Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kusimamia kukamilika kwa ujenzi wa tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mkoani Kagera, ambalo limefikia asilimia 70 ya utekelezaji. Amesema, iwapo ataendelea kuaminiwa kuongoza serikali, atahakikisha chuo hicho kinakamilika na kuanza kutoa huduma ili kuwanufaisha wananchi wa Kanda ya Ziwa kupata elimu ya juu kwa urahisi zaidi.
Dkt. Samia ametoa kauli hiyo Alhamisi, Oktoba 16, 2025, wakati akizungumza na maelfu ya wananchi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Kaitaba, Bukoba Mjini, mkoani Kagera.