Serikali isipandishe mishahara!

Hivi tuna tume ya kudhibiti bei ya bidhaa hasa za chakula? kama ipo ina fanya kazi yake sawasawa? maana issue kama unga,mchele,ngano na maharage ambayo ndio chakula kikubwa cha mtz kinapokuwa uncontrolled ndio tunapoumizana ,issue ya mafuta sio kiviiiile maana kuna watu kule vijijini hawategemei mafuta kwa saana,ie mbongo anatumia kuni kutoka porini,mboga anachuma shambani,chumvi anatumiia magadi (kutoka manyara),maji anachota dimbwini,kiangazi anaenda mtoni,taa wakati wa usiku pia sio lazima maana atawasha moto wa kuni...ingawa influence ya kupanda kwa bei za mafuta pia ipo Kama ndo ningekuwa kubwa yao cha kwanza ningeanza kudeal na control of food prices,kwamba bei elekezi iwe affordable kwa kila mwananchi. Lkn pial wachumi wetu nao mbwembwe tu,mm nahisi hawamshauri mkuu accordingly zaidi ya kumpamba na kumsifia au wanasoma upepo wa mkuu anachopenda kusikia huku asilimia kubwa ya watz wakishindia mlo mmoja tena usio kamili.
 
japo sijasoma post yote, naunga mkono hoja. na hapo waTz wote watafaidika badala ya kagurupu kadogo tu kawaTZ wasiozidi mil1

 
Nawashangaa kweli mnavyojihangaisha na kupoteza muda wenu kumsharu JK. Kama tumeshindwa kumuondoa madarakani kwa NGUVU YA UMMA, basi tumuache amalize muda wake, mwenyewe hana analolijua kuhusu uchumi, japo GENTLEMEN YAKE NI YA UCHUMI, anachokijua ni RIDHIWAN AENDESHE BIASHARA ZAKE KWA AMANI na APATE FAIDA, hata kama ni kuiuza nchi hii kwa WACHINA, kikubwa riz1 afanye lolote analoliweza kuongeza faida!!! Bora tujadili namna ya kuiokoa nchi 2015, lakini kwa rais yeyote kutoka ccm 2015, TUTAMKUMBUKA JAKAYA MRISHO KIKWETE, ATAONEKANA KUWA ALIKUWA RAIS BORA KULIKO YEYOTE ALIYEWAHI KUTOKEA, AMINI MANENO HAYA NA CHUKUA HATUA!!!
 
If I were to grade you, your score is 0%
 

Kama kuna ukweli vileee! yes, siumizi tena akili yangu kwa hii serikali
 
Nadhani mtoa hoja una point ktk hili.
Ila napishana na wewe kidogo tu.
unaposema wafanyakazi waitake/waiombe serikali kudhibiti mfumko wa bidhaa nchini.

hilo ni jambo jema, isipokuwa umelitenga kwao tu ili hali ukijua ugumu wa maisha unatuchapa sisi sote.

Iweje leo jukumu la kuibana serikali kufanya yote hayo waachiwe watumishi wa uma pekee?
Unajua fika serikali uliyonayo ni kiziwi hata kwa mambo ya msingi yanayogusa jamii yote.
mfano mzuri ni madai ya madaktari, je unajua mwisho wake?

Kumbe sasa kwa kuwa hawa watu/jamaa ni miungu watu hawataki kusikia wala kuambilika ni vema wananchi wote kwa pamoja tukasimama na kupaza sauti zetu kuieleza serikali ni mambo yapi yaipasa kufanya kwa ajili ya faida ya uma na si kwa ajili ya watu wachache tu, ( that means itafutwe namna ya kufikisha ujumbe kwa pamoja)
Mi nafikiri na niseme tu wafanyakazi (mf. walimu & madaktari) walishafanya mambo mengi ya kudai na kutetea mambo yao lkn pia yakiwa na dhima kuu ya kuwasaidia wananchi wote kwa ujumla bila kupata mass support ( support from ordinary people who own the government in power) na matokeo (impact) yake tunaiona sasa kwa baadhi ya mambo ktk jamii nzima.

