Mkuu Bepari, kwanza kabisa niombe radhi kwa Lugha niliyotumia...haikuwa na staha, am sorry! ila tuna changamoto nyingi sana katika sekta ya Afya hususani kwa wataalam (madaktari). vifo vingi vinachangiwa na negligence ya watabibu na hivyo kufanya Hospital za serikali kuonekana siyo salama tena. Haijaanza leo wala jana, nafikiri tatizo ni la kimfumo zaidi. kwa mtu niliyezoea huduma za first class kutika hospitali za first world, ukinileta kwenye hospital hizi za daktari kwenda kunywa chai anawaacha wagonjwa kwenye foleni....sizani kama nitamudu na haitowezekana..Madaktari vilaza na mbumbumbu? Watch out your word nigga.
you have a point! sijui kama nitaeleweka ila the way i view it, kuna sababu nyingi na ningependa nieleze kwa kifupi;-Unachosema ni sawa lakini hoja muhimu hapa ni unaenda kutibiwa huko unakoenda kwa Gharama za nani? Kama ni hela zako sawa, Ila kwa hela za serikali HAPANA.
mkuu, nimefurahi umenikumbusha kitabu cha Animal Farm by George Orwell. nimekisoma mwaka 1991 na mpaka leo ninacho kwenye Library yangu. Tofauti yangu na mwandishi Orwell, yeye aliandika kwa kukata tamaa na akijikita kwenye kushauri zaidi. Orwell hakuweza kuzingatia jinsi watu wanavyofikiria, na kwa nini walifanya yale waliyoyakusudia...kitabu cha animal Farm kililenga kujadili matatizo na nguvu za kisiasa, huku wenye nguvu na wenye mamlaka ya kisiasa wakipambana kubakia madarakani na kuwaangamiza wale wote wanaowapinga...(kwa mazingira ya sasa, tunaweza sema wapinzani wanavyoonewa na serikali ya awamu ya 5). Ingawa kitabu hicho kinaweza reflect hali ya kisiasa ya sasa kwa nchi kama Tanzania, lakini relevancy yake haikuwa positive mpaka dikteta uchwara alipoingia madarakani....Mkuu sio wazembe hawawezi.Ni trend ambayo ipo ktk DNA na ndio gap kati yetu na wenzetu wenye fikra huru.lazima tusinzie ktk kitabu,tukijipa moyo tutaendelea kesho au mwingine atatuhadithia.Hata maprof wet ni vilaza sana.Hawasomi concepts vizuri ktk reference zao.Wengi tuu hata km huna level yao ya elimu ukiwashika na kuwapa maswali ktk fair ground (Mahali hawana wa kuwalinda na kukunyamzisha). Utawaonea huruma.Ndio hao Lissue anawatubua kila mahali. Ndio maana NAKIHESHIMU SANA KITABU CHA ANIMAL FARM kina miaka zaidi ya 40.Ila kinaishia Africa ya leo na ile ya Baada ya uhuru.
Mkuu Bepari, kwanza kabisa niombe radhi kwa Lugha niliyotumia...haikuwa na staha, am sorry! ila tuna changamoto nyingi sana katika sekta ya Afya hususani kwa wataalam (madaktari). vifo vingi vinachangiwa na negligence ya watabibu na hivyo kufanya Hospital za serikali kuonekana siyo salama tena. Haijaanza leo wala jana, nafikiri tatizo ni la kimfumo zaidi. kwa mtu niliyezoea huduma za first class kutika hospitali za first world, ukinileta kwenye hospital hizi za daktari kwenda kunywa chai anawaacha wagonjwa kwenye foleni....sizani kama nitamudu na haitowezekana..
