Sitashangaa kuona ripoti kamili ya uchunguzi ikawa ni siri ya waliounda kamati ya uchunguzi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,022
144,380
Huu ni mtazamo wangu kutokana na historia ya Jamuhuri husika ambapo kwa nyakati tofauti zimekuwa zikiundwa tume/kamati mbalimbalu za uchanguzi na mara baada ya kamati hizo kukamilisha kazi na kuziwasilisha kwa walioziteua,matokeo ya kamati hizo hubaki kuwa siri au ripoti kamili ya uchunguzi kutotolewa.

Kwa uzoefu huu,sitashangaa hali hii ikajirudia katika kamati hii kama ilivyotokea kwa baadhi ya kamati zilizotangulia na hasa iwapo itagusa wasiotarajiwa au kuonekana inaumbua watu fulani.

Kamati hii imeundwa hivi karibuni katika nchi moja ambayo sitaitaja hapa ila iko katika Bara moja la mbali.

Tutege macho kupitia BBC au vyombo vingine vya habari vya kimataifa vitapotangaza yatakayoendelea.
 
Kamati imeundwa ili Chattle ipate muda wa kupitia CV za wapendwa wao na kuwasimika pale. Waliosimamishwa wajiandae tu na maisha mapya watakayopangiwa.
 
Uko sahihi
 
Kamati yaweza toa taarifa ambayo itakuwa sawa na mawazo ya mheshimiwa ili isilete aibu kuwa hakuwa sahihi kwa yale aliyo waeleleza watanzania kwa zile samples za papai, mbuzi nk.

Sina uhakika kama kwa kipindi hiki cha kazi ya Kamati tutaweza kupata idadi ya maambukizi mapya kwani vipimo ndiyo hivyo vilivyotiliwa mashaka. Na baada ya taarifa kama matokeo yatakuwa ya kuonesha kuwa vipimo vina shida basi idadi ya wagonjwa itaoneshwa kuwa haikuwa sahihi na watu waliofariki hawakufa kwa ugonjwa wa Corona.
 
Hii report najua haitatolewa
 
Kamati wanaenda kusomewa ilma chato kisha wao wanatype ripoti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi wale wabunge waliokataa amri ya Mbowe mtawafanya nini?
 
Kuna wimbo aliwahi imba doctor lemy ongala,kuhusu kuunda tume za uchunguzi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…