sijielewi


Naunga mkono huyu msemaji, kawaida sana...hata g/f wangu wa zamani hataki kuwa na mtu mwingine tena, anadai haitatokea mwanaume atakayempenda kama mimi, dah hadi namwonea huruma but ZILIPENDWA.
 
Mmmmmhhhhhhh! Dr. Love nimewasili sasa!

Huyo si kwamba unampenda sana wala nini ila ni upweke ule baada ya kumpiga kibuti ndo unakurudisha nyuma! Huyu njia pekee ya kumuacha ni SUBSTITUION method baaaaaaaasss! Yaani tafuta replacement yake kabla hujampa makavu live!!!! Bila hivo kile kipindi cha Transition period hutokiweza aiseee, utamsamehe!

Ila ukiwa na chuma kipya mambo zimenoga huna mudaaaa wa kumuwaza zilipendwa huyo! (Ila tu ukumbuke kumtendea jirani yako unachopenda akutendeeee!)
 
Naona wengi ni wavunjwa mahusiano hapa. Wanashauri umuache badala ya kukushauri uvumilie. Mvumilivu hula mbivu na utaacha waganpi?
 

Asante Lara umekuja,alianza yeye kufanya ndivyo sivyo,dharau kibao but akawa km anajirudi hvi,sass kuna mambo naona yako damuni mwake cwez badili,ngoja npate almasi nimteme mazima japo ngum
 
Dada hujaamua kidhati kabisa ndan ya moyo wako,halafu hujaichukia hiyo hali kutoka moyon,km unaweza kumvumilia hali aliyonayo vumilia kabisa kwan ukipenda boga penda na ua lake,km huwez chapa lapa kimaukwelii kwan utakuwa mtumwa wa penz tena chukia kiuhakika hiyo hali hiyo, amua kutopiga,kutopokea simu zake hali kadhalika sms n.k. Kuwa bize na mambo yako,yape kipaumbele zaid maono yako na hakikisha unayatimiza.
 
your in love with him cha msingi ukubali mapungufu yake na yeye akubal mapungufu yako,kila mtu anamapungufu na strength zake
 
Njoo kwangu kwa siku moja tu utamsahau huyo jamaa wako 4ever ni beep kwenye namba hii 07123456789
 
Kuna kamsemo kanasema, 'in relationship, don't loose your heart, let them loose theirs'.......nadhani wewe ume loose your heart! Imekula kwako mazima hiyo!
 
Ninacho kiona mm hapo wawe bint una mapenzi ya bongofleva yani feki sasa kwataarifa yako zunguka kila mtaa buchani nyama ileile
 

kumbe umezowea kuwabwaga makaka...sasa umepata kiboko yako hahahha
 
kumbe umezowea kuwabwaga makaka...sasa umepata kiboko yako hahahha

sasa wakizingua mie nfanyeje?ukweli mie nkiona tu hapaeleweki huwa sisubiri majanga nawawahi mapemaaaaa, sasa hapa naona panakuwa pagumu ndugu
 
Mmmh.. Hujasema ni mambo gani yanayokufanya udhamirie kumuacha..!!

Nafikiri hayo mambo yanavumilika.... Yangekuwa hayavumiliki ungekuwa umeshamuacha zamaaani na usingerudi nyuma..!!

Msamehe tuu na mvumilie muendelee kuishi vizuri..!!
 
Mrembo wala usitie shaka utaelewa tu. Ukishajua kwa nini mtu anaacha urembo na kuwa kikongwe, basi na hayo mengine ni vivyo hivyo. Huwezi kupata mvuzo bila kukamua muwa kwanza. Tafakali.
 
Shida ya dunia hii mtu hujui nani aliumbwa maalum kwa ajili yako,ndo maana watu wanafikiri kuachana.
::
Tulia,,malipo ya kumuacha utayapata huko utakapoenda.Hakuna mkamilifu,suluhisheni tofauti zenu.
::
Kipya hakinyemi,,na zizi ulilozowea ni bora kuliko dhahabu ya mateso unayotazama nje kabla hujaijua.
=
Kumbuka ni ushauri tu,AMUA, NI MAISHA YAKO.
 

UKWELI LAZIMA USEMWE
Mapenzi ya kweli hapo hayapo, wewe ndio unaye mpenda sana,kwenye mapenzi kuna kuumia na hilo halikwepeki fanya maamuzi mapema,ni vibaya kulazimisha mapenzi. fanya maamuzi sasa japo yata kuumiza lakini itakuwa faida kwako.

usiogope kuumia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…