Siku zote nitawatetea madaktari na manesi. Obovu wa huduma za afya hausababishwi na wauguzi wala madaktari kwani hao ni watoa huduma tu. Nimekaa moja ya tertiary hospital hapa nchini wodi ya wazazi mnaingia nurses wanne, wasaidizi wawili, madaktari wawili na wafanyakazi katika idara zingine kama medical records na IPC wakiingia wodini na kutoka. Nimeshuhudia wazazi tukiwahudumia vizuri sijawahi ona! Kwa sasa nipo health center ambayo iko busy na wodi ya wazazi iko busy kama ya ile ya tertiary hospital lakini balaa ni kuwa kazi tulikuwa tukifanya watu sita kule tertiary hospital huku health center tunafanya wawili!! Sasa ukisikia mgonjwa kawa harassed utashangaa? Kwa nini kule kwa tertiary hospital wagonjwa hawawi harassed? Ni vyema kutambua nurse patient ratio tulonayo ni kubwa mno na ni hatari kwa afya za watanzania.you have a point! sijui kama nitaeleweka ila the way i view it, kuna sababu nyingi na ningependa nieleze kwa kifupi;-
- Mosi, viongozi wa kiafrika wameshindwa kutengeneza mazingira na miundominu katika sekta ya afya ili kulingana na ile ya Dunia ya kwanza kwa sababu ya ufinyu wa rasilimali (poverty) na maalifa (knowledge). Nchi kama Tanzania bado tuko wachanga mno kwenye utaalamu na technology kulinganisha na wenzetu. Ukiangalia almost mashine kubwa kwa ajili ya vipimo vikubwa tumepewa kama msaada kutoka nchi wahisani. hali kadhalika, tunasaidiwa karibia 50% ya ujenzi wa mahospitali na dawa....je tutaanzaje kulingana na hao wenzetu?
- Nchi za kiafrika zinafanana kwa umaskini. kama siyo wa mali basi utakuwa wa maarifa (Ignorance). tuna matatizo mengi sana na hatuwezi kuyapatia ufumbuzi, siyo leo wala kesho. kwa mfano, Daktari hana time na wagonjwa...Nesi naye anawaharasi wagonjwa kwa kejeli na vijembe....(huko kwenye wodi za wazazi)...mwalimu naye hana time na wanafunzi wake...hata wakifeli...hayamhusu! askari naye barabarani...anakubambikizia kosa, anakuandikia notification ya 200,000/- ukishindwa kulipa...ndo furaha yake! mkuu, labda turudi kwenye zama za Nuhu...tuangamize kizazi chote na tuanze upya!
- Naamini kuna utaratibu ama wa kisheria or Regulations zinazotoa haki na fursa kwa viongozi kwenda kutibiwa nje. matarajio ikiwa ni kuona wanapona na kurudi kwenye kulitumikia Taifa. Binafsi kwenye Afya, sina hiyana...acha watibiwe. kuna hata watu binafsi wanatibiwa kwa msaada wa serikali (Kodi ya wananchi)....
Kwanini badala ya kununua mashangingi ya bei kubwa wasinunue just simple transport na pesa wawekeze kwenye hospitali hata ikiwezekana kuwa tunaagiza watalaam kuja kufanya hizo surgery hapa kwetu? Dr. mmoja akija atapewa accomodation lakini anaweza okoa maisha ya watu hamsini kwa mwezi kuliko wanasiasa kutumia pesa nyingi na wasaidizi juu ili kutibu mtu mmoja.mkuu, ishu siyo hospital ,kama majengo na mashine...NO! Hapa naangalia issue ya wataalam na uwezo wao wa kutibu magonjwa makubwa kama kidney transplant etc. Jiulize kwa Mfano, karibia asilimia 58% ya budget ya serikali ya mwaka inatoka kwa nchi wahisani. je hizo hospital za kiwango kama ujerumani, London or USA tutazijenga kwa kutumia rasilimali ipi? vipi kuhusu madaktari wetu vilaza wasiojali uhai wa mtu na umbumbumbu wao kwenye tiba?