Nadhani ni wajibu wa kila mtanzania kuliona hilo na si watumishi wa uma pekee.
 
ndugu huo ndo ukweli wa mambo
 

wakati wa uongozi wa Nyerere serikali iliangalia maisha ya watu wote yaani wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara. Wakati huo ndio sherehe za Mei mosi na saba saba zilikuwa ni sherehe kubwa sana na zilikuwa maarufu sana. Wakati wa Mei mosi wafanyakazi walikuwa wanasherehekea kuongezwa mishahara. Ikifika Saba saba yaani 7/7 ambapo ndio ilikuwa sikukuu ya wakulima wakulima walikuwa wanapewa bei mpya za mazao yao. Wafanyabiashara hawakuwa maarufu sana wakati huo kwani walikuwa kama jamii ya wanyonyaji(ndio maana yakaanzishwa maduka ya ushirika) hivyo walidhitiwa na refa ambaye alikuwa ni tume ya bei. Hivyo wakati huo kila mtu alipata nyongeza.

Hali ya sasa ni tofauti kabisa. Nchi sasa inaongozwa na wafanyabiashara(Ubepari) Ndio wanaoamua hatima ya wafanyakazi na wakulima. Kwa sasa wakulima hawana mtetezi. Wameachwa kama watoto yatima. Wafanyakazi wako chini ya serkali ambayo ndio wafanyabiashara wenyewe. Kwa kuwa wao ndio wanaotawala, ndio wanaoamua mishahara lakini mishahara hiyo inarudi yote huko huko kwa njia ya kodi na kupanda kwa bei za vitu kwa kuwa sasa ni soko huria hivyo hakuna tume ya bei kuwadhibiti. Mfanyakazi anaweza kupata ongezeko la asilimia 50 halafu vitu vikapanda kwa asilimia 60. Hapo atakuwa kapata nini? Hivyo ongezeko lote litarudi kwa wafanyabiashara!

Tatizo kubwa hapa sasa liko kwa wakulima na watu wasio katika sekta rasmi za ajira za mishara. Kupanda kwa mishahara maana yake ni kupanda kwa bei ya kila kitu(Kumbuka nauli zimesha panda kabla hawajapandisha mishahara kama walivyotangaza) Sasa nafuu kidogo itakuwa kwa mfanyakazi. Sasa mkulima na mtu asiye na ajira ya mshahara atamudu vipi kupanda kwa maisha kunakotokana na kuanda kwa mishahara? Njia pekee ya kuwasaida wakulima na wasio na ajira ni kutopandisha mishahara kisha serikali ijitahidi kudhiti mfumuko wa bei na kupunguza kodi kwenye mishahara na bidhaa muhimu kama mafuta na vyakula ili ikibidi bei zishuke. Kwa njia hii itasaidia kupunguza gharama za maisha.
 
Wakati wa uongozi wa Nyerere serikali iliangalia maisha ya watu wote yaani wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara. Wakati huo ndio sherehe za Mei mosi na saba saba zilikuwa ni sherehe kubwa sana na zilikuwa maarufu sana. Wakati wa Mei mosi wafanyakazi walikuwa wanasherehekea kuongezwa mishahara. Ikifika Saba saba yaani 7/7 ambapo ndio ilikuwa sikukuu ya wakulima wakulima walikuwa wanapewa bei mpya za mazao yao. Wafanyabiashara hawakuwa maarufu sana wakati huo kwani walikuwa kama jamii ya wanyonyaji(ndio maana yakaanzishwa maduka ya ushirika) hivyo walidhitiwa na refa ambaye alikuwa ni tume ya bei. Hivyo wakati huo kila mtu alipata nyongeza.

Hali ya sasa ni tofauti kabisa hasa baada ya kuuawa kwa Azimio la Arusha. Nchi sasa inaongozwa na wafanyabiashara(Ubepari) Ndio wanaoamua hatima ya wafanyakazi na wakulima. Viongozi nao sasa sio watumishi wa wananchi tena. Nao sasa ni mabepari, walafi na mafisadi wakubwa. Licha ya kujilimbikizia mali kwa njia haramu, wanajimilikisha hata mali za umma kama walivyojimilikisha nyumba za serikali. Wafanyabiashara ambao zamani wasingethubutu kugombea uongozi wowote, leo ndio viongozi wetu na wanatumi mabilioni kuhahakisha kuwa wanachaguliwa ili waweze kuongoza na kuidhibiti serikali. Chama tawala kilichokuwa ni cha wakulima na wafanyakazi, sasa ni cha wafanyabiashara na viongozi walafi. Nyerere aliishi maisha ya wananchi na alijua taabu na shida ya umasikini hivyo kutumia nguvu zake zote kupambana na umasikini. Hawa wa sasa kwasababu wanaishi maisha ya kibilionea hawajua hata maana ya umasikini. Ndio maana hata wakiulizwa kwanini nchi yako ni masikini, wanasema hawajui. Hii ni kwasababu wao hawaishi katika dunia ya wananchi masikini!

