Mungu ni mkubwa watoto wanne kwa mpigo kisha wanaume wawili na wanawake wawili.
Nafikiri kwa maisha yetu ya sasa hapo inatosha haitaji tena watoto kama wanaume unao, kama wanawake unao pia - upewe nini tena.
Na baba wa watoto sijui yuko wapi sasa kwa kweli huyu bibie anahitaji msaada wa hali ya juu, hili nalo linazidi kuwa tatizo sasa hivi linapokuja swala la ulezi kwenye kushika ujauzito wanashirikiana ikitokea ujauzito na baada ya kujifungua wanaume hatuonekani.
Kwa kweli inabidi tujifundishe hapa sio mambo ya kukimbiana baada ya kumpa ujauzito binti wa watu, hili swala wanaume linatuhusu sana.
Namalizia kwa kumpa pole na hongera pia