Simba walikosea kwenye usajili wamemuuza kotei Hadi sasa hiv pengo lake linaonekana kotei alikuwa mnyama ana nguvu anakaba kwelikweli aliziba udhaifu wa mabeki wa Simba ukiangalia kwa team ya Simba ya sasa mtu Kama huyu hawana.Kiufupi team aipo balance wanawachezaji wengi wakuchezea mpira wakabaji hawana mkude na fraga sio defensive midfielders Bali both ni holding midfielders.
Kosa lingine ni kumuuza okwi bila kuleta mtu sahihi wakuziba pengo lake Kama Kagere akiwa afungi okwi anatupia mpaka okwi anaondoka alikuwa mfungaji wa pili wa Vodacom premier league viongozi wa Simba wakamleta yule striker garasa wa kibrazili.Kingine msimu uliopita Simba walikuwa na tatizo la mabeki nilitegemea wakamleta mtu sahihi Kuna yule beki number 5 wa nkana ni bonge la beki lakini hajamsajili wameleta magarasa.
Kosa lingine ni kumfukuza uchebe ambaye alishatengeneza team vizuri na ameipa Simba Mafanikio makubwa msimu uliopita na mpaka anaondoka Simba ilikuwa inaongoza league na team inacheza vizuri kwa miemuko ya uongozi wakamfukuza kazi badala yake wameleta kocha garasa.
NB: Mpira wa Tanzania una haribiwa na vingozi Mara nyingi kwa maamuzi mabovu wanayofanya kwa kutofuata uweredi kwenye utendaji wao.