Andiko hili mejitahidi sana kujieleza, post ya mwanzo ilikusaliti. Nyerere hakuwa Makini kwa maelezo yake dhidi ya makabila aliyoayaona kuwa makubwa.Pia ujamaa uliprogram watu kuchukia utajiri na matajiri.Ingawa Nyerere alijua wajamaa walikuwa wajinga sana kiasi ch akushindwa hata muelewa yeye mwenyewe,bado aliendelea wapa hotuba zenye kuhitaji akili na maadili.Nimekusoma mkuu! kwanza kabisa mimi siyo beneficiary katika mgongo wa ukabila na haitokuja kutokea kwangu wala kwa kizazi changu. Never! ninafanya kazi kwa kujituma na nikipambana na hali yangu (msemo mpya huko tz). Tanzania ya leo ni tofauti na ile ya 70's na 80's na hali kadhalika jamii nayo imepoteza uhalisia na maadili ya kitanzania nayo yamewekwa rehani. Kasumba ya kwamba watu kutoka ukanda fulani hawafai kuongoza imeanzishwa na nyinyi wenyewe( wananchi)....inawezekana ukawa hujahusika lakini jirani yako ama kiongozi wako uliyempigia kura akawa ndo ana-engineer hizo movements. je wewe kama Mtanzania ulifanya nini kuondoa hizo impunity? ilianza kwamba wahaya hawafai kuongoza nchi, na kweli walibaniwa mpaka leo. sasa imewakumba watu wa kaskazini kwamba hawafai kuongoza.....kwani kosa la watu wa kaskazini na wahaya ni lipi? kwa ufupi huo ni ukabila uliozungumzia hapo juu. Mwl. nyerere alisema, ukabila ni kama kula nyama ya mtu...ukianza huwezi kuacha!
Bila kuathiri sheria na taratibu nyinginezo, jamii yetu ndo mwasisi wa matatizo yanayotokea leo. kuna jamii inayotaka maendeleo especially kwa kujibidiisha na kutafuta mali mchana na usiku na kuna jamii ya kijiweni ambayo kila akipita mwenye nacho, basi wao wana-conclude kuwa amewaibia. Siyo kila mwenye nacho, basi amewaibia watu wengine....(inawezekana ila siamini hivyo). Ni wajibu wa serikali kuwatumikia watu wake, lakini wananchi nao wawe na sitaha kwa kuheshimu utu watu wengine.....! hata akili za Magufuli ziko hivyo, hataki aone watu wakipata ahueni ya maisha or kutajirika...anaamini kila mtu ni mpiga dili....Lakini, kwa busara tu za kijiweni...huwezi kutajirika kwa kumchukia tajiri...
Mkuu watu husoma kitabu kimoja au kwenda shule moja ila matokeo kuwa toauti sana. Well hii ni tafsiri yako.Ila yangu ni kwamba sijaona wapi African Countries wametoka nje ya hicho kitabu. Tunachoweza jadili hapa ni power ya ujamaa kustamp patterns hatari ktk maisha na kili za wajamaa.Kutoaminiana ni kukubwa sana ingawa hawachoki jisifia kwa maadili,utu, uaminifu.Wajamaa hawakosi wa kumshutumu km kibaraka au adui wa taifa. Hakuna tofauti sana na kambi ya magaidi.mkuu, nimefurahi umenikumbusha kitabu cha Animal Farm by George Orwell. nimekisoma mwaka 1991 na mpaka leo ninacho kwenye Library yangu. Tofauti yangu na mwandishi Orwell, yeye aliandika kwa kukata tamaa na akijikita kwenye kushauri zaidi. Orwell hakuweza kuzingatia jinsi watu wanavyofikiria, na kwa nini walifanya yale waliyoyakusudia...kitabu cha animal Farm kililenga kujadili matatizo na nguvu za kisiasa, huku wenye nguvu na wenye mamlaka ya kisiasa wakipambana kubakia madarakani na kuwaangamiza wale wote wanaowapinga...(kwa mazingira ya sasa, tunaweza sema wapinzani wanavyoonewa na serikali ya awamu ya 5). Ingawa kitabu hicho kinaweza reflect hali ya kisiasa ya sasa kwa nchi kama Tanzania, lakini relevancy yake haikuwa positive mpaka dikteta uchwara alipoingia madarakani....
