Nimekuwa nikisikiliza mazungumzo ya watu wengi na hasa wanawake wakiongelea kitu kiitwacho "reception" ama sura.Wamekuwa wakizitunza kwa gharama kubwa sana sura zao na wakati mwingine wamekuwa wakisema usiniharibu reception nisije nikawa sifuatwi na wanaume nk.
Lakini leo nawaletea ka utafiti nilikokafanya mwenyewe kwa muda mrefu. Kwamba mwanamke aweza kuwa anakuja kutokea mbele kisha akatokea kwenye kundi la wanaume. Wakishamwona amejitokeza mbele yao wanaume wote huinamisha vichwa chini ama huangalia pembeni yaani huwa hawamwangalii usoni.
Lakini akishawapita wanaume hao watamwangalia mpaka atakapopotelea yaani upeo wa macho yao yatakapoacha kumwona. Halafu wakati keshawapita utawaona wakimsifia uzuri wake sana.Lakini wakati akija kwa mbele hawakuwa wakimsifia mpaka alipowapita.
Sasa na mimi nawauliza na ninyi je reception ya mwanamke ipo mbele ama nyuma?
Neno reception ni mapokezi, unapozungumzia mapokezi hapo itakuwa ni mbele na obvious usoni!! Mpangilio wa sura na tabasamu linapokuvuta hiyo ndiyo maana halisi ya mapokezi!!
Uzuri wa mwanamke bana kila mwanaume ana yake!! Wengine wanampenda mwanamke sababu ya dental formula ilivyokaa tu, mengine hayaangaliwi. Mwingine atapenda macho, miguu, lips,dimples, makalio, sura, na n.k!!
Na ndiyo maana hakuna mwanamke anayekosa mwanaume! Hata kwako awe mbaya vipi lakini kuna mwanaume mwenzio ananyanyasika na penzi la huyo huyo mbaya mpaka unashangaa!
Nadhani kwa hali hiyo basi, uzuri wa mwanamke maana yake upo kwenye moyo wa mwanaume coz yeye anakuta moyo wake umevutika tu jambo fulani kwa mwanamke si lazima takko au sura!