Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ameshiriki katika dua maalum ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo ilifanyika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo yake, amesema dua hiyo ni kwa ajili ya kumkinga na shari Rais Dkt. Samia kwa sababu Rais amefanya mengi ikiwemo kuleta neema, kutuletea maendeleo na kutuletea maisha mazuri.
Dua hiyo imeongozwa na Mufti Mkuu wa Tanzania ambapo pia watoto yatima walishiriki dua hiyo pamoja na kupata iftar iliyoandaliwa na ofisi ya Meya wa Jiji la Dar es Salaam.