uko sahihi mkuu. ila changamoto ni nyingi hususani miundombinu zetu ambazo siyo rafiki na ndiyo maana serikali imebaki kuwa muumini wa mashangingi.kuna kipindi waziri mkuu (mizengo Pinda as he then was) aliwahi kulitolea ufafanuzi kuhusu serikali kuendelea kutumia mashangingi. Pili, Ningependa kufuta kauli kuhusu madaktari kuwa vilaza. Other thing, Nimewahi kupitia hali wanayopitia vijana wengi wa Kitanzania kwani nami nimewahi kulitumikia Taifa kwa hali na mali, ila nilikuja kuwa disappointed na mambo kadha wa kadhaa...nikaamua kuachana na govt na kufanya mambo mengine. kwa kifupi, Taifa la Tanzania huwezi kuendelea or kupata vyeo vikubwa serikalini bila kuwa mnafiki. jaribu kuchunguza! kuhusu mtu anaumwa jino na anaenda ujerumani, majibu yake yanaweza kuwa mtambuka...ila sababu kubwa ni wataalamu tulio nao wana-abuse taaluma zao na hivyo kufanya wadharaulike na hivyo watu wana opt sehemu ambayo watapata huduma nzuri. wengi wanapenda kwenda Ujerumani or India kwa sababu ya Huduma wanazopata huko ni bora. hujajiuliza kwa nini performance ya Daktari akiwa kwenye Govt hospital na private hospital ni tofauti? Lastly, issue kuhusu kununua magari ya washawasha na ndege za kivita mbazo zitaisha muda wake bila kupigana? nafikiri jibu lake ni simple kuwa usalama kwanza. kwenye issue ya security, elimu na mengineyo comes later. huwezi jua adui atakuja lini kukuchokoza..you have to stay awake!Kwanini badala ya kununua mashangingi ya bei kubwa wasinunue just simple transport na pesa wawekeze kwenye hospitali hata ikiwezekana kuwa tunaagiza watalaam kuja kufanya hizo surgery hapa kwetu? Dr. mmoja akija atapewa accomodation lakini anaweza okoa maisha ya watu hamsini kwa mwezi kuliko wanasiasa kutumia pesa nyingi na wasaidizi juu ili kutibu mtu mmoja.
Je, kweli madaktari wetu ni vilaza au wanafanywa hivyo? Kama kuna kijana ambaye ni mzuri kwa nini serikali ikamsomesha mahali ambapo akirudi ataokoa maisha ya watu wengi kuliko kuwa tunatumia pesa nyingi kupeleka watu India?
Ukweli viongozi wetu wanaabuse hilo. Mtu anashida ya meno anakwenda Germany wakati kuna private hosp. Dar zina wataalamu toka huko?
Tutumie pesa ambazo tunapoteza kununua washa washa zinazotumika kwa ajili ya upinzani na ndege za kivita ambazo zitaisha muda wake bila kupigana, tuelekeze nguvu kwenye afya na elimu ambayo inawafanya viongozi wetu wasepe nje.
Uende kwa fedha zakoMleta thread, acha wivu. kwenye kuumwa, haijalishi ni wapi na ni nani, lazima mtu ukajitibie unapoona panafaa na penye huduma za afya nzuri. hata mimi nikiumwa siendi Muhimbili wala amana, naenda sehemu yenye hazi yangu.
Magufuli alipoingia madarakani alitimua mkurugenzi Muhimbili....Wapinzani wakaanza kulia kuwa hajafuata taratibu.Moja kati ya aibu kubwa kabisa za Tanzania ni kwamba tunayemuita "Baba wa Taifa" alizaliwa Butiama, aliipenda sana nchi yake akaishi Tanzania miaka yote, lakini alipoumwa kulikuwa hakuna hospitali ya kumpeleka Tanzania mpaka akapelekwa Uingereza na kufia huko.
Hii si aibu tu, ni jambo la kuhatarisha Usalama wa Taifa.
Kama hatuna hospitali za kukidhi viwango fulani nchini, hawa viongozi wanaoanzisha vita za kiuchumi na mataifa makubwa wakiumwa na kupelekwa hospitali za nje, tutajuaje kwamba hawawezi kuwekewa vitu vibaya vya kuwaua katika miili yao?
Magufuli alipoingia madarakani alitimua mkurugenzi Muhimbili....Wapinzani wakaanza kulia kuwa hajafuata taratibu.
Pia alichukua hela ya sherehe za bunge akanunulia vitanda chadema wakasema hajafuata taratibu.
Dawa ni moja tu....kupiga marufuku matibabu nje ya nchi kwa fedha ya umma.