Kwa sasa wakulima hawana mtetezi. Wameachwa kama watoto yatima. Sera na kampeni nyingi za kumwinua mkulima kama kilimo kwanza zimekuwa nyimbo za wanasiasa majukwaani. Hakuna msaada wowote kutoka serikalini ambao wakulima wanaupata. Matrekta wanayoimba, wamepeana tenda za ulaji halafu yanawekwa mapambo mijini. Hata yakifika vijijini si wakulima wengi wanao mudu bei zake. Mkulima amebaki kama mtumwa wa serikali. Akilima kwa jasho lake serikali ndio inayoamua auze au asiuze.Hata wakati mwingine inamlazimisha mkulima kuacha kiasi fulani cha fedha kibaki na serikali eti atapewa baadaye - stakabadhi gharani! Wakati bei ya soko ni nzuri mkulima anapigwa marufuku kuuza kwa kisingizio cha kuzuia njaa wilayani au mkoani kana kwamba mkulima alipewa mtaji, mbegu na gharama za kilimo na serikali. Soko likiwa zuri nje ya nchi haruhusiwa kupeleka mazao yake kule ili apate kurudisha gharama zake na faida kidogo, serikali inapiga marufuku. wakati huo ndiyo inajifanya kumtetea mkulima.Wakati anahanganika na jembe la mkono, viongozi wananunua mashangingi(makilimo kwanza)Wafugaji wamebaki kama watumwa au wakimbizi pia. Kila mahali wanaambiwa wavamizi waondoke. Serikali haiwajali. Badala ya kuwapa elimu ya kuongeza ubora na uwingi wa mifugo yao, wanaambiwa wapunguze mifugo wakati ndio utajiri wao. Lakini serikali haijawahi kuwaambia wafanyabiashara mfano wenye magari mengi wapunguze magari yao au wenye maduka mengi wapungueze maduka yao. kwasababu huko ndiko wanakochukuwa kodi za moja kwa moja za kuendesha serikali.

Wafanyakazi wako chini ya serkali ambayo ndio wafanyabiashara wenyewe. Kwa kuwa wao ndio wanaotawala, ndio wanaoamua mishahara lakini mishahara hiyo inarudi yote huko huko kwa njia ya kodi na kupanda kwa bei za vitu. kwa kuwa sasa ni soko huria hivyo hakuna tume ya bei kuwadhibiti. Mfanyakazi anaweza kupata ongezeko la asilimia 50 halafu vitu vikapanda kwa asilimia 60. Hapo atakuwa kapata nini? Hivyo ongezeko lote litarudi kwa wafanyabiashara na serikali yenyewe!Katika hali hiyo mkulima atakuwa wapi wakati hapati ongezeko lolote katika mazao yake, tena labda wakati mfanyakazai anaongezewa yeye ndio kwanza analima au mazao hayajakomaa! Atafidiaje gharama za kupanda kwa pembejeo kama mbole kutokana na kupanda kwa gharama za usafiri? Nayasema haya nikiwaonea huruma sana wakulima na watu wasio katika sekta rasmi ya kulipwa mishahara. Mimi nimeajiriwa napata mshahara lakini kwa uzoefu mshahara wangu ulikuwa na thamani kubwa sana wakati wa kipindi cha Mkapa ambapo mzee yule alijitahidi sana kushusha mfumuko wa bei na kuuthibiti bila kuongeza mishahara mara kwa mara. Mtu anaweza tu kufanya hesabu ndogo tu kwa kuangalia bei ya uniti moja ya umeme wakati wa Mkapa na bei ya uniti hiyo hiyo wakati huu wa ''CHAGUO LA MUNGU!''

