Sijui nimekosea wapi chapati zinavunjika kama mti mkavu

Mambo ya kuthubutu haya sometimes noma sana!! Yaani nimejifunza humu humu JF jinsi ya kupika Chapati.

Sasa leo si wageni wakawa wengi hapa home yaani wageni wa kike, nikaona
hapa ndo pa kuchukua ujiko.

Mwanaume nikafuata hatua zote tena kwa kusoma, nikapika kama chapati nnehivi!!! Kila ninayotest inavunjika "Taa" yaani kama kijiti.

Upande niliokuwa nafanyia shuguli ulikuwa unaniruhusu kutoroka muda
huu napost natoka banda umiza ambako nilijistiri kwa kuhofia aibu ya kuombw chapati ngumu.

Zote na yale madonge yaliyosalia nimeshaziflash huko chooni.

1. Unga ulikuwa nusu
2. Niliweka Blueband
3. Chumvi
4. Niligongea mayai 2 (mawili)
5. Hiliki ilikuwemo
6. Nikachanganya na mafuta ya kula kidogo
7..Nikatia maji ya uvugu vugu.

Dah, Noma sana!!
Ungezipiga mafuta ya taa nakuambia wasingezisogelea
 
chapati ni ukandaji, ukikanda unga ukiwa mgumu lazima zikusumbue kusukuma na pia zisiwe laini sana kias ukisukuma lile donge upate circle nzuri unaenda nayo taratibu inaelekea tu yenyewe
 
Back
Top Bottom