa hili, hii niliipata wanangu walipokuwa wachanga ,inasababisha maumivu makali wakati wa kunyonyesha kiasi kwamba watoto walikuwa wakianza wakitaka kunyonya mie mwili una anza kutetemeka nikifiria maumivu ntayopata
Mara nyingi tatizo ni kwamba mtoto anapopokea ziwa wakati wa kunyonya anashika chuchu tu
inatakiwa anyonye chuchu PAMOJA NA part kubwa ya sehemu nyeusi inayozunguka chuchu (areola). Ili kufanikisha hilo mtoto anapopokea breast inabidi afungue mdomo wake really wide. Baadhi ya watoto wanahitaji msaada ktk hilo..lactation consultant mmoja alinipa solution ambayo ilinisaidia sana kumaliza tatizo haraka
mtoto anapotaka kunyonya asimpe ziwa mara moja ila amguse guse kwanza na chuchu kwenye mdomo wa juu
mtoto atafungua mdomo zaidi ili kupata chuchu
atakapo fungua mdomo wake really wide amshike nyuma ya shingo/kichwa na kumsogeza kwenye ziwa a bit fast but gently and firmly..yaani mtoto afuate ziwa sio mama ampelekee mtoto ziwa mdomoni
wakati huo huo mkono mwingine wa mama ushike ziwa yaani kama analikamua hivi (breast sandwich) to make the areola longer and narrower and easier for baby to take into his mouth
maziwa ya mama pia yanasaidia sana ku soothe sore nipples, akachukue kidogo na kupaka kwenye chuchu baada ya kunyonyesha. Tatizo likiendelea aende hospitali kucheck couses nyinginezo kama candida infections etc
pia nenda kwenye discussion furum ya
www.lalechelegue.net pale kuna kina mama wanaonyonyesha na breastfeeding experts toka kila kona ya dunia, nina uhakika utapata mchango mwingi tu toka kwa wenye experience kama hii
mwisho mwambie rafiki yako asiache kunyonyesha, hili tatizo litaisha tu na mwanae atakuwa feeding expert..