Tatizo kubwa hapa sasa liko kwa wakulima na watu wasio katika sekta rasmi za ajira za mishara. Kupanda kwa mishahara maana yake ni kupanda kwa bei ya kila kitu(Kumbuka nauli zimesha panda kabla hawajapandisha mishahara kama walivyotangaza) Sasa nafuu kidogo itakuwa kwa mfanyakazi. Sasa mkulima na mtu asiye na ajira ya mshahara atamudu vipi kupanda kwa maisha kunakotokana na kuanda kwa mishahara? Njia pekee ya kuwasaida wakulima na wasio na ajira ni kutopandisha mishahara kisha serikali ijitahidi kudhiti mfumuko wa bei na kupunguza kodi kwenye mishahara na bidhaa muhimu kama mafuta na vyakula ili ikibidi bei zishuke. Kwa njia hii itasaidia kupunguza gharama za maisha na hivyo ni kama serikali itakuwa imewaongezea mshahara wananchi wote. Kwa sasa serikali ifute uamuzi wake wa kuongeza bei za nauli na kama ni kuwasaidia wafanyabiashara ya usafiri basi ipunguze kodi kwenye mafuta ili nauli zishuke. Kinyume cha hapo hata kama serikali ikitangaza kupandisha mishahara kwa asilimia mia tano au elfu bado hakutakuwa na nafuu yoyote kwani uzoefu unaonesha hivyo.
Ukifanya utafiti utagundua kuwa mtu aliyelipwa mshahara miaka ya sabini, mshahara wake unawezakuwa ni mkubwa kuliko wa anayelipwa sasa hasa kama utabadilisha mshahara huo katika mfumo wa dola ambayo ndiyo pesa inayotawala uchumi wa dunia. Hii ni kwasababu kwa pesa yetu, kupanda kwa mishahara maana yake ni kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola.

Naomba kutoa hoja!
 
kweli mishahara ikipanda na vitu vingine vinapanda na hivo maana ya kupandisha inapotea. bei za vitu zidhibitiwe. hoja yako nzuri sana
 

Wakuu!

Mie mwenzenu nawashangaa kwa kupoteza muda wenu eti kujadili kama hii!! Kwa serikali hii iliyo kauka kama KAMBALE!!!
 
Kwenye mada za muhimu kama hizi watu kama lukosi,nape na wengine wa aina yao huwezi kuwaona wakikoment
 
yeah hilo ndilo suluhisho la kuleta unafuu katika maisha ya wananchi wa kawaida tanzania yaani kudhibiti mfumuko wa bei na kupunguza viwango vya kodi katika maeneo muhimu lakini hilo pekee halitoshi bila ya serikali na bunge kuwa siriazi katika suala la matumizi,matumizi ndio yanayoleta au kutoleta mfumuko wa bei,matumizi ya serikali hii iliyoko madarakani ni makubwa mno tena yanaelekezwa katika maeneo yasiyo na tija katika uzalishaji na ukuzaji wa pato la taifa badala yake yanaelekezwa zaidi katika anasa.mfumo wetu wa serikali kuwa kubwa mno na kujilimbikizia mamlaka na madaraka katika maeneo mbalimbali ya kibiashara,kiutawala na ya kiserikali pia unachangia matumizi makubwa ya serikali,hapa ndipo ninapoona umuhimu wa utawala wa majimbo utakaopelekea uundwaji wa serikali ndogo ya kitaifa itakayopunguza kwa kiwango kikubwa haya matumizi makubwa tunayoshuhudia sasa.na mbaya zaidi ni huu mtazamo wao kwamba serikali ndio suluhisho la kitu.
 

Hapo umeongea mkuu, mm nichoamin katu hakuna kiongoz wa juu mwenye roho nzur kias kwamba atufikirie sisi wa hali ya chini. Mkapa nilimchukia kwa kupora rasilimali na kuingia mikataba tata lakin huyu jamaa naamin ni mfanyabiashara mkubwa saaaana kitu ambacho nihatar na isije tokea tena mara nyingine kumchagua mtu wa aina hii maana tutauzwa jumla jumla. Ile miaka mitano ya awali ilitosha kutambua tunakopelekwa lakin wadanganyika tumekuwa wazito kufanya maamuz. Ni hayo tu

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…